Kamati ya Zitto yatabiri kifo cha TBC

Mtoboasiri

JF-Expert Member
Aug 6, 2009
5,101
1,946
Kamati ya Zitto yatabiri kifo cha TBC
NA RICHARD MAKORE
24th May 2011



Kamati ya kudumu ya Bunge ya Hesabu za Mashirika ya Umma (POAC), imesema Shirika la Utangazaji la Taifa (TBC) liko hatarini kufirisika na kufa kama ilivyotokea kwa mashirika mengi ya umma hapa nchini kwa kuwa kumebainika kuwepo kwa matumizi mabaya ya fedha pamoja na kushindwa kukusanya madeni yanayofikia Sh. bilioni 4.8.
Kadhalika, kamati hiyo imeshangazwa na TBC kuingia mkataba wa kufanya biashara na kampuni ya Star Media bila kuijulisha Wizara ya Habari, Vijana , Utamaduni na Michezo ambayo shirika hilo lipo chini yake.
Mjumbe wa kamati hiyo ambaye ni mbunge wa Jimbo la Mwibara mkoani Mara (CCM), Alphaxard Lugola alisema matumizi mabaya ya fedha kunatishia kuliua shirika hilo la umma.
Alisema TBC lilipoanza wakati huo likiitwa TVT lilikuwa likienda vizuri lakini bahati mbaya hivi sasa linaelekea kufirisika na hatimaye kufa kabisa.
“Kwa mwenendo huu wa mahesabu TBC halina muda mrefu kuendelea kuwepo kwa kuwa mmeshindwa kudhibiti matumizi yenu pamoja na kuwa wakali katika kukusanya madeni yenu” alisema.
Aliongeza kuwa baada ya kusoma vitabu vya mahesabu ambavyo vilikabidhiwa kwa kamati alibaini kwamba Shilingi bilioni nane zilitumika kununua mafuta ya magari bila kufuata taratibu za manunuzi.
Alikiri kuwa hakuna uhalali wotote wa matumizi ya fedha hizo kwa ajili ya kujaza mafuta ya magari katika kituo cha mafuta cha Victoria cha jijini Dar es Salaam.
Alisema makubalinao ya mkataba wa kujaza mafuta hayo yalifanywa kwa mdomo badala ya maandishi kama sheria na taratibu za manunuzi ya serikali zinavyosema.
Kuhusu mkataba kati ya TBC Star Media, wajumbe hao walisema ulisainiwa kirafiki bila hata wizara inyosimamia shirika hilo kujulishwa.
Baadhi ya wajumbe wa kamati hiyo walihoji kwa nini TBC inazidi kuporomoka badala ya kupanda kama ilivyoanza huko nyuma.
Makamu mwenyekiti wa kamati hiyo ambaye pia ni Mbunge wa jimbo la Ludewa, Deo Filikunjombe, aliiambia kamati hiyo kuwa siku za TBC kuendelea kuwepo zinahesabika.
Alisema TBC inakabiliwa na uhaba wa fedha za kuiendesha hatua ambayo imeanza kusababisha matatizo ikiwemo Televisheni yake kushindwa kufika baadhi ya mikoa hapa nchini.
Kwa upande wake, uongozi wa TBC ulikiri kuwa matangazo yao hivi sasa hayawafikii wananchi wengi kutokana na mitambo yake kuchakaa na kwamba hakuna fedha za kuweza kununua mipya.
Mkurugenzi Mkuu wa TBC, Clement Mshana alijaribu kutoa majibu kwa kamati hiyo lakini mara kadhaa wajumbe wake walimkatisha baada ya kuhisi kama yalikuwa hayajitoshelezi.
Kuhusu ukusanyaji wa madeni ya TBC kutoka taasisi za umma, Mshana alisema wameajiri kampuni ya udalali ya Majembe kwa ajili ya kufanya kazi hiyo.
CHANZO: NIPASHE
 
Aliongeza kuwa baada ya kusoma vitabu vya mahesabu ambavyo vilikabidhiwa kwa kamati alibaini kwamba Shilingi bilioni nane zilitumika kununua mafuta ya magari bila kufuata taratibu za manunuzi. Alikiri kuwa hakuna uhalali wotote wa matumizi ya fedha hizo kwa ajili ya kujaza mafuta ya magari katika kituo cha mafuta cha Victoria cha jijini Dar es Salaam.

Yaani huu ni wizi mchana kweupeeeeee yaani Tshs 8,000,000,000 kwa ajili ya mafuta? Unajua ukichukua hiyo no. ukagawa kwa siku 365 (mwaka) in maana TBC inatumia shilingi 21,918,000 kila siku kununulia mafuta, karibu milioni ishirini na mbili tena kwenye kituo kimoja. This can never be true na kama ni kweli is typical madness!!!!!!
 
Sasa Tido alikuwa anafanya nini hapo Tbc,yaani hii ni hatari kwa taifa,media ya taifa kufilisika?ndio tunarudi nyuma tena kutegemea vyombo vya habr binafsi..
 
Hakuna cha Tido Mhando bali ni wizi maana hawana magari ya kuweza hata kujazwa mafuta ya TZS 5m kwa siku na mishahara ya staff siyo mikubwa. Tupate maelezo ya kina hizo TZS 8 blillion zimetowekaje? Kama hizo fedha zilipelekwa kwenye kampeni za CCM uchaguzi mkuu October 2010 tuelezwe kinagaubaga.
 
wanao filisi ni hao hao viongozi wanapoitwa kwa ajili ya kufanya mahojiano yoyote pale wanataka wapewe mafuta ya magari yao na allowance. Pale kila mtu alikuwa anataka kula ndio shida...

Waswahili wanasemaaa "Mwenda tezi na omo hurejengea ngamani" tutarejea ngamani ITV na STAR TV

Uganda M7 kawatimua wakurugenzi na bod of directors wote wa tv ya taifa UBC kwa ajili ya mambo kama hayo, kisa walinunua gari second hand afu kwa mabilion ya pesa na sasa alifanyi kazi istoshe hawampi mzee coverage ya kutosha, eti wanampendelea Besigye
 
kama CCM inakufa acheni na TBC ife maana haina manufaa yoyote kwa wananchi.
 
kufaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaa
mumemtoa Tildo kwa dhuluma ni bora kufaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaa tu
 

Yaani huu ni wizi mchana kweupeeeeee yaani Tshs 8,000,000,000 kwa ajili ya mafuta? Unajua ukichukua hiyo no. ukagawa kwa siku 365 (mwaka) in maana TBC inatumia shilingi 21,918,000 kila siku kununulia mafuta, karibu milioni ishirini na mbili tena kwenye kituo kimoja. This can never be true na kama ni kweli is typical madness!!!!!!

Hii habari inanipa maswali:
1. TBC wana magari mengi na majenereta makubwa kiasi cha kutumia mil 22 kila siku?
2. Kama jibu la (1) ni hapana, je kuna uuzaji wa mafuta unaofanywa na TBC wakishayachukua toka Victoria?
3. Kama jibu la (2) ni hapana, je Victoria service station inatumika kufisadi pesa za umma??
4. Kama jibu la (3) ni ndiyo, implication zake ni zipi kwa mmilki wa Victoria (Bw. Harrod) kujitambulisha kuwa ni mtumishi wa Mungu na Kufungua kanisa pale??

Mzee Harrod anatakiwa ajitokeze kusema kama kweli alilipwa hayo mabillioni au ni ujanja wa kimahesabu umefanywa ndani ya TBC.

Miaka ya nyuma nimewahi kuwa naweka mafuta pale kwa bill, nilikuwa nalipa kwa mwenzi na tuliandikishana. Iweje taasisi kubwa kama TBC wapeane biashara ya billion 8 kwa makubaliano ya mdomo tu.
Hii ni kusema kwamba TBC kujipendekeza kwa watawala ni kwa masilahi yao zaidi kuliko yale ya watawala maana wakiwa critical kwa watawala ya kwao yatafumuliwa.

Kwa uchafu huu bado ule wimbo wa "Tanzania Tanzania nakupenda kwa moyo wote" una mantiki au tuupeleke makumbusho ya taifa???
 
NI BORA IFE TU kwanza hamna cha maana nimekiona tbc zaidi ya kukopi tu!Niko kwenye maombi ya kuiua TBC ,HAMNA KITU PALE NI UJINGA MTUPU!
 
kufaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaa
mumemtoa Tildo kwa dhuluma ni bora kufaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaa tu
mambo yote hayo yamefanyika wakati wa utawala wa tido mhando.
 
Naomba nipewe maiti ya TBC kuizika nina kaburi kubwa itaingia huku shy town la futi 32 urefu na upana futi 16 ulale mahali pema TBC
 
Kikwete anajisikiaje mashirika muhimu kama ATCL,TRL na TBC yote yanateketea wakati wa utawala wake? Tuombe Mungu muungano usife mikononi mwake; itakuwa noma!!
 
Back
Top Bottom