MBEYA: Kanisa kutoa orodha ya wauza unga

MCHUNGAJI wa Kanisa la Evangelical Pentecost Church (TEC) la mjini Mbeya, William Mwamalanga, amesema wanatarajia kumsaidia Rais Jakaya Kikwete, kutaja hadharani orodha ya vigogo wanaoshiriki katika biashara ya dawa za kulevya.

Kauli ya mchungaji huyo imekuja siku moja baada ya Ofisi ya Rais (Ikulu) kuwataka maaskofu wa Jumuiya ya Kikristo Tanzania (CCT) kuacha kutoa saa 48 kwa Rais Jakaya Kikwete kutaja majina ya viongozi wanaouza dawa za kulevya bali yeyote anayejishuku ajisamilishe au atajwe.


Akizungumza na Tanzania Daima jana kwa njia ya simu, Mwamalanga alisema kundi la viongozi wa dini kutoka makanisa mbalimbali wamepanga kukutana kwa ajili ya kutaja majina ya vigogo wanaojihusisha na biashara hiyo.


Alisema wanatarajia kutaja majina yote, si ya viongozi wa dini ya Kikristo pekee, bali hata wale waliopo nje ya Ukristo, ambao taarifa zao zimefika hadi kwa Rais Kikwete.


"Si kwamba tutataja majina ya maaskofu na wachungaji pekee, bali tutataja hadi wale waliomo ndani ya Ofisi ya Rais, ambao wanafanya biashara hiyo, wabunge pamoja na mawaziri," alidai mchungaji huyo.


Alisema wana taarifa kamili ya viongozi wa dini ambao wanatumia makanisa kama vivuli na kujificha, kumbe wanaendesha biashara hiyo haramu inayoangamiza taifa.


Mchungaji Mwamalanga alisema lengo ya kutaja majina hayo hadharani ni kutaka kumsaidia Rais Kikwete na kuisafisha nchi iondokane na uingizaji, uuzaji na utumiaji wa dawa za kulevya.


"Kwa sasa tupo Dodoma na leo tunatarajia kutaja majina hayo ambayo Rais Kikwete anashindwa kuyataja, ili kumsaidia …maana taarifa za orodha hiyo tuliwahi kumfikishia katika ofisi yake mwaka 2006," alisema.


Alisema viongozi wa dini wanaotumia makanisa kama vivuli huku wakiendesha biashara hiyo wanafahamika wazi, lakini wamekuwa hawachukuliwi hatua.


Aliongeza kuwa wanategemea kuwa orodha hiyo ikiwekwa hadharani wahusika watafikishwa kwenye vyombo vya sheria ili kuwachunguza.


Alibainisha kuwa kama vyombo vya dola vitapuuzia orodha hiyo watakayoitaja, kamwe mapambano dhidi ya dawa za kulevya hayawezi kuzaa matunda.


Mwishoni mwa wiki iliyopita wakati Rais Kikwete akihutubia waumini wa Kanisa Katoliki la Mtakatifu Killian katika sherehe ya kuwekwa wakfu na kusimikwa Mhashamu Askofu John Ndimbo, kuwa askofu wa Jimbo la Mbinga, alikaririwa akisema baadhi ya viongozi wa dini wamekuwa wakishiriki kufanya biashara ya dawa za kulevya.


Kauli hiyo iliwafanya maaskofu wa Jumuiya ya Kikristo Tanzania (CCT) kumpa Rais Jakaya Kikwete saa 48 kuwataja kwa majina viongozi wa dini wanaojihusisha na dawa za kulevya.


Baada ya tamko hilo, juzi Ofisi ya Rais Ikulu iliwakosoa viongozi hao kwa kutoa tamko la kusikitisha, ambalo ililiita kuwa halikustahili kutolewa nao.


Ikulu iliweka bayana kuwa viongozi wa dini si malaika au watakatifu hapa duniani, kwani wanaweza kutumbukia katika majaribu na kujikuta katika vitendo au hali isiyo tegemewa katika jamii.



Source: Tanzania Daima ya Leo

Kanisa kutoa orodha ya wauza ‘unga'

Hii habari naiona imekaa kimagamba magamba..ikiazimia kumletea ahueni raisi..OK ngoja awataje tuone..ila cha ajabu kama kweli Rais alipewa listi hiyo tangu 2006...amefanya nini?? TZ eeehh x2....
 
Duh!!??nimefuatilia kastori katamu haka.na hadithi ya jk ikaishia hapo.
 
Jamani hebu tusaidia

Unajua mtu ukisoma kwa mara ya kwanza hii habari unajua TEC na CCT wamekaa na kuandaa haya.... ati kanisa kutoa orodha, ni bora wangesema kanisa la pentekoste mbeya kutoa orodha

i think it is an intentional move by the media to magnify bullshit na kuendelea kugombanisha wakristu na wanasiasa

sijui inatufikisha wapi hii fooking move

Mimi sikuwa nikifahamu kuwa hicho kifupisho cha TEC kinatumika pia kisheria na dhehebu jingine lililojisajili Tanzania zaidi ya Tanzania Episcopal Conference (TEC) yaani Baraza la Maaskofu wa katoliki Tanzania. Yaelekea habari nzima inalenga kuwagombanisha wakristu na serikali na nadhani hiii imefanywa kwa makusudi ili ku Divert attention.

Pamoja na kwamba mimi si CCM wala siupendi uongozi wa JK bado sioni tatizo kwa yeye kutamka kwamba baadhi ya viongozi wa dini wanajihusisha na madawa ya kulevya. Mnyonge mnyongeni lakini haki yake mpeni. Wafadhili wa madawa ya kulevya katika jamii yetu wapo katika kila nyanja; wapo wafanyabiashara, wachungaji, Maaskofu wa madhehebu yanayoota kama uyoga na ambao hawana wa kuwadhibiti, masheikh, maaskari, mawaziri, wanamichezo, madereva mpaka wasukuma mikokoteni.

Sasa kuna ubaya gani kwa mtu aliyepewa dhamana ya kuangalia usalama kupiga kelele kwamba kuna watu wachche wabaya miongoni mwetu? Jukumu la kujiangalia walivyosimama katika safu zao kwamba ni nani anayewatia dosari viongozi wa madhehebu ni lao na si serikali.

Kwa hiyo Masheikh, Maaskofu, Wachungaji, Maimamu na viongozi woote wa kiroho watusaidie, wajisafishe kwa kuwataja hadharani wanaoichafua safu yao ili kuiokoa nchi hii yetu sote.
 
Mi JK ananishangaza sana................
Ile orodha ya waharibifu wa bandari anayo.......... lakini hajafanya kitu.......
Orodha ya wahusika wa mishahara hewa ................. anayo hajafanya kitu.............
Meremeta................ hata muwasulubishe hawafanyi kitu...................
Huyo askofu kasema orodha ya wauza unga unayo toka 2006............ hujafanya kitu..........
Mafisadi orodha unayo........................... umewashindwa..................


JK....... KUISHIA KUFAHAMU ORODHA TU HAKUTAKUSAIDIA KITU KATIKA HIZI HARAKATI ZA KUVUANA MAGAMBA.....................KWENYE HILI LA MADAWA MMENIKUMBUSHA AMINA CHIFUPA
Mtamsaidiaje huyo mjinga hana maamzi hata siku moja ya ni mwanamke kwa lugha nyingine uanaume wake nipale anapokuwa amevaa nguo za kiume mimi sioni haja ya kulumbana au kutaja maana kila kitu anajua kama majina anayo anataka msaada wa nini?
 
Kesho mimi natoa orodha yangu.........Wamo mawaziri,makatibu wakuu,mabalozi,masheikh,wabunge,wafanyabiashara wakubwa, stay tune
 
mmmh tutasikia mengi..na nyie viongozi wa dini hebu fanyeni kazi ya mungu huko na mzidi kuwaombea kondoo wenu sio madawa madawa :shut-mouth:
Hpana sister,waache waendelee na harakati hizo,kwa kuwa kauli ya rais ina utata mkubwa sana!!
 
na Betty Kangonga

MCHUNGAJI wa Kanisa la Evangelical Pentecost Church (TEC) la mjini Mbeya, William Mwamalanga, amesema wanatarajia kumsaidia Rais Jakaya Kikwete, kutaja hadharani orodha ya vigogo wanaoshiriki katika biashara ya dawa za kulevya.

Kauli ya mchungaji huyo imekuja siku moja baada ya Ofisi ya Rais (Ikulu) kuwataka maaskofu wa Jumuiya ya Kikristo Tanzania (CCT) kuacha kutoa saa 48 kwa Rais Jakaya Kikwete kutaja majina ya viongozi wanaouza dawa za kulevya bali yeyote anayejishuku ajisamilishe au atajwe.

Akizungumza na Tanzania Daima jana kwa njia ya simu, Mwamalanga alisema kundi la viongozi wa dini kutoka makanisa mbalimbali wamepanga kukutana kwa ajili ya kutaja majina ya vigogo wanaojihusisha na biashara hiyo.

Alisema wanatarajia kutaja majina yote, si ya viongozi wa dini ya Kikristo pekee, bali hata wale waliopo nje ya Ukristo, ambao taarifa zao zimefika hadi kwa Rais Kikwete.

“Si kwamba tutataja majina ya maaskofu na wachungaji pekee, bali tutataja hadi wale waliomo ndani ya Ofisi ya Rais, ambao wanafanya biashara hiyo, wabunge pamoja na mawaziri,” alidai mchungaji huyo.

Alisema wana taarifa kamili ya viongozi wa dini ambao wanatumia makanisa kama vivuli na kujificha, kumbe wanaendesha biashara hiyo haramu inayoangamiza taifa.

Mchungaji Mwamalanga alisema lengo ya kutaja majina hayo hadharani ni kutaka kumsaidia Rais Kikwete na kuisafisha nchi iondokane na uingizaji, uuzaji na utumiaji wa dawa za kulevya.

“Kwa sasa tupo Dodoma na leo tunatarajia kutaja majina hayo ambayo Rais Kikwete anashindwa kuyataja, ili kumsaidia …maana taarifa za orodha hiyo tuliwahi kumfikishia katika ofisi yake mwaka 2006,” alisema.

Alisema viongozi wa dini wanaotumia makanisa kama vivuli huku wakiendesha biashara hiyo wanafahamika wazi, lakini wamekuwa hawachukuliwi hatua.

Aliongeza kuwa wanategemea kuwa orodha hiyo ikiwekwa hadharani wahusika watafikishwa kwenye vyombo vya sheria ili kuwachunguza.

Alibainisha kuwa kama vyombo vya dola vitapuuzia orodha hiyo watakayoitaja, kamwe mapambano dhidi ya dawa za kulevya hayawezi kuzaa matunda.

Mwishoni mwa wiki iliyopita wakati Rais Kikwete akihutubia waumini wa Kanisa Katoliki la Mtakatifu Killian katika sherehe ya kuwekwa wakfu na kusimikwa Mhashamu Askofu John Ndimbo, kuwa askofu wa Jimbo la Mbinga, alikaririwa akisema baadhi ya viongozi wa dini wamekuwa wakishiriki kufanya biashara ya dawa za kulevya.

Kauli hiyo iliwafanya maaskofu wa Jumuiya ya Kikristo Tanzania (CCT) kumpa Rais Jakaya Kikwete saa 48 kuwataja kwa majina viongozi wa dini wanaojihusisha na dawa za kulevya.

Baada ya tamko hilo, juzi Ofisi ya Rais Ikulu iliwakosoa viongozi hao kwa kutoa tamko la kusikitisha, ambalo ililiita kuwa halikustahili kutolewa nao.

Ikulu iliweka bayana kuwa viongozi wa dini si malaika au watakatifu hapa duniani, kwani wanaweza kutumbukia katika majaribu na kujikuta katika vitendo au hali isiyo tegemewa katika jamii.


Source: Tanzania Daima.

Angalizo langu: Ni mpambano kati ya Kanisa na Rais. Nafuu itakuwa kwa sie walalahoi kwani wauza unga wanaiharibu jamii na kama ni watu wenye nguvu basi nafikiri mahakama ya umma inawatosha kuwahukumu. Nawapa hongera sana maaskofu kwa ujasiri wenu watajeni jamii iwahukumu!!!!

Ndugu yangu,
Ninaona kama serikali na kikwete wake wamejitisha mzinga wa nyuki kichani ndani yake kukiwa na kila aina. Tusubiri huo mzinga udondoke kama utakuwa salama.
 
Waangalie wasije wakapoteza maisha yao, biashara ya madawa ya kulevya inahusisha watu hatari na wenye nguvu kwenye serikali. Hawa pia ni wachangiaji wakubwa kwenye vyama tawala vya nchi wanayofanyia kazi, wana watu wao kwenye vyombo vya usalama, serikalini na mahakamani....

Hata hivyo tunamtakia kila la heri Mtumishi wa Mungu na wenzeka ili walisaidie taifa kupambana na aibu hii!
 
Mbona inasemekana huyu mchungaji wa Mbeya hana kanisa wala nini ni mwanaharakati tu kama Mtikila. Tena ni kihere here kinachojipendekeza kwa dola. Na ni huyu aliyeitoa hiyi listi mnayodai Jk kukabidhiwa tangu 2006 na akausugua.
Rais yeye katika ile hutuba yake ya tareha 02 asingelaumiwa na kupewa saa za kwataja wauza unga kama engesema, 'baazi wa viongozi wa dini wanajihusisha na dawa za kulevya' tatizo lake lilikuwa ni ku- generalise kwa kusema 'viongozi wa dini wanajihusisha na biashara ya dawa za kulevya' maana yake ni kwamba wote ni wauza unga. Hivyo ni busara raisi kuirejelea ile hutuba yake ilii kubaini kosa lake. Ni uchaguzi wake kuomba radhi ama kukaa kimya na kuendelea na zoezi lake la kupropagate kwa kuwavuta viongozi wa dini kwenye mchezoo wa propaganda za siasa.
.
 
Kwa kweli katika hili kanisa inabidi kujidhatiti sana maana laweza kutaja hata wateule wa mzee wa kaya hivyo bidhaa zao zaweza anza kutozwa ushuru.Pia utajikuta hao wachungajin baadhi wakawa ndo wahusika wakuu.
 
Aangalie wasijewaka mchifupa kabla hajawataja
Waki mchifupa tutataka zaidi kikwete awataje! Si alishapewa orodha? Hapa anasaidiwa, wanaomsaidia wakichifupwa yeye ataisaidia polisi, maana wauaji lazima wawe toka hiyo orodha! Lakini subiri kidogo! Hivi kumbe Bongo hatuna polisi.. Mwena ni mkuu wa kitengo cha usalama cha ccm...
 
Back
Top Bottom