Msomaji mwenzangu: Naomba unitegee sikio. Hapa Ulaya kamusi za matusi na maneno yenye sifa mbaya ziko madukani. Niwie radhi kama maoni yangu hapa yanazua karaha hata iwe kidogo miongoni mwenu lakini sina nia mbaya hata kidogo. Lazima tutambue kwamba lugha mchafu ndio sehemu muhimu sana isiyotengeka ya lugha yoyote duniani. Ni kiambato cha utamaduni wa lugha. Mimi nia yangu ni kutunga kamusi ya kiswahili yenye kujumlisha maneno mabaya/machafu kama matusi, laana, apizo na vingine vingi vya aina hiyo (yaana misemo ya kutukana, kukebehi, kukemea, kuaibisha, kufedhehesha na hali kadhaika) ambayo siku hizi hutumiwa katika jamii ya kisasa. Mara nyingi vijenzi hivi vya kilugha huboresha uelewa wetu kiroho na kiakili na kihisia wa wanadamu wenzetu tena huangaza sehemu zenye kina sana ubongoni mwa mtu.
Ikiwa mradi huu muhimu unakuvutia tafadhali niandikie kupitia anwani ya pepe yangu klf100@iolfree.ie. Afadhali toa maana ya msemo pia ili tusidanganyike kuhusu kusudi linalofichika humo ndani. Michango yote yanakaribishwa na yatakiriwa … Natanguliza shukrani za dhati
Ikiwa mradi huu muhimu unakuvutia tafadhali niandikie kupitia anwani ya pepe yangu klf100@iolfree.ie. Afadhali toa maana ya msemo pia ili tusidanganyike kuhusu kusudi linalofichika humo ndani. Michango yote yanakaribishwa na yatakiriwa … Natanguliza shukrani za dhati