Le Grand Alexei
Senior Member
- Nov 9, 2011
- 116
- 83
Katika hali ya kushtusha kambi ya mwanasiasa mkongwe, mashuhuri na maarufu sana mh Edward Lowassa imezidi kuzorota ndani ya chama hicho kikongwe kilichojaa mizengwe na makundi makubwa ya kuwania urais 2015.
Kuzorota huko kumetokana na mambo mengi yakiwemo wasiwasi uliotanda ndani ya kambi hiyo kuwa waziri mkuu huyo mstaafu ana matatizo makubwa ya kiafya na hivyo kufifiza matumaini ya kuwa mgombea muafaka wa kambi hiyo. Hili linazidi kuwa kikwazo kwa kambi hiyo kwa kuwa Lowassa hapendi kuona mtu mwingine yeyote katika kambi hiyo anatamani kuwa rais zaidi ya yeye tu.
Habari za ndani ya kambi hiyo zinasema kuwa Lowassa alikorofishana na Emmanuel Nchimbi pale tu aliposema wawe na plan 'B' endapo itatokea kuwa yeye Lowassa ameshindwa kugombea Urais, na plan 'B' hiyo iwe kijana mwenye nguvu na afya bora kama Nchimbi! Toka aseme maneno hayo wakubwa hawa hawapatani tena kama zamani na kuna ushahidi kwamba Nchimbi haitwi tena kwenye vikao mbalimbali vya kambi hiyo.
Wasiwasi huo umeonekana ukisababisha uaminifu kwa kambi hiyo upungue nguvu sana na watu waanze kutazama fursa zilizopo kwenye makambi mengine yanayoibuka kila siku na kujikuta yakiwa na nguvu kubwa. wengi wanahisi anguko la Lowassa 2015 lisije kuwa anguko lao pia, wanaanza sasa kuchukua chao mapema.
Pamoja na sababu hiyo, nyingine kubwa inayotajwa kuisambaratisha kambi hiyo ni maamuzi magumu na yaliyoonekana kutoiunga mkono kambi hiyo yaliyofanywa na vikao mbalimbali vya maamuzi katika chama mfano maamuzi ya kuyafyeka majina ya watu walioonekana vinara wa siasa za kundi hilo kama akina Hussein Bashe, ambaye anaonekana kuwa ni nguzo muhimu ndani ya kambi hiyo yenye ufuasi kwa Lowassa, pia kuna vijana wengine ndani ya UVCCM waliokatwa majina yao bila sababu za msingi kujulikana - hapa mfano mzuri ni Naibu katibu mkuu wa UVCCM Zanzibar Jamal Kassim, aliyekuwa akigombea Uenyekiti wa Taifa wa UVCCM na aliyekuwa anapewa nafasi kubwa ya kushinda kama jina lake lingeteuliwa na NEC ya CCM, pia Sango Kasela ambaye aligombea nafasi ya Makamu Mwenyekiti UVCCM
Sababu kubwa ya tatu ya kuanguka kwa kambi hii ni kushindwa kwa makada wa chama hicho kwenye chaguzi za ndani ya chama zinazoendelea - mfano mzuri ni Makongoro Mahanga, mbunge wa segerea na naibu waziri wa kazi, na kaka yake Didas Massaburi (Mzee wa kufikiria kwa kutumia makalio) ambaye pia ni mayor wa Dar es salaam, ambao walishindwa kwenye nafasi ya NEC japokuwa walitumia pesa nyingi.
Pia kuanguka kwa wafuasi wa kambi hiyo mkoani tabora - jambo linaloashiria kuanguka kwa ngome ya Rostam Azizi (mshirika mkubwa wa Lowassa) na kupotea kwa umuhimu wa Hussein Bashe aliyeonekana kutaka kurithi nafasi ya king maker Rostam. Mkoani Tabora hakuna wilaya hata moja iliyopata mwenyekiti wa chama mwenye mlengo wa kambi hiyo ya watu wenye pesa. Pia wajumbe wa Nec Nzega, Igunga (Peter Kafumu aliyemshinda mlinzi wa jimbo la Rostam Azizi na mwenye kiti wa halmashauri hiyo Mh Abubakari Shabani) hawapo katika kundi hilo. Je hii inamanisha Samwel Sita anajipanga ama ni matokeo tu?
Kuzorota huko kumetokana na mambo mengi yakiwemo wasiwasi uliotanda ndani ya kambi hiyo kuwa waziri mkuu huyo mstaafu ana matatizo makubwa ya kiafya na hivyo kufifiza matumaini ya kuwa mgombea muafaka wa kambi hiyo. Hili linazidi kuwa kikwazo kwa kambi hiyo kwa kuwa Lowassa hapendi kuona mtu mwingine yeyote katika kambi hiyo anatamani kuwa rais zaidi ya yeye tu.
Habari za ndani ya kambi hiyo zinasema kuwa Lowassa alikorofishana na Emmanuel Nchimbi pale tu aliposema wawe na plan 'B' endapo itatokea kuwa yeye Lowassa ameshindwa kugombea Urais, na plan 'B' hiyo iwe kijana mwenye nguvu na afya bora kama Nchimbi! Toka aseme maneno hayo wakubwa hawa hawapatani tena kama zamani na kuna ushahidi kwamba Nchimbi haitwi tena kwenye vikao mbalimbali vya kambi hiyo.
Wasiwasi huo umeonekana ukisababisha uaminifu kwa kambi hiyo upungue nguvu sana na watu waanze kutazama fursa zilizopo kwenye makambi mengine yanayoibuka kila siku na kujikuta yakiwa na nguvu kubwa. wengi wanahisi anguko la Lowassa 2015 lisije kuwa anguko lao pia, wanaanza sasa kuchukua chao mapema.
Pamoja na sababu hiyo, nyingine kubwa inayotajwa kuisambaratisha kambi hiyo ni maamuzi magumu na yaliyoonekana kutoiunga mkono kambi hiyo yaliyofanywa na vikao mbalimbali vya maamuzi katika chama mfano maamuzi ya kuyafyeka majina ya watu walioonekana vinara wa siasa za kundi hilo kama akina Hussein Bashe, ambaye anaonekana kuwa ni nguzo muhimu ndani ya kambi hiyo yenye ufuasi kwa Lowassa, pia kuna vijana wengine ndani ya UVCCM waliokatwa majina yao bila sababu za msingi kujulikana - hapa mfano mzuri ni Naibu katibu mkuu wa UVCCM Zanzibar Jamal Kassim, aliyekuwa akigombea Uenyekiti wa Taifa wa UVCCM na aliyekuwa anapewa nafasi kubwa ya kushinda kama jina lake lingeteuliwa na NEC ya CCM, pia Sango Kasela ambaye aligombea nafasi ya Makamu Mwenyekiti UVCCM
Sababu kubwa ya tatu ya kuanguka kwa kambi hii ni kushindwa kwa makada wa chama hicho kwenye chaguzi za ndani ya chama zinazoendelea - mfano mzuri ni Makongoro Mahanga, mbunge wa segerea na naibu waziri wa kazi, na kaka yake Didas Massaburi (Mzee wa kufikiria kwa kutumia makalio) ambaye pia ni mayor wa Dar es salaam, ambao walishindwa kwenye nafasi ya NEC japokuwa walitumia pesa nyingi.
Pia kuanguka kwa wafuasi wa kambi hiyo mkoani tabora - jambo linaloashiria kuanguka kwa ngome ya Rostam Azizi (mshirika mkubwa wa Lowassa) na kupotea kwa umuhimu wa Hussein Bashe aliyeonekana kutaka kurithi nafasi ya king maker Rostam. Mkoani Tabora hakuna wilaya hata moja iliyopata mwenyekiti wa chama mwenye mlengo wa kambi hiyo ya watu wenye pesa. Pia wajumbe wa Nec Nzega, Igunga (Peter Kafumu aliyemshinda mlinzi wa jimbo la Rostam Azizi na mwenye kiti wa halmashauri hiyo Mh Abubakari Shabani) hawapo katika kundi hilo. Je hii inamanisha Samwel Sita anajipanga ama ni matokeo tu?