Kampeni ya Ubunge Arusha Mjini - Batilda Burian Vs Lema

KATI YA BATILDA NA LEMA YUPI ATIBUKA KIDEDEA?


  • Total voters
    52
kaka nakubaliana nawe kabisa, "huyo" hatufai na riferensi za mheshmiwa alizotoa hazitoshi kutushawishi, mbona hajamtaja "John Terry"
 
Hili halina ukweli hata kidogo. Kwanza mfumo wetu wa maisha na ule wa kimagharibi ni tofauti kidogo. Mtu akiwa na mkewe/mumewe anakumbana na mengi kuanzia presha za extended family, kucheat nk. Lakini pia nikutolee mfano mdogo tu wa watu waliowahi kudivorce kutoka huko unakokuita kwenye maendeleo. Kuna Reagan (USA) na Sarkozy (France) achana na yule muhun wa Italy.

Heshima kwako anfaal.

Mkuu nakubaliana na wewe lakini nachouliza ni hiyo namba ya wanaume watatu wewe haikutishi.
 
Watu wameichoka CCM. Batilda hatapita. Nakumbuka jinsi alivyokuwa mkali alipokuwa Chief Whip. Bora apite Lyimo!
 
TLP jimbo la Arusha mjini wanazindua kampeni zao leo kwenye uwanja wa soko la Kilombero.

Msafara mrefu wa magari,pikipiki na baiskeli wa mgombea ubunge Bwana M Lyimo tayari umesababisha kero ya msongamano wa magari hasa barabara inayotokea maeneo ya polisi,mnara wa azimio la Arusha kuelekea stend ya mabasi.Jeshi la polisi linaongoza msafara huku askari wake wakionekana wakiwa tayari kudhibiti vurugu zozote zinazoweza kutokea.Hongera jeshi la polisi mkoa Arusha hasa kamanda Matei,inaonyesha wamejiandaa vyema kudhibiti vurugu kipindi cha uchaguzi.

Wapita njia wengi wako katika hali ya mshangao mkubwa kuona TLP imeweza kuandaa maandamano makubwa kiasi hiki kwani wengi wanadhani chama hakipo na mpambano ni baina ya CCM na CHADEMA.Wanachama wengi wa CCM tawi la Bondeni mahali ambapo ni ngome kuu ya Mama Batilda Salha Buriani wanakiri Bwana Lyimo anaweza kutoa upinzani wasioutarajia kwasababu hawamjui udhaifu wake tofauti na mgombea wa CHADEMA Bwana G Lema anayetumia jukwaa kumshambulia mgombea wao mambo binafsi badala ya kuwaeleza atawafanyia nini wapiga kura wa Arusha.
 
Hongera Ngongo umeleta hoja ya maana sana.

umesahau jambo moja muhimu sana kuhusu udhaifu wa batilda salha.kwanza kabadili dini ukubwani kwasababu ya mwanaume,huu nao udhaifu angekuwa na mtu wa msimamo asingebadili dini eti kwasababu ya kuolewa tu.Tumeshuhudia akina mama kibao wakiolewa na wakristo au waislam wakiendelea kuabudu dini zao.

batilda ameolewa na kuachika mara tatu.Huu nao ni udhaifu kuachwa mara tatu ni doa kubwa sana.

Batilda kaolewa Zanzibar ni kwanini asigombee huko alikoolewa au anataka kujifanya Anna kilango.

Batilda ana uhusiano wa karibu usikuwa wa kawaida na lowassa

Duh mkuu meza mate its better mjadili hoja sio watu jamani jadili uwezo wa mtu kwa elimu yake na muonekano wake ukirefer valid evidences kuacha au kuachwa, masuala ya dini upagani hayo ni maisha binafsi ya mtu.
 
Duh mkuu meza mate its better mjadili hoja sio watu jamani jadili uwezo wa mtu kwa elimu yake na muonekano wake ukirefer valid evidences kuacha au kuachwa, masuala ya dini upagani hayo ni maisha binafsi ya mtu.

Heshima kwako Sokomoko,

Mkuu CCM sikuhizi ukuitaja EPA wanakwambia umetukana.wanataka uzungumzie sere tu hawataki uzungumzie watu wataozitekeleza hizo sera amabo ni muhimu sana.Watu wa hovyo sirahisi kutekeleza sera hataziwe nzuri kiasi gani mkuu wangu.Hili limekuwa ni tatizo kubwa sana kwa nchi yetu ya Tanzania,tunakubali kuongozwa na watu wa hovyo wasiozingatia maadili hata chembe.huwezi kuwa kiongozi mzuri kwa taifa wakati uongozi wa familia yako umekushinda.
 

Heshima kwako Sokomoko,

Mkuu CCM sikuhizi ukuitaja EPA wanakwambia umetukana.wanataka uzungumzie sere tu hawataki uzungumzie watu wataozitekeleza hizo sera amabo ni muhimu sana.Watu wa hovyo sirahisi kutekeleza sera hataziwe nzuri kiasi gani mkuu wangu.Hili limekuwa ni tatizo kubwa sana kwa nchi yetu ya Tanzania,tunakubali kuongozwa na watu wa hovyo wasiozingatia maadili hata chembe.huwezi kuwa kiongozi mzuri kwa taifa wakati uongozi wa familia yako umekushinda.

Mimi nadhani kuna mengi sana yanayomfanya mtu awe kiongozi bora bila kutizama ya kifamilia na dini.... hivi hujui kuwa kwa jinsi Hilter alivyokuwa akiogopewa lakini kwa mkewe alikuwa mboga kabisa? Au Rais fulani hukumbuki alipigwa na kitu na waifu wake mpaka akawa anatembelea mguu wa tatu? naheshimu ufaragha wa mtu na kiongozi bora sio lazima atoke chadema na cuf hata CCM wapo na naweza kuwataja.....ane kilango, samwel sitta etc etc sio wote wenye mawazo mgando wengine wanapambanunua na kujua pumba na mchele TAFAKARI
 
Mimi nadhani kuna mengi sana yanayomfanya mtu awe kiongozi bora bila kutizama ya kifamilia na dini.... hivi hujui kuwa kwa jinsi Hilter alivyokuwa akiogopewa lakini kwa mkewe alikuwa mboga kabisa? Au Rais fulani hukumbuki alipigwa na kitu na waifu wake mpaka akawa anatembelea mguu wa tatu? naheshimu ufaragha wa mtu na kiongozi bora sio lazima atoke chadema na cuf hata CCM wapo na naweza kuwataja.....ane kilango, samwel sitta etc etc sio wote wenye mawazo mgando wengine wanapambanunua na kujua pumba na mchele TAFAKARI

Heshima kwako Sokomoko,

Sijazungumzia dini ya Mama Batilda hata kidogo,najua anao uhuru wa kuabudu dini aitakayo kama ilivyoainishwa kwenye katiba ya JMT.Naamini kiongozi mzuri anaanza kuonekana tangu akiwa na famila yake na si vinginevyo mkuu wangu.

Habari za Rais fulani kupigwa na mke wake hadi kutembea na mguu wa tatu [magongo] nadhani hizo ni habari za mitaani hazina ushaidi wowote.

Unapotaka kuwa kiongozi lazima ujue ufaragha unatoweka kabisa,maisha yako yatazungumzwa,yatachunguzwa na jamii kuhabarishwa,laukama hutaki basi unaachana na mambo ya siasa [uongozi]
 
Tarehe 27-08-2010 Niliona msafara wa Mgombe wa ubunge Arusha (Dk Batilda) , alikuwa na msafara wa pikipiki zisizo pungua 30 baskeli, magali yasiyo pungua 40..Nilishituka huyu mama jeuri hii kaipata wapi?, Nikauliza Nikaambiwa ni mtu wake na Lowasa na siku ya kurudisha Form ilikuwa balaa..Magari, mikokoteni, basikeli, pikipiki..nikadokezwa anacho kifanya ni toyo yako anakujazia tank la mafuta na TZS 10000 na msosi sijui watu wa magari wanapata kiasi gani...wengine wana bandika mapicha yake kwenye magari kisa eti ukiwa na bendera ya CCM hakuna trafic atakeye thubutu kumkamata..mama lishe na wafanya biashara ndogondogo nao wanaweka bendera ya CCM hakuna mgambo atae mkamata hasa kwa kipindi hiki hata kama anafanya biashara sehemu ambayo haitakiwi...Je hawa jamaa wanajiita TAKUKURU hawalilioni hili....au hii siyo rushwa
 
Mgombea ubunge Arusha mjini kwa tiketi ya TLP Bwana M Lyimo jana alizindua kampeni zake kwenye uwanja wa soko la Kilombero mjini Arusha.
Bwana M Lyimo aliwaambia umati mkubwa wa watu waliohudhuria ufunguzi wa kampeni kwamba hatamzunguzia mtu /chama au wagombea wengine bali kampeni zake zitajikita zaidi kuwaambia wapiga kura atawafanyia nini iwapo watamchagua.Bwana Lyimo aliwaambia wananchi akichaguliwa atatoa kipaumbele kwenye mambo matano katika kipindi cha miaka mitano.

[1] Atahakikisha mapato ya jiji la Arusha yanatumika katika shughuli za maendeleo badala ya fedha nyingi kutumika kwenye vikao,warsha,semina,makongamano na safari za viongozi zisizo na faida kwa jiji la Arusha.

[2] Mapato ya jiji la Arusha pamoja na ruzuku toka serekali kuu kwa mujibu wa bajeti yalikadiriwa kufikia tsh bilion 30 kwa mwaka lakini kwa sasa mapato yanakusanywa ni chini ya bilion 20 kwa mwaka.Atahakikisha anaziba mianya ya ukwepaji kodi na kubuni vyanzo vipya bila kumuumiza mwananchi wa kawaida.

[3] Ataimarisha huduma za afya hasa afya mama na mtoto.Hali ya Hosipital ya mkoa wa Arusha [Mt Meru] ni mbaya sana akina mama wanaokwenda kujifungua wanalala chini kwasababu ya wingi wao.Jibu la tatizo ni kujenga hospital za kata badala kila mgonjwa kukimbilia MT Meru Hospital ambayo imelemewa na wagonjwa wengi.

[4] Ataimarisha elimu ya msingi na sekondari na kutilia mkazo ujenzi wa nyumba za waalimu,vifaa vya kufundishia.pia alizumzia sehemu za wazi na viwanja vya michezo ambavyo hivi sasa vimeuzwa kwa matajiri atapigania kurejeshwa ili watoto wapate sehemu za michezo.

[5] kuboresha mazingira ya jiji la Arusha ambalo hivi sasa linaongoza kwa uchafu kwa kuweka sheria ndogo ndogo zitakazo wabana wachafuzi wa mazingira.Pia alisisitiza ujenzi wa barabara za jiji la Arusha angalau kilometa kumi kila mwaka.

Mwisho alizumzia elimu ya wapiga kura kutambua umuhimu wa kura zao na kukazia kuutukuza utaifa wa Tanzania 'Tanzania kwanza mengine baadae'Aliwataka watanzania kurejesha enzi za kuthamini nchi yao,alisisitiza miaka ya nyuma Tanzania ilikuwa ikisifika kwa uzalishaji wa katani,kahawa na almasi siku hizi tunazalisha dhahabu nyingi lakini hakuna mtanzania anaeona fahari hiyo kwasababu hawaoni matunda yake.
 
Ngongo, asante kwa uchambuzi yakinifu kuhusu kinyanganyiro cha ubunge Arusha. Ninachokiona hapo ni kwa TLP na Chadema kugawana kura za upinzani, hivyo CCM kupita kwa ulaini. Mikoa ya Kaskazini ni mikoa yenye vuguvugu la upinzani, watu hawauzi uhuru wao kwa shibe ya siku moja 'pilau', au kwa t-shirt na kofia, lakini inapotokea wapinzani kupingana, hivi ni vita vya panzi, faida kwa kunguru.

Uongozi ni kipaji na uwezo na sio elimu, japo elimu ni just an added advantage, kama mtu ana uwezo wa uongozi hata darasa la saba, atakuwa kiongozi bora, ndio maana kuna mababu zetu hawakusoma, lakini walikuwa viongozi wazuri tuu wenye busara. Wapinzani lazima waungane, vinginevyo Arusha hiyo...CCM!.

Kaka,

Ngongo na Kabonde ni mtu mmoja ni mpigadebe wa mgombea wa TLP...Ukweli ni huyu jamaa anahitaji kuonana na wenziwe wa Bumbuli na Kyela waweze kutambua kuwa propaganda hizi za ujanjaujanja kamwe hazilipi...Sitashangaa kuwa huy ni huyohuyo mgombea...Lyimo wa TLP
 

Heshima kwako HM Hafif,

Mkuu nilitegemea ungesoma hoja vizuri na ungekuja na majibu ya kukataa au kuunga mkono yote niliyoandika kuhusiana na Mama Batilda Buriani badala yake unakuja na viroja kwamba ni chaguo la wengi Arusha.Mkuu hata Lowassa pamoja na madudu yake kibao bado ni chaguo la wengi Monduli vivyo hivyo Rostam ni chaguo la wengi Igunga.

Asome hoja zikowapi zaidi ya propaganda zako......Nini madudu ya Batilda Burian?? Je Lema ana nini cha kumzidi Batilda?? Hivi Phd ya Batilda ni ya nini na Phd ya Lyimo ni ya nini na kutoka vyuo gani? Uzoefu wa Batilda upo wazi, nini uzoefu wa Lyimo ambao tutautumia kumpima?? Kama chama hivi kweli TLP kuna chma zaidi ya nafasi ya kisiasa ya LYATONGA MREMA?? Propaganda zako NGONGO/KABONDE zinaonyesha wazi mtazamo mgando ulio nao kuhusu wanawake ambao ndio unaotawala katika chama cha msimu cha TLP. No wonder katika wote waliopo huko mkampata Mr Cut and Paste Book Writer/Mission town Mtamwega kupeperusha bendera yenu ya Urais......

Mwacheni Batilda wa watu kabla hamjaamsha mnaodhani wamelala....

Omarilyas
 
Mgombea ubunge kwa tiketi ya CHADEMA Bwana G Lema amekana kumtukana Mama Batilda Buriani matusi ya nguoni wakati wa kampeni zake.Bwana G Lema alisema alichokisema kuhusu maisha ya Mama Batilda kuolew na wanaume watatu ni kweli na anaushahidi wa kutosha.pia alisisiza Mama Batilda kaolewa Zanzibar kuwaambia wapiga kura si dhambi bali kuwatahadharisha hatari iliyopo mbele yao ya kuongozwa na mtu mwenye makazi Zanzibar tofauti na yeye anaishi Arusha.

Bwana Lema amehaidi kuimarisha huduma za afya,elimu,miundombinu na huduma za uhakika za maji jijini Arusha.Pia Bwana Lema amevishutumu vyama vya upinzani kwa kukataa kushirikiana kuiondoa CCM madarani.alisema anashindwa kuona mantiki ya vyama vya vya upinzani kushindwa kumuunga mkono kwa kumsimamisha pekee yake kupambana na Mama Batilda mjini Arusha badala yake TLP na CUF vimewasimamisha wagombea kwa nafasi za ubunge na udiwani Arusha mjini.

Bwana Lema amehaidi kulifikisha suala la uraia wa Mama Batilda kwenye vyombo vinavyohusika ili sheria ichukue mkondo wake.
 
Mwanaume anasema viti maalum viondolewe na wanawake wagombee na kupambana sawa na mgombea mwanaume.

Akijitokeza mwanaume kugombea ubunge ni sawa, akijitokeza mwanamke, ana jeuri ya mwanaume au watu kuuliza jeuri anaitoa wapi.

Mwanaume wakiwa na girlfriend 100, tena sometimes 10 at one time it is okay tena ni kidume cha mbegu. Akitokea mwanamke kaolewa mara 3, hana maadili.

Asante mke kwa kukubali kuolewa, asante Mama kwa kukubali kuzaa. Ikitokea siku moja hawa wanawake wanaodharauliwa na wanaume wakagoma kuolewa au kuzaa...... tutatafutana.
 
Asome hoja zikowapi zaidi ya propaganda zako......Nini madudu ya Batilda Burian?? Je Lema ana nini cha kumzidi Batilda?? Hivi Phd ya Batilda ni ya nini na Phd ya Lyimo ni ya nini na kutoka vyuo gani? Uzoefu wa Batilda upo wazi, nini uzoefu wa Lyimo ambao tutautumia kumpima?? Kama chama hivi kweli TLP kuna chma zaidi ya nafasi ya kisiasa ya LYATONGA MREMA?? Propaganda zako NGONGO/KABONDE zinaonyesha wazi mtazamo mgando ulio nao kuhusu wanawake ambao ndio unaotawala katika chama cha msimu cha TLP. No wonder katika wote waliopo huko mkampata Mr Cut and Paste Book Writer/Mission town Mtamwega kupeperusha bendera yenu ya Urais......

Mwacheni Batilda wa watu kabla hamjaamsha mnaodhani wamelala....

Omarilyas

Wakubwa kuna hii pettition inaendeshwa na nani sijui kuhusu proposed Serengeti highway

Gonga hapa STOP THE SERENGETI HIGHWAY - Sign the Petition | Change.org

Dunia nzima inapiga kelele ujenzi wa barabara serengeti Mama Batilda hatujamsikia akisema chochote.wewe unakuja na pumba zako eti tumwache Batilda ana uzoefu wa kutosha wakati ameshindwa kutoa tamko kama waziri anayeshughulikia mazingira.
 
Tunajua Mama Batilda anauzoefu wa kuwazuia wabunge wasijadili hoja ya RICHMOND.Ukiniuliza sababu za Omarlyas kumtetea Mama Batilda nashindwa kuelewa na pengine hii ni sababu tosha ufisadi unaendelea kutamalaki Tanzania.

Mtu yuko tayari kumtetea fisadi kwasababu ni ndugu yake,rafiki yake,jirani yake,kabila lake,dini yake,shangazi yake au mjomba.baba au chama chake.Omarlyas anaangukia katika kundi moja wapo niliyoyataja.Sina haja ya kubishana / ligi ya kipuuzi.
 
Mwanaume anasema viti maalum viondolewe na wanawake wagombee na kupambana sawa na mgombea mwanaume.

Akijitokeza mwanaume kugombea ubunge ni sawa, akijitokeza mwanamke, ana jeuri ya mwanaume au watu kuuliza jeuri anaitoa wapi.

Mwanaume wakiwa na girlfriend 100, tena sometimes 10 at one time it is okay tena ni kidume cha mbegu. Akitokea mwanamke kaolewa mara 3, hana maadili.

Asante mke kwa kukubali kuolewa, asante Mama kwa kukubali kuzaa. Ikitokea siku moja hawa wanawake wanaodharauliwa na wanaume wakagoma kuolewa au kuzaa...... tutatafutana.


Duh hili nalo neno.Hakuna mtu anaekataa mwanamke kugombea nafasi za kisiasa kinachogomba au ninachokiangalia ni uwezo wa mtu.kamwe hatuwezi kumchagua mtu kwasababu ni mwanume au mwanamke tunamchagua mtu kwakuwa ana uwezo na si vinginevyo.Hoja yangu kubwa kuhusu Mama Batilda ni uwezo wake unatia shaka shaka nyingi,nimejaribu kutaja mbili na nikaomba wengine wachangie wamekuja wakaongeza hilo la kuolewa mara tatu pia ikumbukwe mgombea wa CHADEMA kalisema hili Mama Batilda badala ya kujibu kakimbilia kushtaki kwa msimamizi wa uchaguzi kwamba katukanwa tunasubiri majibu ya msimamizi wa uchaguzi tujue kama ni matusi hayo ua vinginevyo.
 
Safi sana Lema.Hii sera endelea nayo hadi mwisho,utashinda kwa kishindo:becky::becky::becky:
 
Tunajua Mama Batilda anauzoefu wa kuwazuia wabunge wasijadili hoja ya RICHMOND.Ukiniuliza sababu za Omarlyas kumtetea Mama Batilda nashindwa kuelewa na pengine hii ni sababu tosha ufisadi unaendelea kutamalaki Tanzania.

Mtu yuko tayari kumtetea fisadi kwasababu ni ndugu yake,rafiki yake,jirani yake,kabila lake,dini yake,shangazi yake au mjomba.baba au chama chake.Omarlyas anaangukia katika kundi moja wapo niliyoyataja.Sina haja ya kubishana / ligi ya kipuuzi.

Inaonyesha wazi usivyojua hata hiyo kazi ya ubunge ama uwaziri ilivyo. Kabla kujaongelea suala la batilda alipokuwa Chief Whip ni muhimu ukatambua nini maana ya chief whip katika mabunge yetu. Na pia jaribu kuulizia nini maana ya uwaziri na prnciple ya collective responsibility katika governance of any society ndio uanze kutoa shallow critics kama unazozitoa hapa.

Pili kama wewe umeamua kumpigia debe LYIMO kwa ukabila wako usidhani kila mtu anamitazamo kama yako. Mimi sina undugu wala ujamaa na Batilda na wala hajawahi kunipa kitu wala sijawahi kufikiria kutaka kitu chochote kutoka kwake. Lakini nimefuatilia harakati zake kisiasa na kiuongozi ikiwemo hata kabla hajawa waziri na pia katika nafasi yake kama Chief Whip na najua perfomance yake lakini zaidi haiba ya heshima kwa watu ni moja ya nguzo kuu za uwezo wake kiuongozi na hicho ndicho kinafanyacho nimuone kuwa chaguo bora kuliko hao jamaa zako LEMA na LYIMO (ambaye naamini yaweza kuwa ndiye wewe).

Lakini pia ni siasa hovyohovyo kama zenu hapa ambazo nikilinganisha na ustaarabu na heshima ya Batilda ndio inanipelekea kujitoa mstari wa mbele kumpigania dhidi ya siasa chafu zenu??

Zaidi ni huu mtazamo hasi dhidi ya wanawake ambao mnao uonyesha hapa na katika kampeni zenu ndizo zinanitia moyo zaidi ya kusimama naye kwani to me male chauvinist and corrupt buffoon are all the same and have to be stopped from dominating our political arena...
 


Duh hili nalo neno.Hakuna mtu anaekataa mwanamke kugombea nafasi za kisiasa kinachogomba au ninachokiangalia ni uwezo wa mtu.kamwe hatuwezi kumchagua mtu kwasababu ni mwanume au mwanamke tunamchagua mtu kwakuwa ana uwezo na si vinginevyo.Hoja yangu kubwa kuhusu Mama Batilda ni uwezo wake unatia shaka shaka nyingi,nimejaribu kutaja mbili na nikaomba wengine wachangie wamekuja wakaongeza hilo la kuolewa mara tatu pia ikumbukwe mgombea wa CHADEMA kalisema hili Mama Batilda badala ya kujibu kakimbilia kushtaki kwa msimamizi wa uchaguzi kwamba katukanwa tunasubiri majibu ya msimamizi wa uchaguzi tujue kama ni matusi hayo ua vinginevyo.

Nimekuuliza, nini uzoefu wa LYIMO ambao tunapaswa kuutumi kumpima na hata elimu yake unayotamba nayo hapa ni ya nini na alipata wapi hujajibu kitu bado. Hizo ndio hoja na sio propaganda zako za bei rahisi hapa....
 
Back
Top Bottom