drphone
JF-Expert Member
- Sep 29, 2009
- 3,542
- 281
Nawashukuru wote walionipa mawazo mazuri sana. Kwa Pdidy na drphone nasikitika kuona mnaanza kunishutumu bila kuniuliza zaidi. Mimi ninaishi ughaibuni kwa miaka mingi (zaidi ya ishirini), lakini kila mwaka ninakuja Tnazania mara mbili au tatu, kwa hiyo siyo kweli kuwa sijui thamani ya pesa na siwasaidii wazazi. Na baba mzazi ni mdhaifu, kila mwaka ninamchukua anakuja kutibiwa ughaibuni na kumrudisha. Hata mwaka jana alikuwa huku. Kinachosikitsha tu ni hicho cha kuuza nyumba na kutaka kuuza ya pili. Zile milioni moja na laki saba zilizotolewa kanisani, zilitokana na mzigo niliotuma mimi, wao wakaupokea na kuuza kwa milioni kumi na saba. Wakanijulisha wenyewe (mama) kuwa wameuza na wamepata milioni kumi na saba, wamechukua milioni moja na laki saba wamepeleka kanisani. Wakati mimi nilitaka wakiuza, waweke pesa bank, ili ziweze kutumika kununua dawa za baba, na zingine iwe nauli yao wakija huku kutibiwa nisiwe na lazima ya kutuma pesa za nauli. Hakuna neno kubwa kwani zilizobaki niliambiwa ziliwekwa bank. Kasheshe ikaja wakati miezi michache baada ya hapo naombwa nitume laki tatu za dawa!!!!
Nimeshaanza kulishughulikia kutokana na ushauri mzuri niliopewa na wanajamvi wengine wengi. Ninatanguliza shukrani zangu za dhati. Safari hii nitajizatiti mpaka kieleweke. Kwa wale wasiotaka kuamini kuwa kuna watu wanaotumia dini kuwalaghai wazee, msishangae hata ninyi yakiwafika!
pole sana mkuu atujakushutumu bali tumejibu kutokana na maelezo yako maana ata mm naishi mbali na familia na mzazi wangu afanyi jambo lolote achilia mbali kama hlo la kuuza nyumba bila ya kutushirikisha kabisa wote na huu ni utamaduni wa wazazi wengi wenye watt pole kama majb yangu yalikukwaza ila na mm nilikwazika pia na kichwa cha habari na maelezo yako yasiyokamilika maana unahisi kama mtumishi wa mungu ni tapeli lakini unauhakika na mahakama pekee ndio inamtia mtu hatiani si mtetei hapana bali hili naongelea kwa yyote tuwaheshimu watumishi wa mungu naamanisha wote wa kikristo na wakiislam.
kama uliwapa wazazi wako wauze bidhaa ya 17m hyo walopeleka linaitwa fungu la kumi wenye ufahamu wanaelewa kwamba kila sehemu ya kumi ya kipato chako si chako ni cha mungu