tindikalikali
JF-Expert Member
- Jan 14, 2011
- 4,855
- 1,117
Ni rafiki yangu toka o'level, hatujawahi kwaruzana wala kupishana kauli. Kwa kipindi chote nimejitahidi kumuonesha kwa vitendo kwamba namjali na kumpenda. Miaka imepita tukiwa marafiki na nimeweza kumfahamu vizuri kitabia. Hivi majuzi niliamua kuvunja ukimya, na nimwandikia hivi "naomba unielewe ninachotaka kusema, sidhani kama itakuwa busara kwangu kumung'unya maneno, kwa kifupi nakuhitaji uwe mpenzi wangu, sisemi haya kwa bahati mbaya kwani najua nini nafanya na kumaanisha. Kumbuka ni ngumu kuukwepa ukweli, hata nisingesema leo basi ningesema kesho, naomba hekima na busara itawale maamuzi yako".....toka nimemtumia hiyo text kauchuna kimya wakati siyo tabia yake, sifikiri kama nimekosea kumwambia niliyomwambia, lakin nifanyeje ili nimlete katika mud yake ya mwanzo, maana nahisi hata urafik unaweza kwisha. Ushaur wenu wadau unahitajika.
UPDATED
Jamani nawashukuru wote mlionipa ushauri kunikosoa na kunipa zaidi. Tumepanga tukutane leo jioni, kitakachojiri nitawajuza. jumapili njema kwenu nyote
UPDATED
Jamani nawashukuru wote mlionipa ushauri kunikosoa na kunipa zaidi. Tumepanga tukutane leo jioni, kitakachojiri nitawajuza. jumapili njema kwenu nyote