Kampuni iliyooza na miradi ya barabara za manispaa ya Kinondoni

Zamazamani

JF-Expert Member
Jun 13, 2008
1,859
763
Jamani kwa kweli uvumilivu umetushinda huku mtaani...kwa wakazi tunaoishi Victoria , Uporoto street, imekuwa kero kubwa kutoka kwa waliopewa jukumu la kutengeneza barabara za manispaa ya kinondoni ambao ni mradi wa World Bank....

Kampuni ya BADR EAST AFRICA..(kama sijakosea au kitu kama hicho).. .Nasikia walishakuwa blacklisted na Tanroads….Hawa jamaa ni hopeless kabisa nasikia sifa yao kubwa ni kuhonga hela nyingi ili kupata kazi,....hili linawezekana kabisa sababu jamaa hawana vifaa kabisa ..na walivyonavyo au walivyoazima vimechoka mno ...yaani inakatisha tamaa...wanatuharibia miundo mbinu yetu huku Victoria ......

Kwa kweli hakuna anayeelewa wanachofanya hawa jamaa.......ni zaidi ya mwaka mmoja sasa wanahangaika na kipande kifupi sana cha barabara...sasa wanachimbua na kusababisha matope na mitaro haieleweki na wameiziba muda mrefu maji yanafurika yakiwemo yale maji taka....kweli TUMECHOKA KABISA.....hatuwezi hata kuwashitaki kwa viongozi wa serikali ya mtaa au manispaa sababu yote haya wanayaona lakini wamesha legezwa...hawana la kufanya........

TUNAOMBA USHAURI TOKA KWA WASAMARIA WEMA ,TUFANYE NINI KATIKA HILI???WATU WA WORLD BANK MPO? AU NA NYIE WALEWALE?(NAJUA KUNA WANAOJUA KISWAHILI,ila nitadondosha ya kiingereza vilevile)
 
hii kampuni ni kichekesho wanajenga pia barabara ya bahari beach-ununio-boko ccm yani mwaka sasa kazi yao kumwa vifusi tuu!wana usumbufu sana maana mara wafunge barabara mara wafunge hawaeleweki
 
Back
Top Bottom