Elections 2010 Kamati za kitaifa na kimajimbo kufuatilia ahadi

Mbunge

Senior Member
Aug 7, 2008
104
10
ILI kuhakikisha kwamba wanaotoa ahadi katika kampeni zinazoendelea hivi sasa wanazitekeleza, tena wanazitekeleza kwa wakati ninapendekeza kuundwa kwa kamati kuu ya kufuatilia ahadi za kitaifa na zile za kimkoa na kiwilaya kwa upande mmoja na kwa upande mwingine kamati za kimajimbo za kufuatilia ahadi kwa kila jimbo na kila kata.

Haifai kusema tu hatudanganyiki. Muhimu zaidi ni kuhakikisha kuwa wanaogombea udiwani, ubunge na urais wanapopiga kampeni zao wanatoa ahadi zinazowezekana lakini sio kuropoka tu majukwaani ili mradi washinde.

Lazima ijulikane kwa siku zake 100 za kwanza kiongozi anayechaguliwa atafanya nini na kisha kila robo mwaka, nusu mwaka na kila baada ya mwaka lazima pawe na tathmini inayoonesha ubora au udhaifu wake.

Iwepo sheria katika katiba mpya ya kumaliza muda wa ubunge wa mtu katikati ya njia bila kungoja miaka mitano.

Kamati hizi za ufuatiliaji hapa Tanzania zitachangia sio haba katika kuharakisha juhudi zetu za maendeleo na kuufukuza umasikini kwa kasi kubwa kuliko ilivyo hivi sasa.
 
Lakini Kazi na majukumu ya mbunge, Diwani ni nini.?
Wasi wasi wangu hawa jamaa wao na sisi hatuju scope hasa nini wanatakiwa kufanya. Wakati wa kampeni wanatoa ahadi ambazo ziko nje ya majukumu na uwezo wao. Muda wao ukiishisha wanasema walikwamisha na bajeti finyu ya serikali.

Nimewai kuandika thread kuuliza majukumu na ya mbunge yana tofauti gani kitendaji na majukumu ya mkuu wa wilaya. Au majukumu ya Mbunge yanatofauti gani na majukumu ya diwani au Meya?

  • Mfano kama kazi ya bunge na mbunge ni kutunga sheria kwa nini asishtakiwe kudangaywa watu ataleta barabara,kujenga shule?
  • Ni kero gani anatakiwa azishughulike diwani na zipi zinatakiwa ziende kwa mbunge. Je hakuna muingiliano? Je hatuwalipi watu mishahara mingi kwa kazi ile ile kwa majina tofauti?

Lakini naunga mkono hoja Viongozi ianzishwe thread yenye mpangilio mzuri itakayokuwa na kumbukumbu ya ahadi za viongozi Watarajiwa .
 
Kuunda kamati za ufuatiliaji ni kupeana mlo mwingine...
Kinachotakiwa kufanyika ni kutunga sheia ya kuwadanganya au kuwarubuni (Misrepresentation) wananchi wakati wa kampeni kwamba chagua mimi nitafanya A, B C, wakati wanajua kwamba uwezo wa kufanya hivyo haupo... sheria hiyo kama ikiwekwa itazua wapiga kampeni kufikiria mara mbili kabla ya kutoa ahadi... Pia mtu mwenye madaraka ya kuleta au kufungua kesi asiwe ni AG bali kuwekwe office ya private prosecutors kwa gharama za serikali.. hii itasaida ma-private prosecutors kuchangamkia tenda kwa kuwafikisha mahakamanin wale wote waliowarubini watu wakati wa kampeni... Mahakama pia ifanywe chombo huru kwa maana ya kwamba majaji wa mahakama zote wasichaguliwe na Raisi Bali awapendekeze tu na wapitshwe na Bunge kwa usaili maalum
 
Back
Top Bottom