Jaguar
JF-Expert Member
- Mar 6, 2011
- 3,438
- 1,026
Kampuni za OILCOM,CAMELOIL,BP na ENGEN zimepewa masaa 24 kusitisha mgomo wao na kuanza kuuza mafuta kwa bei rasmi iliyotangazwa na Ewura.Endapo watakaidi amri,Ewura imetishia kuziburuza mahakamani.Wakati huo huo mheshimiwa Zito Kabwe ameshauri endapo kampuni hizi zitaendeleza mgomo,JWTZ iingilie kati kwa kuvamia vituo vya mafuta kinguvu na kuuza mafuta kwa wananchi.