Kambi ya mateso yagunduliwa Zimbabwe

sulphadoxine

JF-Expert Member
Nov 1, 2010
2,257
645
BBC Panorama imegundua kwamba, kambi ya mateso inayosimamiwa na majeshi ya usalama ya Zimbabwe inafanya shughuli zake katika eneo lenye utajiri wa almasi, Marange.
Kipindi hicho kilizungumza na walioathirika hivi karibuni wakielezea walivyopigwa sana na kudhalilishwa kijinsia.
110808105313_zimbabwe_diamonds_304x171_bbc_nocredit.jpg
Almasi ya Zimbabwe


Madai hayo yanatolewa huku Umoja wa Ulaya EU ukishinikiza kuruhusu baadhi ya almasi zilizopigwa marufuku kutoka nchi hiyo inayoongozwa na Rais Robert Mugabe kurejeshwa kwenye masoko ya dunia.
Serikali ya Zimbabwe haijasema lolote kuhusu utafiti huo wa BBC.
Katika nyaraka iliyoonekana na BBC, EU ulisema kuwa sasa una imani kuwa migodo miwili eneo hilo zinafikia viwango vya kimataifa na kutaka almasi zinazoztoka eneo hilo kuidhinishwa haraka iwezekanavyo ili ziuzwe nje, ambayo itaondoa kizuizi cha biashara kilichowekwa mwaka 2009.
Kuzuiwa huko kuliwekwa na Kimberly Process (KP), shirika la kimataifa linalosimamia almasi, kufuatia ripoti za mauaji ya watu chungu nzima na udhalilishaji unaofanywa na majeshi ya usalama ya Zimbabwe katika eneo la machimbo la almasi huko Marange.
 
Back
Top Bottom