Kanuni zavunjwa tena Arusha...hii ndiyo bongoland.

Ukisusa wenzio wala siungi mkono ususiaji wa madiwani wa CHADEMA katika masuala muhimu nadhani dhani nzima ya ususiaji inakosa maana kabisa.Bejeti itagusa maeneo nyeti kama Hospital,elimu,ujenzi wa barabara na nk ukisusa maana yake shughuli zote hizo zisimamishwe kisa unataka nafasi ya umeya.

CHADEMA wananchi wanajua hila na ghiliba za uchaguzi wa Meya wa jiji la Arusha kususia sidhani kama ni jambo muhimu kwa wakati huu.Zipo mahakama kwanini hamataki kwenda huko.Shughuli za maendeleo lazima zienziwe na madiwani wote wa CHADEMA na CCM na vyama vingine vyote,Tanzania ni kubwa kuliko vyama vyenu.
 
Tunaomba ufafanuzi wa hili kutoka Chadema Makao makuu, kwa nini waingie wajiorozeshe halafu watoke nje, nafikiri wangetakiwa kutofika kabisa ili idadi isifike na kutoa hoja zao kupitia media ili sisi tunaowamini tuwaelewe lakini kwa hili, nahitaji kuelimishwa na wakubwa ni kwanini wamefanya hivyo na lengo lilikuwa nini, na hata kama wangebaki na kupiga kura ya kutopitisha je sheria inasemaje wengi wameshinda au mpaka idadi ifikie pia.

Na kwa taarifa nilizo nazo kuwa jamaa baada ya kutoka walirudi baadae kuchukua bahasha zao za posho, kweli hawa jamaa njaa kali
 
hao kama wamefika wakajiorodhesha wamukalia Ndugu zanguni ..
Kwanza niwapuuzi kabisa mnasema amhudhurii alafu unakwenda unatka nje Meya fanya kazi achana na hawa pumba UPINZANI LAZIMA MUWE NA UHAKIKA MNACHOKIFANYA ...


Mkuu Piddy wanatuzuga hawa kanuni hiyo hiyo CCM waliitumia kuchagua meya sasa iweje leo wanasema hawajui/wamesahau.
 
Na kwa taarifa nilizo nazo kuwa jamaa baada ya kutoka walirudi baadae kuchukua bahasha zao za posho, kweli hawa jamaa njaa kali

Usisahau watu walikufa majeneza yakabebwa mwisho wa siku utagundua wanasiasa wanaangalia matumbo yao.
 
Waliingia kuonesha dhamili zao za kuwatumikia wana wa arusha. Walitoka mara baada ya anayeitwa meya kusimama kuonesha hawamtambui kama meya halali wa arusha. Mmeelewa???

Kawadanganye machaliii.
 
CDM kuna machizi wengi duuh! Wanaandikisha majina kisha wanafufuta kwa peni? Hiyo kali!!!!!!!!!!!!!!
 
Cdm wanaboa na wanajijua kwamba wanafanya ujinga, na kamwe jamii haiwezi kuwaelewa.
Kikao cha madiwani ni cha muimu sana kwa ajili ya maamuzi juu ya maendleo ya wananchi,
kuonesha ujinga wameingia wakasaini ili kutimiza idadi alafu wanatoka,.
Au kutoka nje ya vikao ni moja ya sera ya chama chao? Maana haya matukio yanatia kichefuchefu sasa.
 
Mimi naunga mkono CDM kupinga meya lakini hili la kususia bajeti naona hawajewatendea watu wa ARS haki. Pili kisheria corum inategemea attendence register of which walisaini kuingia hata kama walitoka baadaye haijalishi. hivyo kwa hapo wamechemka..
 
Cdm wanaboa na wanajijua kwamba wanafanya ujinga, na kamwe jamii haiwezi kuwaelewa.
Kikao cha madiwani ni cha muimu sana kwa ajili ya maamuzi juu ya maendleo ya wananchi,
kuonesha ujinga wameingia wakasaini ili kutimiza idadi alafu wanatoka,.
Au kutoka nje ya vikao ni moja ya sera ya chama chao? Maana haya matukio yanatia kichefuchefu sasa.

Mkuu BCR kuna jambo umesahau kusema walirejea kuchukua posho ukisusa susia na posho.Ngoja waje manazi utashagaa jinsiwatakavyotetea upuuzi.
 
Naunga mkono. CCM ndiyo wenyewe kwa kupindisha kanuni ili mambo yao yaende. Na mara nyingine hutumia ubabe. Huyo meya ni wa kuchakachuliwa -- hamlisemi hili -- mnakalia tu eti madiwani CDM walifuta majina, mara kile. Cha msingi kwamba Meya huyo ni wa kuchakachua hamsemi.

Nyie wote mnaopinga hatua ya madiwani wa CDM ni watu wa ajabu kweli kweli. Hiyo CCM yenu itakuwa inavurunda mambo hadi lini? haidhuru sasa kwa kuwa gamba linatoka, labda mivurundo ya kanuni na sheria itakoma, na haki na utawala bora kutawala! Lakini itachukuwa muda! Maana mzoea vya kunyonga vya kuchinja haviwezi.
 
Hongereni sanaaaaa madiwani wa CDM! Lazima CCM wajuwe kwamba hawawezi wakafanya mambo kwa kupindisha kanuni zilizowekwa! Majimbo mengi ya uchaguzi walipindisha sheria na kanuni kwa kutumia NEC yao ili washinde! hawakushinda chochote -- wizi mtupu!

Makinda wao huko Bungeni kazi yake kubwa naye ni kupindisha tu kanuni. CDM lazima ikae imara kwa manufaa ya utawala bora -- msisikie visingizio eti wananchi watakosa huduma kwa kukosa bajeti. Bajeti gani iwapo nusu ya hela za bajeti huibiwa na watu wa CCM?

Uzi ule ule hadi kieleweke.
 
Naona vijana walio dodoma wameamua kuleta vichefuchefu vyao vya ccm humu...

mlidiscuss na hili swala la cdm huko? tujuzeni.

Ila kuhusu kwanini cdm wamefanya mtaelekezwa, maana najua ugonjwa wenu 'inferiority complex' hamlali mpaka mjue cdm anafikiria nn!
 
Hongereni sanaaaaa madiwani wa CDM! Lazima CCM wajuwe kwamba hawawezi wakafanya mambo kwa kupindisha kanuni zilizowekwa! Majimbo mengi ya uchaguzi walipindisha sheria na kanuni kwa kutumia NEC yao ili washinde! hawakushinda chochote -- wizi mtupu!

Makinda wao huko Bungeni kazi yake kubwa naye ni kupindisha tu kanuni. CDM lazima ikae imara kwa manufaa ya utawala bora -- msisikie visingizio eti wananchi watakosa huduma kwa kukosa bajeti. Bajeti gani iwapo nusu ya hela za bajeti huibiwa na watu wa CCM?

Uzi ule ule hadi kieleweke.


Sawa kabisa Mkuu. Kufuata kanuni (na siyo amri -- yaani kutii amri) ndiyo kitu cha msingi cha utawala bora popote duniani. CCM wamezoea sana kufanya mambo ya 'bora twende'. Hatutaki tena.
 
Naona vijana walio dodoma wameamua kuleta vichefuchefu vyao vya ccm humu...

mlidiscuss na hili swala la cdm huko? tujuzeni.

Ila kuhusu kwanini cdm wamefanya mtaelekezwa, maana najua ugonjwa wenu 'inferiority complex' hamlali mpaka mjue cdm anafikiria nn!

Wameambiwa wakaanzishe forum yao, na waachane na hii JF kwani imesemwa kuwa ni ya Chadema! Kama kutetea mafisadi wao, au kushabikia uvunjaji wa kanuni basi hayo wayapeleke huko huko.
 
Yaani Meya wa kuchakachuwa bado anakuwa na jeuri ya kupindisha kanuni ya quorum? Kweli CCM bado ina matatizo makubwa. Bravo CDM -- enedeleeni kuwakumbusha hao vilaza!
 
hao kama wamefika wakajiorodhesha wamukalia Ndugu zanguni ..
Kwanza niwapuuzi kabisa mnasema amhudhurii alafu unakwenda unatka nje Meya fanya kazi achana na hawa pumba UPINZANI LAZIMA MUWE NA UHAKIKA MNACHOKIFANYA ...


Hawakuwepo wakati agenda ya Bajeti inapojadiliwa. Hivyo, hawakushiriki katika kuijadili na hawakupiga kura katika kuipitisha. Iweje kuandika jina ndiyo kupitisha bajeti?
 
Wameambiwa wakaanzishe forum yao, na waachane na hii JF kwani imesemwa kuwa ni ya Chadema! Kama kutetea mafisadi wao, au kushabikia uvunjaji wa kanuni basi hayo wayapeleke huko huko.

si wanataka watu wa mawazo mgando, mbona forum zipo nyingi tu, tumejisajili JF wenyewe--kwamba tumeikubali na misingi yake+ubora.

Iweje hili la kuhusu forum liwe dili leo?

wako huko dodoma wanavimbiwa matumbo, hata hawafikiriii kwa vichwa vyao. Hata wakiongea pumba wanakubaliana tu
 
Lazima ieleweke kuwa CDM wangekuwa wasaliti zaidi kama wasingehudhuria kikao kile kwani walichaguliwa ili kuwakilisha wananchi katika vikao.
*KUHUDHURIA ni suala moja na KUPITISHA BAJETI ni suala lingine ambalo linahitaji KUPIGIWA KURA.na madiwani wote waliohudhuria.
*CCM ilikuwa lazima wachakachuwe hii kwa sababu ndio INAWARUHUSU KUANZA ULAJI WA MAFUNGU HUSIKA YA FWEZA....suala ambalo ndio ajenda yao rasmi kitaifa.
 
Kuna kususia lakini hili la Bajeti halikuhitaji kususiwa - kuna hospitali, mashule, kazi za usafi zote zinategemea bajeti hii ya manispaa.

Huwezi kuvunja sheria eti kwa sababu kuna mashule au manispaa. Kiini cha tatizo hili ni uvunjwaji wa sheria, kuna umuhimu gani wa hizo sheria kuwepo? Ni vizuri hizo sheria ziondolewe kisha waendelee kutoa maamuzi wayapendayo. Lakini nchi hii na hususani Jiji la Arusha linatakiwa kuendeshwa kwa utawala wa sheria na si kwa mapenzi ya kundi fulani.
 
walioshiriki kwenye kupiga kura ndio wanaopaswa kutimiza quoram na siyo kila atakaesaini kitabu basi ameshiriki kupitishwa bajeti na ndio maana mara kwanza ilishindikana kwa sababu hakukuwa na wajumbe wa kutosha ktk kupiga kura.
 
Back
Top Bottom