pumbatupu
JF-Expert Member
- Jul 20, 2011
- 256
- 82
Sikuwepo muda flani hapa Jamvini kwa amani ya Bwana naamini wote hatujambo. Sasa wadau wa MMU mimi najaribu kuuliza hivi kuna wakati ni muhimu kusema uongo kwenye Mahusiano?. Nasema hv kwa sbb ni majuzi tu mkewangu kaniambia kuwa mshahara wake umepanda.Mwanzoni nilipomuuliza alikataa. Ananiambia kuwa alinidanganya mwanzoni kwa sbb alitaka kuona ninaweza kufanya nini ili ku'supplement' kipato chetu. Kwa hiyo anadai alinidanganya kwa nia nzuri.Hivi hii inaweza kuwa sawa..'Kudanganya kwa nia nzuri'.