Kansa huamki kwa siku moja.....!!!

J.K.Rayhope

JF-Expert Member
Oct 26, 2011
316
31
Baadhi ya maneno ya Mwl.Nyerere kwa serikali ya CCM ya sasa yanaonekana kuwa makali kuliko mkaa wa moto,na baadhi ya viongozi huzima hata redio kwani wakiyasikia huwachoma kweli na huwasuta nafsini mwao.Misingi ya utawala bora na demokrasia ya kweli imekiukwa,Mfano yanayoendelea Arusha leo ni kama kansa inayosambaa tartiibu mwilini mwa mgonjwa.CCM leo imepoteza majimbo mengi na muhimu kwao.Kama ni maziwa ya ng'ombe fresh tayari yamechanganywa maji.Ubungo,Kawe,Ilemela,Nyamagana,Arusha mjini,Maswa,Moshi mjini,Rombo,Mbeya n.k.Yamekwenda upinzani.Wapo baadhi ya Wanaccm wamediriki kusema bora kupoteza majimbo hata 60 (vijijini) kuliko haya zaidi ya 20(mijini) yaliyokwenda upinzani...Ushauri,CCM iache mara moja tabia ya visasi na siasa za chuki,Kama kweli tuliiweka madarakani,ipambane na majukumu mazito ya kuleta maendeleo.Hii ni nchi ya kidemokrasia,raia wake wako huru kusikilizwa,kuishi popote kwa kufuata sheria lakini dola hutumiwa kichama zaidi.Bila CCM,CHADEMA,CUF n.k Nchi yaTanzania ipo daima tu.Mbona nchi haikupata uhuru na CCM?Nawasilisha
 
Hawamwogopi Mungu, hasikii,hawana ufahamu, hawaoni,hawaamini,hawana Utu,hawana hisia basi ni kuwapa pole manake binadamu mwenye hayo uwa anajua kwa kutenda haya mwisho wangu ni huu.Cha kuwaombea ya Ghaddafi yasiwafike,kwa kuwa nina imani watanzania kama kansa hiyo ya machungu ikisambaa mwili mzima wa Tanzania basi yatakayotokea kwa viongozi ni picha isiyoelezeka kwa kuwa kama Mtanzania ambae raia mmoja aliyebiwa simu ya mkono,umma umuhukumu mwizi wa simu hiyo ya kwa kumchoma moto na tairi la gari au mafuta ya taa.Pata picha itakuwaje watakapojichukulia sheria mkononi kusaka mafisadi kwa mikono yao.
 
Baadhi ya maneno ya Mwl. Nyerere kwa serikali ya CCM ya sasa yanaonekana kuwa makali kuliko mkaa wa moto, na baadhi ya viongozi huzima hata redio kwani wakiyasikia huwachoma kweli na huwasuta nafsini mwao.

Misingi ya utawala bora na demokrasia ya kweli imekiukwa, Mfano yanayoendelea Arusha leo ni kama kansa inayosambaa tartiibu mwilini mwa mgonjwa. CCM leo imepoteza majimbo mengi na muhimu kwao. Kama ni maziwa ya ng'ombe fresh tayari yamechanganywa maji. Ubungo, Kawe, Ilemela, Nyamagana, Arusha mjini, Maswa, Moshi mjini, Rombo, Mbeya n.k. Yamekwenda upinzani.

Wapo baadhi ya Wana ccm wamediriki kusema bora kupoteza majimbo hata 60 (vijijini) kuliko haya zaidi ya 20 (mijini) yaliyokwenda upinzani...Ushauri, CCM iache mara moja tabia ya visasi na siasa za chuki, Kama kweli tuliiweka madarakani, ipambane na majukumu mazito ya kuleta maendeleo. Hii ni nchi ya kidemokrasia, raia wake wako huru kusikilizwa, kuishi popote kwa kufuata sheria lakini dola hutumiwa kichama zaidi. Bila CCM, CHADEMA, CUF n.k Nchi yaTanzania ipo daima tu.Mbona nchi haikupata uhuru na CCM

My take. Mr Ray hope has smthing for us to contemplate!!

 

Similar Discussions

0 Reactions
Reply
Back
Top Bottom