Halisi
JF-Expert Member
- Jan 16, 2007
- 2,802
- 613
Kamati Maalumu ya NEC ya CCM imeanza kikao chake muda mchache uliopita hapa Zanzibar, Kisiwandui. Kikao hicho kitachagua wana CCM watano kwenda Kamati Kuu na baadaye NEC.
Majina yanayotajwa kupita ni pamoja na Dk. Ali Mohamed Shein, Dk. Mohamed Bilal, Haroun Suleiman, Alli Juma Shamhuna na Shamsi Vuai Nahodha. Mwingine anayepewa nafasi ni Mohamed Aboud, ambaye hata hivyo kuna utata katika elimu yake.
Uwezekano mkubwa ni kuwa kuna kila dalili za Dk. Shein kubaki kuwa mgombea urais wa Zanzibar kutokana na kuwa na nguvu kubwa ndani ya serikali na CCM. Tatizo kuna hofu kubwa hapa Zanzibar ya JK kutotabirika, maana "anaweza kubadilika"
Majina yanayotajwa kupita ni pamoja na Dk. Ali Mohamed Shein, Dk. Mohamed Bilal, Haroun Suleiman, Alli Juma Shamhuna na Shamsi Vuai Nahodha. Mwingine anayepewa nafasi ni Mohamed Aboud, ambaye hata hivyo kuna utata katika elimu yake.
Uwezekano mkubwa ni kuwa kuna kila dalili za Dk. Shein kubaki kuwa mgombea urais wa Zanzibar kutokana na kuwa na nguvu kubwa ndani ya serikali na CCM. Tatizo kuna hofu kubwa hapa Zanzibar ya JK kutotabirika, maana "anaweza kubadilika"