sir.JAPHET
JF-Expert Member
- May 18, 2012
- 699
- 133
Na Pendo Fundisha, Mbeya MKUU wa Mkoa wa Mbeya, Abbas Kandoro, ametoa miezi miwili kwa uongozi wa Halmashauri ya Wilaya ya Mbarali kurudisha zaidi ya Sh bilioni mbili zilizotakiwa kutumika katika miradi mbalimbali ya maendeleo.
Fedha hizo zilipaswa kutumika katika idara ya elimu, afya, maji na kilimo, lakini hazikutumika, licha ya uongozi kueleza kuwa matumizi yake yalibadilishwa kutokana na sababu mbalimbali.
Agizo hilo alilitoa mjini hapa jana, katika kikao maalumu cha Baraza la Madiwani kilichokuwa kinapitia majibu na hoja za Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali kwa kipindi kinachomalizika.
Alisema katika michanganuo ya matumizi hayo, inaonyesha zaidi ya Sh bilioni moja zilizotakiwa kutumika katika miradi hiyo hazikutumika na hazieleweki zilipo.
Alisema kitendo cha halmashauri hiyo kudai fedha hizo zilikopwa na kutumika katika utawala pasipo kuomba ridhaa kutoka hazina ni makosa, kwa kuwa fedha yoyote ile ya Serikali inapaswa kufuata taratibu na misingi iliyojiwekea.
Mnadai kubadilisha matumizi ya fedha hizo, lakini mbona hata kwenye matumizi ya upande wa pili mliyotumia hayana viambatanisho, kwa kweli suala hili haliniingii akilini, alisema Kandoro.
Alisema hapo inaonyesha kuwapo kwa matumizi mabaya ya fedha hizo ambazo malengo yake makubwa yalilenga kumkomboa mwananchi kwa kutekeleza miradi iliyokusudiwa kutumika.
Naomba fedha hizo zirudishwe ndani ya miezi miwili kama mlivyonieleza ili fedha hizi ziingizwe katika matumizi halisi ya utekelezaji wa miradi ya maendeleo ya wananchi, alisema Kandoro.
Aidha, aliwataka wakuu hao wa idara kutambua kuwa wakati wa kufuja fedha za Serikali haupo kwa kuwa Serikali haiwezi kukaa na kuangalia jinsi wananchi wanavyoteseka kwa kukosa mahitaji muhimu kama elimu, maji na afya.
Mimi sijui fedha hizo mtazitolea wapi, ila ninataka zirudishwe na kwa hili siwezi kukubali kwa kuwa siwezi kuwajibishwa kutokana na uzembe na tamaa za watendaji wachache ambao kazi yao kubwa ni kuangalia matumbo, huku jamii ikiendelea kuteseka, alisema Kandoro.
[h=4]Toa Maoni yako kwa habari hii[/h]
Fedha hizo zilipaswa kutumika katika idara ya elimu, afya, maji na kilimo, lakini hazikutumika, licha ya uongozi kueleza kuwa matumizi yake yalibadilishwa kutokana na sababu mbalimbali.
Agizo hilo alilitoa mjini hapa jana, katika kikao maalumu cha Baraza la Madiwani kilichokuwa kinapitia majibu na hoja za Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali kwa kipindi kinachomalizika.
Alisema katika michanganuo ya matumizi hayo, inaonyesha zaidi ya Sh bilioni moja zilizotakiwa kutumika katika miradi hiyo hazikutumika na hazieleweki zilipo.
Alisema kitendo cha halmashauri hiyo kudai fedha hizo zilikopwa na kutumika katika utawala pasipo kuomba ridhaa kutoka hazina ni makosa, kwa kuwa fedha yoyote ile ya Serikali inapaswa kufuata taratibu na misingi iliyojiwekea.
Mnadai kubadilisha matumizi ya fedha hizo, lakini mbona hata kwenye matumizi ya upande wa pili mliyotumia hayana viambatanisho, kwa kweli suala hili haliniingii akilini, alisema Kandoro.
Alisema hapo inaonyesha kuwapo kwa matumizi mabaya ya fedha hizo ambazo malengo yake makubwa yalilenga kumkomboa mwananchi kwa kutekeleza miradi iliyokusudiwa kutumika.
Naomba fedha hizo zirudishwe ndani ya miezi miwili kama mlivyonieleza ili fedha hizi ziingizwe katika matumizi halisi ya utekelezaji wa miradi ya maendeleo ya wananchi, alisema Kandoro.
Aidha, aliwataka wakuu hao wa idara kutambua kuwa wakati wa kufuja fedha za Serikali haupo kwa kuwa Serikali haiwezi kukaa na kuangalia jinsi wananchi wanavyoteseka kwa kukosa mahitaji muhimu kama elimu, maji na afya.
Mimi sijui fedha hizo mtazitolea wapi, ila ninataka zirudishwe na kwa hili siwezi kukubali kwa kuwa siwezi kuwajibishwa kutokana na uzembe na tamaa za watendaji wachache ambao kazi yao kubwa ni kuangalia matumbo, huku jamii ikiendelea kuteseka, alisema Kandoro.
[h=4]Toa Maoni yako kwa habari hii[/h]