Kanali mstaafu kugombea ubunge Tarime kupitia CCM

ngoshwe

JF-Expert Member
Mar 31, 2009
4,131
931
Date::12/5/2009Kanali mstaafu atangaza kugombea ubunge Tarime kupitia CCM
broken-heart.jpg
Na Samson Chacha, Tarime
KANALI Mstaafu wa Jeshi la Wananchi (JWTZ), Mahende Kichonge (65)ametangaza kugombea Ubunge katika Jimbo la Tarime mwakani kupitia Chama cha Mapinduzi CCM.

Kichonge alitangaza nia hiyo wakati wa mazishi ya kaka yake aliyewahi kuwa Ofisa Utumishi Tawala wa Kwanza katika Wilaya ya Tarime na Mkaguzi wa Mahakama za Mwanzo nchini, Kichonge Mahende aliyefariki Novemba 30, mwaka huu na kuzikwa Desemba 4, mwaka huu kijijini kwake Kemakorere Kata ya Nyarero.

Katika mazishi hayo, alikuwepo kanali Raphael Isarra Chacha na kijana mkubwa wa marehemu Kichonge Luteni Kanali David Kichonge,na mamia ya waombolezaji, akiwemo Mkuu wa Wilaya ya Kwimba, Ryoba Kangoye Masero ambaye ni ndugu wa marehemu.

Akitoa kauli hiyo katika umati mkubwa wa waombolezaji waliofika katika mazishi hayo, Kanali Mahende alisema kuwa

"Mimi kama mwana Tarime ninayo haki ya kugombea Ubunge katika Jimbo langu hili la Tarime mwakani kupitia chama changu ambacho sitakihama daima cha CCM na ninazo sababu za kuwania kiti hicho, kwanza kuwaunganisha Jamii ya Kabila la Wakurya na kuwa kitu kimoja na kuondoa dhana potofu za mila zilizopitwa na wakati za kubaguana, kuwashirikisha wazee wa mila wa koo zote za kabila la Wakurya na kukomesha wizi wa mifugo kwa kushirikiana na Sungusungu,” alisema.


Kanali Mahende alisema endapo atachaguliwa atahakikisha barabara zote ambazo hazipitiki kwa urahisi zinafanyiwa matengenezo, kukamilisha madarasa na nyumba za walimu na kwamba ataiomba serikali kuongeza walimu katika shule za Sekondari za kata kutokana na kuwepo kwa tatizo la walimu.

Pia alisema ataanzisha vikundi vya vijana na Wazee kwa lego la kuwapatia mikopo ya kuanzisha miradi mbalimbali ya kiuchumi.
Naye Mkuu wa Wilaya ya Kwimba, Christopher Kangoye na Kanali David Gichonge waliwashukuru wananchi na marafiki waliofika katika shughuli za kumzika kaka yao Gichonge Mahende.

HIVI HAWA MAKANALI HUWA NI MAKADA WA CCM HUKO JESHINI????
 
Date::12/5/2009Kanali mstaafu atangaza kugombea ubunge Tarime kupitia CCM
broken-heart.jpg
Na Samson Chacha, Tarime
KANALI Mstaafu wa Jeshi la Wananchi (JWTZ), Mahende Kichonge (65)ametangaza kugombea Ubunge katika Jimbo la Tarime mwakani kupitia Chama cha Mapinduzi CCM.

Kichonge alitangaza nia hiyo wakati wa mazishi ya kaka yake aliyewahi kuwa Ofisa Utumishi Tawala wa Kwanza katika Wilaya ya Tarime na Mkaguzi wa Mahakama za Mwanzo nchini, Kichonge Mahende aliyefariki Novemba 30, mwaka huu na kuzikwa Desemba 4, mwaka huu kijijini kwake Kemakorere Kata ya Nyarero.

Katika mazishi hayo, alikuwepo kanali Raphael Isarra Chacha na kijana mkubwa wa marehemu Kichonge Luteni Kanali David Kichonge,na mamia ya waombolezaji, akiwemo Mkuu wa Wilaya ya Kwimba, Ryoba Kangoye Masero ambaye ni ndugu wa marehemu.

Akitoa kauli hiyo katika umati mkubwa wa waombolezaji waliofika katika mazishi hayo, Kanali Mahende alisema kuwa

"Mimi kama mwana Tarime ninayo haki ya kugombea Ubunge katika Jimbo langu hili la Tarime mwakani kupitia chama changu ambacho sitakihama daima cha CCM na ninazo sababu za kuwania kiti hicho, kwanza kuwaunganisha Jamii ya Kabila la Wakurya na kuwa kitu kimoja na kuondoa dhana potofu za mila zilizopitwa na wakati za kubaguana, kuwashirikisha wazee wa mila wa koo zote za kabila la Wakurya na kukomesha wizi wa mifugo kwa kushirikiana na Sungusungu,” alisema.


Kanali Mahende alisema endapo atachaguliwa atahakikisha barabara zote ambazo hazipitiki kwa urahisi zinafanyiwa matengenezo, kukamilisha madarasa na nyumba za walimu na kwamba ataiomba serikali kuongeza walimu katika shule za Sekondari za kata kutokana na kuwepo kwa tatizo la walimu.



HIVI HAWA MAKANALI HUWA NI MAKADA WA CCM HUKO JESHINI????

- Mkuu vipi wanajeshi wamekosa nini kwani? Au wao sio wananchi wenye haki sawa na wengine ya kuamini chama wanachokitaka?

Respect.


FMEs!
 
- Mkuu vipi wanajeshi wamekosa nini kwani? Au wao sio wananchi wenye haki sawa na wengine ya kuamini chama wanachokitaka?

Respect.

FMEs!
waende zao siasa na kushika bunduki ni vitu tofauti ndo maana tunawaona wakina Mkuchika wanakurupuka sasa
 
Nimetafuta sana ndani ya katiba yetu kama kuna kipengele kinachomkataza mwanajeshi au mtumishi yeyote mstaafu asigombee nafasi yeyote ya kisiasa nyumbani TZ,lkn sijakiona!

Sheria inakataza tu kwa mtumishi wa UMMA kujihusisha na siasa akiwa bado ni mtumishi wa serikali;kikomo chake cha kutoshiriki siasa kinagota pale ama anapoamua kuacha kazi kwa hiari yake mwenyewe ili ajitumbukize kwenye siasa au anapostaafu kazi!

Kwa maana hiyo basi ni haki yake ya msingi na ya kikatiba kwa Kanali huyu mstaafu kugombea;kama wana Tarime watamuona anafaa atashinda;then ataapishwa kuwa mbunge halali wa Tarime bila pingamizi lolote la kikatiba!
 
Agombee tu aone kama Chadema hawajamshinda! asije na bunduki tu.

Nimebaini kumbe huyu jamaa alisindwa kwenye kura za maoni mwaka 2005. Alikuwa anataka kugombea kwa tiketi ya CCM pale Kinondoni. Nchi hii inaendeshwa kijeshi.Hii ni baadhi tu ya mafisa waandamizi Jeshini ambao naongoza/wamewahi kuingoza hii nchi katika awamu ya 4:
  1. Luteni Kanali J.M Kikwete
  2. Capt. J. Chiligati
  3. Capt.G. Mkuchika
  4. Luteni Y. Makamba
  5. Maj. Gen S. Kalembo
  6. Kanali F. Massawe
  7. Generali T. Kiweru
  8. BRIG. GEN.E. Balele
  9. Kanali Anatori Tarimo
  10. BRIG. GEN.A . Ramadhani
  11. Kanali Enos Mfuru
  12. Kanali Issa Machibya
  13. Kanali Joseph Simbakalia
  14. Kanali Madaha
  15. Kanali Issa Njiku
  16. Kanali mstaafu Ayub Kimbau
  17. Kanali Elmon Mahawa
  18. Kanali Samwel Ndomba
  19. Luteni Kanali Serenge Mrengo
  20. Kanali Edmund Mjengwa
  21. captain Jaka Mwambi
  22. Comm. A. Rajabu
 
Agombee tu aone kama Chadema hawajamshinda! asije na bunduki tu.





Nimebaini kumbe huyu jamaa alisindwa kwenye kura za maoni mwaka 2005. Alikuwa anataka kugombea kwa tiketi ya CCM pale Kinondoni. Nchi hii inaendeshwa kijeshi.Hii ni baadhi tu ya mafisa waandamizi Jeshini ambao naongoza/wamewahi kuingoza hii nchi kisiasa katika awamu ya 4:
  1. Luteni Kanali J.M Kikwete
  2. Capt. J. Chiligati
  3. Capt.G. Mkuchika
  4. Luteni Y. Makamba
  5. Maj. Gen S. Kalembo
  6. Kanali F. Massawe
  7. Generali T. Kiweru
  8. BRIG. GEN.E. Balele
  9. Kanali Anatori Tarimo
  10. BRIG. GEN.A . Ramadhani
  11. Kanali Enos Mfuru
  12. luteni Kanal John Mzurikwao
  13. Kanali Issa Machibya
  14. Kanali Joseph Simbakalia
  15. Kanali Madaha
  16. Kanali Issa Njiku
  17. Kanali Ayub Kimbau
  18. Kanali Elmon Mahawa
  19. Kanali Samwel Ndomba
  20. Luteni Kanali Serenge Mrengo
  21. Luteni Kanali Benedict Kitenga
  22. Kanali Edmund Mjengwa
  23. Kapteni James Yamungu
  24. Luteni Kanali John Mzurikwao
  25. Kapteni Geoffrey Ngatuni
  26. Kapteni Assary Msangi
  27. Luteni Winfrid Ligubi
  28. Kapteni John Barongo
  29. Kapteni Malle
  30. Kapteni Evans Balama
  31. Kapteni Seif Mpembenwe
  32. Kapteni Mwapinga
  33. Luteni Abdallah Kihato
  34. Luteni Chiku Gallawa
  35. luteni Edward Ole Lenga
  36. Kapten John Komba
  37. Kapteni John Henjewele
  38. Luteni Chiku Gallawa
  39. Luteni Kanali Leopald Kalima
  40. Kapteni Seif Mpembenwe
  41. captain Jaka Mwambi
  42. Comm. A. Rajabu
 
Back
Top Bottom