Kenge (Eng)
JF-Expert Member
- Dec 7, 2006
- 543
- 156
Ndio nimeingia Bukoba jioni hii na nimebahatika kusikiliza kipindi cha kimoja ndani ya radio hii mnamo saa 3.30 usiku. kilichokuwa kinazungumzwa nimeshindwa kuelewa hasa muda wa kampeni zinaisha saa ngapi? Wakati kampeni kisheria zinaisha saa kumi na mbili radio hii inaanza kampeni dhidi ya mgombea wa CHADEMA.
Niliyoyasikia.
1. Lwakatare anaendesha kampeni za matusi dhidi ya mgombea wa CCM (Kagasheki).
2. Chadema wanasema mgombea wa CUF (Kasimbazi) ni kibaraka wa CCM na amepandikizwa na Kagasheki na pale pale alihojiwa studio na kutoa msimamo wake kama kweli ni kibaraka, alichosema dhidi ya mgombea wa CHADEMA wazi alidhibitisha ukibaraka.
3. Dai kuwa mbunge wa CCM Kagasheki alihadi madawati mia kwa shule ya msingi BUNENA na hakutekeleza, walijibu kuwa mbunge anatoa ahadi na aliyeahadiwa anatakiwa kukumbusha hivyo hakutekeleza kwa sababu DIWANi wa Bunena (CUF) hakufuatilia na shule yenyewe "wanahisi iliyakataa madawati ahyo kwa sababu ni ya Kikristu RC ndo maana hawakufuatilia. Pamoja na kuahidi shule yenyewe haikuwa na sehemu ya kuweka madawati hayo kwani misheni, RC hawahitaji madawati. Lwakatare anasema Kagasheki tapeli vipi, hana sera ni matusi tu chagua CCM.
4. Mzungumzaji mwingine mgombea udiwani wa kata ya Nyanga (Deus) yeye alisema mgombea wa CUF ni safi na mikutano yake haina matatizo kwa CCM kwani anayoongea ni mazuri na anakiri kuwa CCM ni kiboko. Ndio maana hata hapa tunaye kudhibitisha kuwa CHADEMA hawana sera na mgombea wa CHADEMA ndio kibaraka wa CCM na kumtaka atoe maoni yake kuhusu CHADEMA. HApoooo msaada kwenye TUTA. Kutaja mapungufu na ahadi hewa zisizotekelezeka ni MATUSI.
Redio hii inapiga kampeni za Chagua CCM, Chagua KAGASHEKI, Chagua Dkt KIKWETE ili Radio iendelee kuwapo. saa 24 hakuna kitu kingine zaidi ya kuhimiza na kutangaza ratiba za wagombea wa CCM ubunge na udiwani. Hapo maadili ya vyombo vya habari yapo?
Redio hii imesajiliwa kisheria?
Wataaluma nisaidie.
HIVI tuna RADIO za Kampeni za vyama fulani na waandishi au watangazaji walio bias kwa CCM tu? Naomba kuelimishwa.
Niliyoyasikia.
1. Lwakatare anaendesha kampeni za matusi dhidi ya mgombea wa CCM (Kagasheki).
2. Chadema wanasema mgombea wa CUF (Kasimbazi) ni kibaraka wa CCM na amepandikizwa na Kagasheki na pale pale alihojiwa studio na kutoa msimamo wake kama kweli ni kibaraka, alichosema dhidi ya mgombea wa CHADEMA wazi alidhibitisha ukibaraka.
3. Dai kuwa mbunge wa CCM Kagasheki alihadi madawati mia kwa shule ya msingi BUNENA na hakutekeleza, walijibu kuwa mbunge anatoa ahadi na aliyeahadiwa anatakiwa kukumbusha hivyo hakutekeleza kwa sababu DIWANi wa Bunena (CUF) hakufuatilia na shule yenyewe "wanahisi iliyakataa madawati ahyo kwa sababu ni ya Kikristu RC ndo maana hawakufuatilia. Pamoja na kuahidi shule yenyewe haikuwa na sehemu ya kuweka madawati hayo kwani misheni, RC hawahitaji madawati. Lwakatare anasema Kagasheki tapeli vipi, hana sera ni matusi tu chagua CCM.
4. Mzungumzaji mwingine mgombea udiwani wa kata ya Nyanga (Deus) yeye alisema mgombea wa CUF ni safi na mikutano yake haina matatizo kwa CCM kwani anayoongea ni mazuri na anakiri kuwa CCM ni kiboko. Ndio maana hata hapa tunaye kudhibitisha kuwa CHADEMA hawana sera na mgombea wa CHADEMA ndio kibaraka wa CCM na kumtaka atoe maoni yake kuhusu CHADEMA. HApoooo msaada kwenye TUTA. Kutaja mapungufu na ahadi hewa zisizotekelezeka ni MATUSI.
Redio hii inapiga kampeni za Chagua CCM, Chagua KAGASHEKI, Chagua Dkt KIKWETE ili Radio iendelee kuwapo. saa 24 hakuna kitu kingine zaidi ya kuhimiza na kutangaza ratiba za wagombea wa CCM ubunge na udiwani. Hapo maadili ya vyombo vya habari yapo?
Redio hii imesajiliwa kisheria?
Wataaluma nisaidie.
HIVI tuna RADIO za Kampeni za vyama fulani na waandishi au watangazaji walio bias kwa CCM tu? Naomba kuelimishwa.