Elections 2010 Kanuni za Uchaguzi 2010 na mgogoro wa Sheria ya Gharama

Status
Not open for further replies.
Ndio maana wabunge walikuwa wanaipinga hii sheria!
Mbunge agawa mchele, nyama kujipigia debe
Salim Said

MBUNGE wa Jimbo la Wawi wilayani Chake, Hamad Rashid Mohamed (CUF) ameongeza changamoto katika udhibiti wa rushwa kwenye uchaguzi baada ya kugawa mchele, nyama na vifaa vingine vyenye thamani ya zaidi ya Sh1.5 milioni, akijitetea kuwa analindwa na sheria.

Wiki iliyopita, Rais Jakaya Kikwete alisaini kwa mbwembwe Sheria ya Gharama za Uchaguzi ambayo inadhibiti matumizi ya fedha, lakini wakati maandalizi ya matumizi ya sheria hiyo yakiendelea, watu wanaotarajia kuwania ubunge wamekuwa wakilalamikia wabunge wanaoshikilia viti kwenye majimbo yao kuwa wanatoa rushwa za wazi kutokana na kulindwa na sheria.

Hamad Rashid ameungana na wabunge wanaojitetea kuwa wanalindwa na sheria hiyo baada ya kufadhili sherehe iliyoandaliwa kwa ajili ya kuwapongeza wanafunzi 30 wa Shule ya Sekondari ya Mwandani ambao walifaulu kwa asilimia 100 mtihani wa kidato cha pili na kuifanya shule hiyo kuwa ya kwanza kisiwani Pemba na ya pili kitaifa.

Rashid pia ameshatoa misaada ya vifaa vya michezo kwa zaidi ya timu 30 za jimboni kwake ambazo ziko daraja la kwanza, pili na tatu.

Kwa mujibu wa msaidizi wake wa karibu, miongoni mwa vifaa hivyo ni viatu, mipira, jezi na soksi.

"Mkataba wangu ni wa miaka mitano... nimeomba tafsiri ya sheria kwa Mwanasheria Mkuu inayohusu rushwa katika kampeni na ameniambia ukomo wangu ni baada ya uteuzi, sasa wao wamelitoa wapi hilo," alisema alipoulizwa na Mwananchi kuhusu kitendo chake cha kutoa misaada hiyo.

Rashid alisema anawashangaa wananchi wanaohusisha misaada anayotoa na kujipigia debe kwa ajili ya uchaguzi mkuu ujao, akisema kwamba sheria haimkatazi kuendelea na shughuli zake kama mbunge na kwamba anayo haki ya kufanya hivyo hadi pale shughuli za bunge zitakapokoma.

Misaada hiyo imetolewa katika kipindi ambacho baadhi ya wananchi wa jimboni kwake, wamekuwa wakimlalamikia mbunge huyo kwa madai kuwa amelihama jimbo lake na kwamba, anaonekana wakati wa uchaguzi unapokaribia tu.

Wananchi pia wanadai kuwa katika kuonyesha kuwa mbunge huyo haishi jimboni humo, hata gari lake la ubunge amelihamishia Tanzania Bara.

“Angalia hivi sasa akija anatumia gari la Mbunge wa Konde, Dk Tarab Ali au la Mwakilishi wa Jimbo la Ziwani, Maalim Rashid Seif,” alisema mwananchi mmoja ambaye hakutaka jina lake liandikwe gazetini.

Mwananchi ilishuhudia mbunge huyo akitumia gari na dereva wa mwakilishi wa Jimbo la Ziwani katika safari zake tangu juzi.

Shamra shamra za shughuli ya kuwapongeza vijana hao zilianza mapema jana asubuhi wakati gari linalotumiwa na mbunge huyo lilipofika shuleni hapo na kushusha kilo zipatazo 45 za nyama, wakati mchele ulishatumwa tangu juzi.

Shughuli hiyo ambayo mbunge huyo alikuwa mgeni rasmi ilipambwa na maulidi ya kumsalia Mtume Muhammad (S.A.W), dua na kufuatiwa na utenzi, risala na hotuba ya mgeni rasmi iliyoanzia saa 7:00 mchana.

Akisoma utenzi wa hafla hiyo, mwanafunzi wa kidato cha tatu Asha Masoud alimpongeza mbunge huyo kwa kuisaidia shule hiyo, malori 13 ya mawe kwa ajili ya kujenga jengo jipya.

Naye Mwalimu Hamad Kombo alimpongeza na kumsifu mbunge huyo kwa kuweza kufadhili shughuli yote ya kuwapongeza vijana hao.

"Mheshimiwa tunakushukuru kwa kufadhili shughuli yote ya leo (jana). Hii si kwa kujionyesha kama una fedha nyingi, bali ni kwa imani, upendo na uchamungu wako. Tunamuomba Mungu akuzidishie... insha Allah," alisema Kombo katika risala yake kwa mgeni rasmi.

Akijibu risala hizo kwenye hafla hiyo, Rashid alisema katika elimu hana masihara na kwamba hata kama ni kukopa popote, atafanya hivyo ili kufanikisha maendeleo ya elimu jimboni kwake.

"Ombi langu kwenu, kama mwalimu mkuu alivyosema, muhakikishe nyote mnafika chuoni. Tumieni vizuri muda wenu, kuweni na nidhamu shuleni na nyumbani na mhakikishe kwamba masomo ya sayansi mnayapa kipaumbele," alisema Rashid.

"Nitasaidia vitu na vifaa mbalimbali vya sayansi, kwa hiyo kama tulivyofanya kwa shule nyingine jimboni hapa. Pia naahidi kutoa kompyuta moja... mwalimu mkuu andika vifaa hivi naweza kuleta siku yoyote kuanzia sasa... katika elimu sina masihara, nitakopa popote.”

Awali Rashid alisema amekuwa akisaidia jamii ya Jimbo la Wawi katika michezo, elimu na matatizo mengine ya kijamii.

“Hivi sasa wazee wanacheka; timu za mpira zinacheka na shule wanafunzi si mnacheka jamani; mbunge wenu yupo safi, ataendelea kuwasaidia kwa hali na mali,” alisema Rashid.

Mbunge huyo amepata upinzani mkali jimboni kwake baada ya watu watatu kutoka chama hicho kikuu cha upinzani visiwani hapa kuchukua fomu za kugombea ubunge wa jimbo hilo, jambo lililomfanya Rashid kupiga kambi kisiwani Pemba kwa ajili ya kuweka mambo sawa. Rashid ni katika wabunge waliopita kwa kura chache za maoni ndani ya vyama vyao katika uchaguzi wa 2005.
 
MMJ,
Njia pekee ya kutibu (redress hiyo situation) ni kwa Serikali kuleta Bunge la April Miscelaneous Amendment.

Hilo linawezekana lakini linawezekana kiasi kwamba CCM wawe wameona matatizo kwenye sheria yenyewe. HOfu yangu ni kuwa wakati mchakato umeanza ndio watu wataona ugumu wa sheria na taratibu zake zilivyo. Hivi Waziri anayeshughulikia masuala haya ndiyo nani?
 
Dr Slaa,
Naheshimu saaana michango yako ktk siasa za nchi na hasa kuelekea kutatua matatizo ya wananchi.

Lakini nahisi kwamba kuna tofauti kubwa sana kati ya muelekeo wako na wa hiki chama Tawala, CCM. Hii inayoitwa serikali ya CCM haina niya njema na inanifanya nitie mashaka kwa kila wanalolifanya. Hili la sheria ya gharama za uchaguzi, Wananchi wanadhani serikali ya CCM ina lengo zuri lakini siamini kama ni hivyo.

Kwa mtiririko wa matukio ya kampeni zilizopita, hisia zangu ni kwamba sheria hii imekuja kwa sababu ya mwenendo wa CHADEMA ktk kampeni. CCM walidhani ni peke yao wenye uwezo wa kuzunguka nchi nzima kwa gari na nyimbo za John Komba. Sasa wamejikuta hata CHADEMA wakiweza kufanya hivyo kwa kutumia helikopa. Ikimaanisha kwamba kama ni misuri sasa hata wengine wanayo.

Kwa ufupi sheria hii imeletwa ili kuwadhibiti wengine wasionyeshe uwezo wao kifedha. Nina maana kwamba sasa ndo tutaona matumizi yasiyolingana ya sheria hii. Usione ajabu CCM wakaendelea kuzidisha hizo gharama na vyama vingine vikijaribu tu, ndo utaona sheria ikitumika. Nahisi hata ndani ya CCM wengine watabanwa na wengine hasa wanaotaka wapite wataachiwa. Kumbuka jinsi wabunge kama akina Chitalilo walivyodanganya viwango vya elimu yao na bado wameachwa kwa miaka 5 ktk ubunge wakati kuna watu walishaenguliwa.

Hii ni kuwazuia wasiotakiwa kutumia pesa na wengine watatumia watakavyo.
 
Wana JF,

Pamoja na kuitoa hapa, nakala pia nilipeleka kwa Msajili na imejadiliwa katika Semina iliyofanyika tarehe 22 March na 23 March. Kwa ujumla naomba niwaarifu kuwa karibu maeneo yote niliyoyataja yamepokelewa. Swala linalobaki ni je zitakubaliwa ziingie katika Kanuni na Waziri husika!

Pamoja na yote haya nimegundua jambo mmoja kubwa na baya. Kifungu cha 7 sha Sheria yenyewe iliyojadiliwa Bungeni, iliongezewa kifungu kidogo cha 2 yaani 7(2). Na ndiyo iliyopitishwa Bungeni. Mswada uliowasilishwa kwa Mhe. Rais, na kusainiwa na Rais, unasehemu ya 7(3) ambayo haikujadiliwa kabisa Bungeni. Nimeipitia Hansard, nimepitia Schedule of Ammendment, nimepitia na Majadiliano ndani ya Bunge katika Kumbukumbu Rasmi ya Bunge yaani Hansard, iliyoandaliwa tarehe 16/2/2010...

Inaelekea, katika hatua fulani, kati ya Draft hiyo na siku ya kuiwasilisha kwa Mhe. Rais, kuna mtu katumbukiza kifungu kipya cha 7(3); Kifungu hiki kinazungumzia Campaign Team. Kinasema kuwa Approving authority wa Campaign Team atakuwa Registrar of Political Parties kwa Presidential Candidate, na District Administrative Secretary (DAS) kwa Mgombea Ubunge, na Ward Executive Officer kwa Mgombea udiwani. Approving Authority ya Kampen Team haiwezi kuwa nje ya Chama husika, na hasa kuiweka mikononi mwa watu ambao ni watumishi wa Serikali ambao wengi wao kwa sasa wanafanya kazi ya Chama Tawala.

Kesho nitachukua hatua kuwasiliana rasmi na Ofisi ya Spika kujua hasa ni nani aliingiza kifungu hiki ambacho hakikujadiliwa na kuridhiwa na Bunge. Jambo hili ni baya, lakini pia linaweza kuwa Forgery ambayo ni kosa la Jinai. Nitawajulisha rasmi kesho.

Thanks for all your contributions. Mengine nitayajibu kwa wakati mmoja mmoja pale panapohitaji elimu maalum.
Dr Slaa , Heshima yako Mkuu!
Kama kweli kuna kifungu kimechomekwa na ushahidi upo basi hiyo sheria ni batili.Swala la msingi si kuongea na spika tu na kuishia hapo bali ni kwenda Mahakama kuu na kuomba kuifuta hiyo sheria kwa msingi wa kwamba kifungu 7(3) HAKIKUJADILIWA BUNGENI hasa ukizingatia bunge ndiyo chombo cha kutunga sheria. sasa imekuwaje kuwe na kipengele ambacho hakikujadiliwa na bunge ndani ya sheria mama na kumpelekea Mh. Rais kusaini kitu batili,je Rais kabla ya kusaini sheria tarajiwa mbali mbali kuwa sheria kamili, pamoja na kuisoma sheria tarajiwa husika Je anapitia Hansard za bunge kujiridhisha kwamba anacho saini ndicho kilichopitishwa na bunge au ndiyo bora twende?
 
[B said:
Kazi Ndiyo Kipimo Cha Utu[/B];858101]Dr Slaa , Heshima yako Mkuu!
Kama kweli kuna kifungu kimechomekwa na ushahidi upo basi hiyo sheria ni batili.Swala la msingi si kuongea na spika tu na kuishia hapo bali ni kwenda Mahakama kuu na kuomba kuifuta hiyo sheria kwa msingi wa kwamba kifungu 7(3) HAKIKUJADILIWA BUNGENI hasa ukizingatia bunge ndiyo chombo cha kutunga sheria. sasa imekuwaje kuwe na kipengele ambacho hakikujadiliwa na bunge ndani ya sheria mama na kumpelekea Mh. Rais kusaini kitu batili,je Rais kabla ya kusaini sheria tarajiwa mbali mbali kuwa sheria kamili, pamoja na kuisoma sheria tarajiwa husika Je anapitia Hansard za bunge kujiridhisha kwamba anacho saini ndicho kilichopitishwa na bunge au ndiyo bora twende?

I have to admit it.. kurudi kwako kumenichangamsha. Karibu na kokote ulikokuwa umepotolea natumaini wote wazima na mmesalimika!
 
  • Adai mchezo mchafu umefanyika sheria ya uchaguzi
na Irene Mark

KWA mara nyingine, Rais Jakaya Kikwete, amepotoshwa ukweli kuhusu sheria ya gharama za uchaguzi aliyoisaini hivi karibuni katika Ikulu yake jijini Dar es Salaam baada ya kubainika kuwa baadhi ya vipengele vimeingizwa kinyemela nje ya Bunge, Tanzania Daima Jumatano, imebaini.

Kipengele kilichoingizwa kinyemela bila kujadiliwa na kupitishwa na Bunge mjini Dodoma, ni kile kinachohusu uthibitishwaji wa wajumbe wanaounda timu za kampeni kwa ajili ya wagombea wa urais, ubunge na udiwani.

Wakati Bunge linajadili na kupitisha sheria ya gharama za uchaguzi, sehemu inayohusu uthibitishaji wa timu za wagombea ilijadiliwa na wabunge wote, lakini haikueleza nani anayepaswa kukagua timu za kampeni za wagombea wa nafasi mbalimbali, lakini katika sheria aliyosaini rais, inafafanua watu wanaostahili kukagua timu za kampeni.

Kwa mujibu wa sheria iliyosainiwa kwa mbwembwe na Rais Kikwete, kipengele kinachodaiwa kuchomekwa bila ridhaa ya Bunge, kinaonyesha kuwa timu za kampeni za wagombea urais, zitathibitishwa na Msajili wa Vyama vya Siasa, timu za kampeni za wagombea ubunge, zitathibitishwa na Makatibu Tawala wa Wilaya wakati timu za kampeni za wagombea wa udiwani, zitakaguliwa na kuthibitishwa na Makatibu Tarafa.

Akizungumzia utata wa sheria hiyo, Katibu Mkuu wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA), Dk. Wilbroad Slaa, alisema anashangazwa na kilichotokea Ikulu siku ya kusaini mkataba huo, huku akitaka kujua nani aliyehusika kuongeza vipengere hivyo bila idhini ya Bunge.

Dk. Slaa alitoa ufafanuzi wa kasoro hiyo jana wakati wa semina ya kujadili kanuni zinazofafanua Sheria ya Gharama za Uchaguzi, iliyoandaliwa na ofisi ya Msajili wa Vyama vya Siasa nchini, John Tendwa.

Dk. Slaa, ambaye pia ni Mbunge wa Karatu, alionyesha kitabu cha kumbukumbu za Bunge ‘Hansard’ ambacho haikuonyesha viongozi wanaopaswa kufanya uhakiki wa timu za kampeni za wagombea.

“Katika sheria aliyosaini rais kuna kifungu cha 7 (3), ambacho hakikuwepo kabisa kwenye muswada uliojadiliwa na kupitishwa bungeni. Kwa kweli nimeshangazwa sana kwa sababu rais amedanganywa katika hili.

“Bungeni hatukusema nani anatakiwa kukagua timu ya kampeni ya nani, lakini kwenye kipengele ambacho kimo kwenye sheria iliyosainiwa na rais inaonyesha kwamba timu za kampeni za mgombea urais zinatakiwa kuhakikiwa na Msajili.

“Timu za kampeni za mgombea ubunge, zinaonyesha zinapaswa kuhakikiwa na Makatibu Tawala wa Wilaya na kwa kesi ya wagombea udiwani, timu zao kampeni zinapaswa kukaguliwa na Makatibu Tarafa,” nani kaichomeka hii?” alihoji Dk. Slaa, huku wajumbe wengi wakipigwa na butwaa.

Alisema, haiwezekani timu za kampeni ambazo ndiyo kikosi cha ushindi cha mgombea yeyote, kukaguliwa na mtu wa nje ya chama chake, hususan anayetoka chama tawala, yaani Chama Cha Mapinduzi (CCM).

Katibu huyo wa CHADEMA ambaye alikuwa mbogo wakati wa kujadili utata huo wa sheria hiyo, alisema kuna mchezo mchafu uliofanyika kwa lengo la kufifisha kambi ya upinzani nchini.

Dk. Slaa alifafanua kuwa Msajili wa Vyama vya Siasa ni nafasi ya kuteuliwa na rais, hivyo kambi ya upinzani haitakuwa na imani kwa timu zake za kampeni za mgombea wao wa urais, zikaguliwe na mtu huyo.

Alisema si sahihi pia kwa Makatibu Tawala wa Wilaya au Makatibu Tarafa, kuzikagua timu za kampeni ya wagombea ubunge ama madiwani kwa vyama vya upinzani kwa kuwa watendaji hao ni makada wa CCM, hivyo haki haitatendeka.

“Hawa wenzetu wana mbinu nyingi hasa za kuwanunua wafuasi wa upinzani, hivyo kesho nikikubali timu yangu ya kampeni ikaguliwe na DAS (Katibu Tawala wa Wialaya), ni rahisi kwake kuniingizia mamluki...

“Unatakiwa kujua kwamba timu ya kampeni, ndiyo yenye mbinu zote za ushindi hivyo yanaweza kutokea kama yaliyonitokea mimi mwaka 2005, ambapo mmoja wa watu wangu wa kampeni aliyekuwa anaingia kwenye vikao vya siri alirubuniwa na CCM akanikimbia wakati tunakaribia uchaguzi,” alisema Dk. Slaa.

Dk. Slaa alisema kwa mchezo mchafu huo uliofanywa na serikali, anakusudia kuchukua hatua za kisheria ili kumbaini aliyeingiza kipengele hicho kinachofinya uhai wa demokrasia kwa vyama vya upinzani nchini.

Machi 17 mwaka huu, taifa liliandika historia pale wabunge, wawakilishi wa vyama vya siasa, mabalozi, viongozi wa dini na wasomi mbalimbali walipokutana Ikulu ya Dar es Salaam kushuhudia utiwaji saini wa sheria ya gharama za uchaguzi uliofanywa na Rais Kikwete. Sheria hiyo itaanza kutumika kwenye uchaguzi mkuu ujao.

Kwa mujibu wa sheria hiyo, kifungu kidogo cha pili, kinaeleza maana ya timu ya kampeni kuwa ni kundi la watu lililoundwa na mgombea wakati wa zoezi la uteuzi lenye madhumuni ya kumwakilisha au kumsaidia mgombea kwenye kampeni za uchaguzi ambaye amepitishwa kuwania.

“(a) Kwa kesi ya urais watathibitishwa na Msajili, (b) Kwa kesi ya Mbunge watathibishwa na Katibu Tawala wa Wilaya na (c) Kwa kesi ya Diwani watathibitishwa na Katibu Tarafa...,” ilieleza sehemu ya sheria hiyo iliyosainiwa na Rais Kikwete ambayo nakala yake tunayo.

Muswaada huo wa sheria ulioasisiwa na Rais Kikwete mwenyewe, ulipitishwa kwa mbinde Februali 12 mjini Dodoma huku ukiibua malumbano makubwa baina ya Mwanasheria Mkuu wa Serikali, Jaji Frederick Werema, na Mbunge wa Bariadi Magharibi, Andrew Chenge, pamoja na wabunge wengine kuhusu vipengele mbalimbali vya muswada huo.

Mwanasheria Mkuu wa serikali alipingana waziwazi na Chenge aliyekuwa mwanasheria mkuu wa zamani hali iliyomlazimu Naibu Spika kuingilia kati mara kwa mara.

Muswada huo ulimlazimisha Mwanasheria wa Serikali kusimama kwa zaidi ya mara 11 kwa ajili ya kutoa ufafanuzi huku akitahadharisha kuwa yeye ni jaji, hivyo kuwataka wabunge kuwa watulivu baada ya kubaini kuwa baadhi yao walikuwa wakizungumza kwa sauti za juu wakati mwanasheria huyo aliposimama.

Wanasheria hao pamoja na wengine walikuwa wakibishania kifungu cha saba ambacho hakikuwa na ufafanuzi kuhusu gharama za watu wanaosaidia katika kampeni ambapo Chenge alitaka baadhi ya mambo yaongezwe ili kupanua wigo kwa wapiga kampeni hao katika kugharamiwa baadhi ya mambo ikiwemo chakula na malazi.

Chenge alitaka kifungu hicho kiwekwe kwani kwa mtazamo wake ni halali kwa mgombea kuwalisha na kuwagharamia watu ambao wanamsaidia katika kampeni jambo lililotafsiriwa vibaya na baadhi ya wabunge. Wabunge wengine ambao walikuwa moto na muswada huo ni pamoja na Halima Mdee, Dk Slaa, na Peter Serukamba.


The blue bolded statement from mzee wa vijisent worries me if he is real a lawyer if he knows the meaning of corruption.
 
a) Kwa kesi ya urais watathibitishwa na Msajili, (b) Kwa kesi ya Mbunge watathibishwa na Katibu Tawala wa Wilaya na (c) Kwa kesi ya Diwani watathibitishwa na Katibu Tarafa...," ilieleza sehemu ya sheria hiyo iliyosainiwa na Rais Kikwete
bado naishangaa nguvu ya serikali katika utungaji wa sheria ambazo zimepitishwa na bunge, naungana na Slaa kushangaa namna watawala wanavyolipuuza Bunge kwa kuingiza vitu vyao nnje ya sheria iliyopitishwa na Bunge.
 
NINYI WATU,
hakukuwa na sababu ya ku-paste magazeti wakati muhusika mwenyewe alianzia humu kulielezea hilo swala.i mean,hata aliyeandika hilo gazeti ametoa humu humu jf!
 
Nampenda sana Dk.Slaa, anajituma, anasoma sana na kutufundisha alichosoma bila kudai malipo. Nampenda sana kwa anafanya tafiti kabla hajasema! Kwa kweli anatujuza Watanzania madudu yanayofanyika nyuma ya Pazia hasa anapokuwa bungeni.

Haka ka mchezo kaliko fanyika ka kuchomekea kanadhihirisha kuwa the whole process has a hidden agenda! Kwa nini in the first place mswaada huo ulikuwa wa kulazimisha lazimisha vile? Kwa nini ulisainiwa kwa mbwembwe kubwa kinyume na miswada yote iliyopita tangu tupate uhuru?

Tutayaona mengi mwaka huu!
 
Huu ni Mkuki kwa Upinzani na uvunjaji wa Sheria za nchi (Kama hii ni kweli basi Sasa ikulu inatunga sheria), Sasa ngoja tusikie Mweshimiwa Six(6) Mzee wa Standard na Speed anasemaje kuhusu hili? Na kama ni kweli nani awajibishwe? Nashauri kama ni kweli basi wapinzani wakimbilie mahakamani haraka sana.
 
inawezekana kile ki babu kinachoitwa philip malmo, naona kina powers za ajabu siku hizi
 
Huu ni Mkuki kwa Upinzani na uvunjaji wa Sheria za nchi (Kama hii ni kweli basi Sasa ikulu inatunga sheria), Sasa ngoja tusikie Mweshimiwa Six(6) Mzee wa Standard na Speed anasemaje kuhusu hili? Na kama ni kweli nani awajibishwe? Nashauri kama ni kweli basi wapinzani wakimbilie mahakamani haraka sana.
Umefika wakati sasa CCM na serikali yao waache kufanya mambo kwa mazoea na pia wakumbuke kwamba pamoja na hii michezo michafu wanayocheza hawatakuwepo madarakani milele hivyo wanapaswa kuwa fair ili kamba wanazozitayarisha zije ziwanusuru na wao pia.

Uchunguzi wa kina ufanyike na yeyote aliyehusika na uhuni huu ana kesi ya kujibu mahakamani, huwezi kuwa unacheza na sheria za nchi halafu ukategemea tunaendelea kukuchekea. We have to be serious on this.

I support Dr Slaa, to me he is a real Tanzanian.
 
2: Kifungu cha 5(2) Kinatamka kuwa "….. the nominating organ shall be …(b) in the case of a Member of Parliament, the members of the Political Party within the District…and (c) in the case of a Councilor, the members of the political party within the ward…"
Kifungu cha 6(2) kinaweka "Regional Women organ" kuwa chombo cha kufanya Short listing ya Wagombea wa viti maalum.

Huu ni uCCM ndani ya kanuni. Hivi huyu anayetunga kanuni hizi anajua anachokifanya au anafikiri Watanzania wote ni wajinga? Kama ni waziri, basi ni wazi hafai kabisa!
Hili lingine la kumsainisha Rais sheria ambayo haijapitishwa bungeni, ni la hatari sana. Kama vipengele fulani vya sheria vilichomekwa baada ya bunge kupitisha, ni wazi, alichosaini Rais sicho kilichopitishwa na Bunge; na hivyo alichosaini Rais ni batili!
 
Status
Not open for further replies.
0 Reactions
Reply
Back
Top Bottom