Kanisa Katoliki LATOA MWONGOZO WA MAONI YA KATIBA

Hebu mleta uzi weka habari yote iloyoandikwa kwenye gazeti la mwananchi....ndo tujadili kichwa cha habari kinaweza kikawa na upotoshaji.
 
Kwa hiyo wakatoliki tutatoa maoni kama kundi baada ya kupata mwongozo toka kwa maaskofu? Vitu kama hivi ndivyo huleta chokochoko. Wenzetu wa upande wa pili nao wakitoa muongozo kwamba mahakama ya kadhi iingie kwenye katiba itakuwaje?

Najua maaskofu wameongelea tu hayo madaraka ya rais lakini hivi ni muhimu wao kutoa muongozo kwa waamini? Kwa nini tusiachiwe tutoe maoni yetu kama watu huru bila viongozi wetu wa kiroho kuingilia? Hayo yatakuwa ni maoni ya kanisa au maoni ya waamini?

kaka ungeuona kwanza mwongozo wenyewe ndo ukachangia au kulaumu hao maaskofu inawezekana mleta thread kawa interested na madaraka ya rais tu. Pia watoto wa ma mdogo mbona walishatoa na wao msimamo wao kitambo tu , na walishataka swala la mahakama yao liwemo kwenye katiba, pia ijumaa iwe siku ya mapumziko kama jmosi na j2, na mengine ya kwao
 
kweli nyani haoni kundule, kunya anye kuku akinya bata kaharisha, ndo sasa nazidi kuamini hii misemo. ki ukweli udini upo wazi wazi kwenye nchi hii ya tanzania, je? wangesema wale wa upande wa pili ingekuwa reactiona za watu kama si kusengenya na kejeli, na post ingewekwa humu jf ingekuwa ishashambuliwa sana mpaka sasa! nazidi kuamini mfumo wa dini fulani kuiongoza na kutoa maamuzi kati hii nchi kweli upo, na ingekuwa upande wapili wametoa yao, humu ungesikia jk dhaifu kaupandikiza mwenyewe udini, duuh, tunaelekea kubayaM sana.
mbona bado jk hawezi kujitoa kwa hili mkuu.
 
mbona bado jk hawezi kujitoa kwa hili mkuu.

ilo ni wewe! na mimi naamini udini umeanza kwa nyerere bila kificho na madhara yanaonekana sasa, kama nyerere asingeweka udini haya yote yasingejitokesa kwa vipindi vya awamu tofauti za viongozi tofauti! kama kweli angetuweka kwa usawa kwenye udini pindi icho haya leo yasingekuwepo.
 
Kanisa Katoliki lahoji madaraka ya Rais

LATOA MWONGOZO WA MAONI YA KATIBA, LATAKA ASITEUE MAJAJI, WABUNGE WAKUU WA MIKOA, ASHTAKIWE

KANISA Katoliki Jimbo Kuu la Dar es Salaam, limetoa mwongozo kwa waumini wake, likiwataka kushiriki mchakato wa kutoa maoni ya Katiba Mpya, huku likihoji madaraka makubwa aliyonayo Rais katika mambo mbalimbali.

Huo mwongozo limetoa wapi na lini?

Nashangazwa na wote mliokurupuka kuchangia bila kuomba kuona huo waraka. Na kama ni maneno tu yalisemwa kwenye ibada, huo sio msimamo wa kanisa, yatakuwa ni maoni ya Padre aliyekuwa akiongoza ibada.

Kanisa Katoliki lina uongozi na lina msemaji wake. Ili niamini kuwa Kanisa Katoliki limetoa msimamo au mwongozo ungeniambia umetolewa wapi, lini na saa ngapi ili niweze kufahamu.

Kanisa Katoliki sio kijiwe cha wahuni wa kila mtu kujitolea tamko, mara huyu kasema hivi kesho wa kigango kile kikasema hakimtambui aliyesema jana mara kesho wanyanyuke watu kumi waseme wanaenda kubadili kauli ya askofu n.k. weka heshima kwa Kanisa Katoliki.
 
chombo pekee kilichopewa mamlaka ya kusikiliza na kuratibu maoni ya katiba ni Tume ya mabadiliko ya katiba na ipo kisheria na sio kanisa katoliki,...
Hivi ni wapi ulipoambiwa Kanisa katoliki linasikiliza na kuratibu maoni? Mwee jamani, tuwe tunasoma maelezo kwa utulivu na kutumia akili!
 
Mimi nawashangaa wasukuma wako wengi sana lakini hawatoi miongozo sijui hawautaki uraisi...hahahahaahahaha
 
Sioni tatizo maaskofu kutoa maoni yao wao kama watu binafsi katika jamii waishimo na mbaya wakitoa kama kundi na siyo mwongozo. Lakini kwamba ni mwongozo kwa waumini hili sina hakika na silitegemei. Miongozo ya Kanisa Katoliki ina utaratibu wake. Maoni kuhusu katiba mpya ni mambo ya kisiasa zaidi na hayahusiki kabisa na imani ya dini ya wakatoliki. Na wanachodai Maaskofu wamesema ni kati ya maoni common masikioni mwa watu. Kwahiyo hapa hoja ni kuchafuana. Mtu mwenye akili atawapuuza. Naomba reliable source kuhusu hili kwamba kuna huo mwongozo vinginevyo imetoka kwa watu wale wale wabaya wanaochochea na kuanzisha chuki kati ya dini na kati ya wanainchi.
 
hilo ni tamko la maaskofu,wachungaji,mapadre na viongozi wa tec,cct,cpct jijin mwanza wametoa maangalizo yafuatayo hoja ya mahakama ya kadhi hamna sababu ya tume kuchukua maoni juu ya swala ambalo limeshatolewa uaumuzi so kitendo cha serikali kugharamia mafunzo ya watendaj wa mahakama ni kinyume na katiba iliyo sasa. Mbili sheria za kidin zanzibar nchi yetu sio ya kidini .tatu mgawanyo wa madaraka uzingatie uwezo wa mtanzania na tusiangalie uwiano kidini.
 
iLALA WENYE MWONGOZI UWEKE WAZI TUJADILI
 
kanisa katoliki lahoji madaraka ya rais

latoa mwongozo wa maoni ya katiba, lataka asiteue majaji, wabunge wakuu wa mikoa, ashtakiwe

kanisa katoliki jimbo kuu la dar es salaam, limetoa mwongozo kwa waumini wake, likiwataka kushiriki mchakato wa kutoa maoni ya katiba mpya, huku likihoji madaraka makubwa aliyonayo rais katika mambo mbalimbali.

si vema kuwasemea wenzako waache wenyewe wajisemee,na kama wamekutuma ilibidi wakupe vielelezo ili kuonesha ushiriki wako juu ya huo ujumbe uliotuletea hapa jukwani.wakati mwingine si busara kuwakilisha mambo mazito kama haya kiuwepesi namna hiyo,na hata kama ni kweli wale wote waliandaa ujumbe huo wataonekana si wenye maono thabiti juu ya mustakabali wa taifa letu.
 
viongozi wetu wa dini bwana, sadaka zetu wanakula dhambi zetu tunaungama kwao sasa sijui tuwape nn cha ziada ili watulee kiroho badala ya porojo
 
wale hawawezi kupiga kelele maana wamepewa urais wame prove mautumbo tupu

Kuna watu wengine kama mnaishi mapangoni....

Wewe moja kwa moja unawalenga waislamu na inaonesha ni mdini uliyekithiri

Hembu tuchukulie kweli kikwete amefanya utumbo ....swali je amefanya utumbo kwa kuwa yeye ni Muislamu au Kwa kuwa Hajui Kuongoza.

Muasisi wa ufisadi nchini ni MKAPA ....Hii inamaanisha wakristo wote ni Mafisadi
Yule waziri wa elimu aliyesema Tanzania ni Muuangano wa Zimbwabwe na Pemba ni Mkristo ..hii inamaanisha wakristo wote ni vilaza wakiogozwa na wewe.....
Mzee wa vijisenti ni Mkristo ...Hii inamaanisha wakristo wote wazee wa vijisenti.....
Mapadri wanakula 0713 watoto wa kiume huko Sunday Schools .....Hii inamaanisha wakristo wote ndio michezo yaooo...


Kama una Matatizo na mtu elekeza tuhuma zako kwake binafsi usiwatukane watu wa jamii yake wote

Msalimie PADRI wako aliyekutuma

Kwa taarifa yako tu Yaya Touré is a strict practicing Muslim...mtoe katika Avatar yako kabla hajakurushia majini
 
kwani mbona muslims mpaka wameunda tume na hamkusema. Kwa taarifa yako mahubiri makanisani mara nyingi hutolewa kulingana na mambo yanayozunguka jamii ukilinganisha na maandiko ya siku. hivyo ni muhimu kwa waumini kujua mambo yanayowazunguka. Kumbuka Mapadri na wachugaji hawa ni watanzania na wasomi wa taifa hili na wanajua udhaifu wa jamii inayowazunguka, ndiyo maana kwenye tume hadi vikundi vya dini vimezingatiwa lengo kuu ni kuwa hawa vioungozi wa dini ndio wanaokaa na watu na ndiyo wenye influence zaidi kwa jamii. Kwa hiyo kama mkatoliki naamini hizi ni njia sahihi kabisa. na yaliyosemwa sioni ubaya wake kama kuna ubaya wa maoni yaliyotolewa onyesha hapa tujadili. haya yaliyozungumzwa ndiyo mahitaji na madai ya watanzania waliowengi. Muslims wamekuwa wakiotoa matamko ambayo moja kwa moja yanaonyesha kabisa ni yakichochezi na katika hali ya kawaida kabisa huoni kama yatakubalika mbona hamsemi. hebu acheni upuuzi tujadili hoja coz din zote zinanafasi katika uundwaji wa hii katiba mpya ili mradi tu itetee maslahi ya taifa na si kikundi cha dini fulani. Kama kanisa Katoliki litaleta maslahi yake binafsi kwenye uundwaji wa katiba mpya hata mimi kwa jina la Yesu Kristo nitalikana, lakini kwa haya yaliyosemwa naamini ndo mahitaji ya wananchi kwa ustawi wa Taifa.
naomba kuwasilisha
 
Siamini kama ni mwongozo umetolewa labda niwe sijui maana ya neno hilo. Naamini lengo la Kanisa lilikuwa ni kuwahimiza waamini wake kushiriki katika utoaji wa maoni. Na mwisho wa siku anayetoa maoni ni raia wa Tanzania lakini lililo la muhimu aende kutoa maoni akiwa anajua ni nini anachotakiwa kutetea kwa ajili ya mustakabali wa maisha yake kama raia kwa ajili ya ustawi wa TAIFA LETU.

Na wakati mwingine kitu kama huna uhakika wa kilichoongelewa siyo vizuri kuchangia kwani michango ya aina hiyo huwa haisaidii kujenga badala yake kuna hatari ikasaidia kubomoa zaidi.
 
Siiamini kauli hii mpaka huo unaoitwa mwongozo uletwe hapa mezani. Jimbo kuu la Dar es Salaam lina askofu mkuu na halina maaskofu wengi kama mtoa uzi anavyodai. Askofu wa jimbo katoliki la Dar es Salaam ni Muadhama Polycarp Cardinal Pengo na ana msaidizi. Na hawa kamwe hawezi toa tamko la pamoja. Pengo ni kiongozi makini ambaye hawezi kukurupuka kutoa muuongozo. Leteni ushahidi hapa vinginevyo huu ni uzushi
 
kanisa katoliki tumewazoea ni miongozo hata kipindi cha uchaguzi walitoa muongozo na hakusaidia kitu bado slaa alianguka
 
Back
Top Bottom