Kampuni za sim zimekosa ubunifu?

Escobar

JF-Expert Member
Sep 16, 2011
574
440
Kitendo cha kumpigia mtu badala ya kuambiwa kama hapatikani au simu yake inaongea sasa kimegeuka kuwa ni sehemu ya MATANGAZO YA LAZIMA!

Tabia hii ambayo kampuni ya Tigo ndio vinara wa uozo huo inanichefua sana mpaka nimefikia hatua ya kununua laini ya zantel last friday ili kuepukana na matangazo ambayo siko interested nayo! Mimi sikusoma marketing na sinauhakika kama hii inayofanyika sasa ndio marketing yenyewe au ni umachinga tena wa kijinga kweli kweli maana unalazimishwa usikilize vitu usivyovihitaji kwanza then mwishoni ndio unaambiwa unayempigia hapatikani, thats stupid.

Kwa mimi ninayepiga simu nyingi kwa siku kulingana na shughuli zangu ni KERO YA AJABU SANA i hate this so much! Kwa mwendo huu ipo siku wale wanaotumia matangazo ya mabango makubwa kandokando ya mabarabara watakuwa wanatufunika nayo kwenye vioo vya magari ili tuyasome!

What a poor creativeness is this!
 
Back
Top Bottom