Kamati Kuu ya CHADEMA yakutana Igunga

ombi langu kwa chadema ni kila kituo msimamizi msije mkatuambia kituo X hakikuwa na msimamizi na ningependa muwape semina ya kutosha sina wasiwasi kwa hilo yuko kama G. Lema..
 
Kwanini CUF wasiungane na CCM kumsimamisha mgombea wao mmoja? au wewe hujui kuwa CUF na CCM lao ni moja?
Mkuu,
wala usihangaishe kichwa, huyu mwenzetu sometimes ni very controversial.

Umesababisha nikumbuke utata wa misimamo yake tangu alipokuwa akituelezea habari za mgomo wao UD siku za nyuma.

Maelezo yake mengi yalikuwa ndivyo sivyo!! huyu ndugu ni lukewarm
Muhimu kwa wapambanaji ni kusonga mbele tuu.
 
Asante kwa taarifa Regia, tunategemea hekima,umakini na utashi mkubwa katika mchakato wa kumpata mwakilishi. Ikumbukwe kua uchaguzi huu ni kipimo cha mabadiliko na ukuaji wa nguvu ya chama baada ya uchaguzi wa mwaka jana na kasi ya kuelekea uchaguzi mkuu 2015.
Kamati kuu ya chama cha chadema kuweni makini na mamluki wa chama tawala,Kumbuka ktk msafara wa mamba na kenge wapo.
 
Kamati Kuu ya CHADEMA inatajiwa kufanya kikao chake kesho katika jimbo la Igunga.Kikao hicho ni maalum kwaajili ya kupitisha jina la mgombea Ubunge katika uchaguzi mdogo unaotarajiwa kuanza tarehe 7 Sept 2011. Vile vile kikao hicho kinatrajiwa kupitisha mkakati na bajeti ya uchaguzi huo katika kuhakikisha kuwa jimbo hili linachukuliwa na CHADEMA.Dalili zote za awali zinaonesha kuwa jimbo hili kuchukuliwa na CHADEMA.Kutoka njiani Manyoni tukiwa tunaelekea Igunga.Nawasilisha.

Hongera dada Regia,nawaombea mfike salama,Igunga yetu, lakini huyu Shibuda tunamfanyaje jamani?

Naomba wembe ulitumika kuwanyoa madiwani utumike upande wa pili ukiwa na makali zaidi ya madiwani kumng'oa huyu kibaraka wa CCM, CHADEMA FOR CHANGE.
 
Asante Regia kwa taarifa. Nje ya mada hii sisi wananchi tumesononeshwa sana na kuumia mno na kauli ya mbunge mwenzenu Mh Shibuda. Yaani nilitamani kupiga simu yangu kwenye screen wakati huyu mbunge akichangia mambo ambayo yanaonekana wazi wazi kuwa si mwenzetu kabisa. si mimi tu ila wananchi wengi wapenda haki na usawa wameumia sana.<br />
<br />
Nakuomba Regia fikisha suala hili mbele ya kamati kuu, sisi tunapendekeza mtu huyu apumzishwe maana si mwenzetu. ni vyema tukatibu ndonda leo badala ya kulifuga cause linaweza lisitibike tena badala yake kama lipo mguuni basi lazima ukatwe kuokoa maisha. sisi hatutaki tufike huko. <br />
<br />
Fikisha ujumbe wa hao wapiganaji-- tunawaombea mafanikio. najua wananchi wakakuwa barabarani kila mnapita cause mmebeba sura ya Tanzania mpya - Tanzania yenye Tumaini Jipya. Mungu awababariki sana tupo pamoja nanyi kwenye sara na dua zetu. Peoples Poweeeer.
<br />
<br />
Naunga mkono maelezo yako 100%,na ikumbukwe kua huyu bwana Shibuda ni rahisi sana hata kutoa siri za Chama huko tuendako eg.chukulia karibu tunaelekea uchaguzi na akajaribu kuvujisha SIRI za Chama hamuoni kua atakua ametuharibia sana? mtu gani huyu hataki kuendana na Philosophy ya Chama?

Jana nimekeleka sana na ameniumiza sana na huko Igunga kuweni makini na watu wanaofanana na huyu kiruka njia,nina hasira sana na maisha haya tunayoishi.
 
Msisahau kuwa kikubwa ni kulinda kura kama Nyamagana, Ilemela, Mbea Mjini na Arusha. maana magamba wameshagombana wao kwa wao kuwa ama kwa dola au kwa pesa lazima jimbo lirudi CCM, hawataki kusikia lugha za kina Bashe kuwa "nataka tushindwe Igunga tuheshimiane"



Na nyinyi msiifanye CHADEMA kama si chama kisichostahili kupitia misukosuko. Kuna kazi nzito Igunga mnaleta habari ya Shibuda. Mnadhani akiondoka Shibuda watakosekana wa aina hiyo. Kwa ninavyowajua CHADEMA suala la Shibuda sidhani linawaumiza kama chama. Wao wachukue hansard kisha wamuite kwenye chama apate nafasi ya kufafanua lengo la anayoeleza bungeni na magazetini. Kesi ya Shibuda ni rahisi sana kwa sababu ina ushahidi mzuri wa maneno yake moja kwa moja. Muhimu ni kujua nia yake ni nini hasa na ikibidi afanye hivo kimaandishi.

Hapo kwenye red. Kwa mujibu wa Katiba, Mbunge ana kinga ya ajabu sana kwa lolote atakaloongea AKIWA KWENYE VIKAO RASMI NDANI YA UKUMBI WA BUNGE.

Hakuna mamlaka yoyote, hata Mahakama ya Rufaa, yenye uwezo wa kumhoji Mbunge kwa kauli zake "ndani ya Bunge". Labda kwa kujua hilo, ndio maana Shibuda anafanya mizaha anayoifanya.
 
Hapo kwenye red. Kwa mujibu wa Katiba, Mbunge ana kinga ya ajabu sana kwa lolote atakaloongea AKIWA KWENYE VIKAO RASMI NDANI YA UKUMBI WA BUNGE. Hakuna mamlaka yoyote, hata Mahakama ya Rufaa, yenye uwezo wa kumhoji Mbunge kwa kauli zake "ndani ya Bunge". Labda kwa kujua hilo, ndio maana Shibuda anafanya mizaha anayoifanya.
Kwa hiyo hata ukimtukana rais matusi ya nguoni bungeni hansad inakulinda........labda mimi sielewi.
 
Kwa hiyo hata ukimtukana rais matusi ya nguoni bungeni hansad inakulinda........labda mimi sielewi.

Kuna taratibu zake na hatua zinachukuliwa humo humo ndani ya Bunge na si nje ya hapo. Ndio maana Spika/Mwenyekiti wakati wote hachezi mbali na kauli za wabunge wanapochangia kuhakikisha hakuna ukiukwaji wa Kanuni za Bunge ikiwamo hilo la kutukana.

Ndio maana utasikia "futa kauli", "lete ushahidi", n.k.
 
Ahsante kwa taarifa mpiganaji wetu.zingatieni kua magamba ni wazuri sn katika rafu na rushwa katika uchaguzi na ni vema mkumbuke kua cuf hawaipendi cdm na wapo tayari kuwasaport ilimradi cdm ikose ushindi.

Hivyo nashauri makamanda muwe makini na mumtumie sn huyo diwani wetu wa hapo igunga.
 
Asante kwa taarifa tunaiamini kamati kuu itamteua m2 makini atakae toa ushindi wa kishindo. Naamini kuanzia kesho Igunga itafunikwa na VAZI LA TAIFA (magwanda)
 
quote_icon.png
By Speaker
Kwa mujibu wa habari za uhakika ni kwamba chadema itashika nafasi ya
tatu katika uchaguzi huo,....na kama chadema isipo simamisha mgombea
basi cuf itashinda lakini kwa kua vyama vya upinzani vinaenda kugawana
nusu
ya nyama huko igunga,basi mzee kafumu ataingia mjengoni kwa mbwembwe sana.
Nyie mnaolazimisha CDM iungane na CUF kwanini CUF wasiungane na CCM halafu mtuambie ni wapi wapinzani waliungana wakashinda,
kama ni kugawana kura hata CCM itagawana na CUF maana CDM wanaenda bila kuwa na kura hata moja, ngoja niwape mahesabu yatavyokuwa,

Uchaguzi uliopita CCM walipa kura 35,000 safari hii watapata nusu ya hizo nusu iliyobaki itakwenda Chadema yaani 17,500.
CUF walipata kura 11,000 safari hii hata nusu yake hawapati basi tuwape nusu 5,500 na nusu iliyobaki itakwenda Chadema yaani 5,500.
Final results
Chadema kura 17,500 + 5,500 = 23,000.
CCM kura 35,000/2 = 17,500.
CUF kura 11,000/2 = 5,500.
 
Wait a minute..... kwa hiyo lile jina la mwalimu tulopewa limetoka wapi ikiwa hii kama ti haijafika hata Igunga ndio kwanza wako safarini kuelekea huko?..Huyo mwana JF aliyetuletea habari za kura za maoni anaweza kutueleza ni kina nani walioendesha kura hizo maanake isijekuwa tumelishwa myamafu ili watuchekke baadeye kamati itakapochagua jina jingine.. Mchezo huu umefanyika sana ili kuleta vurugu ndani ya vyama hasa nikifuatia chaguzi zilizopita wa vijana CCM na CDM.
Nadhani swali lako limejibiwa vizuri na Mwita Maranya.....
 
Mheshimiwa Regia nakubali CDM mko serious lakini jambo dogo tu huwa tunamalizwa na CCM, mimi ni mzaliwa wa igunga na nimeishi igunga muda mrefu sana kwahiyo nafuatilia kwa karibu mchakato wa igunga tangu kujiuzulu kwa rostam, nawajua wafuasi wa CCM na CDM. weakness ya CDM Igunga hakuna uongozi imara wa CDM, nasema hivyo kwasababu mwenyekiti wa wilaya Majimoto, Kashindye na Pili mnene (amekuwa mwenyekiti wa wanawake wa chadema wilaya tangu kujiuzulu kwa rostam kabla ya hapo alikuwa ccm) walikuwa wakala wa rostam uchaguzi wa 2010.

Majimoto alijitoa kugombea ubunge kwa kupewa fungu na rostam, Kashindye alteuliwa kuhamasisha kura za uraisi kwa jakaya kwa kauli mbiu aliyokuwa anawambia wanaigunga vijijini kuwa DR. SLAA ni fisadi wa mapenzi ili wanawake wasimpigie kura. Pili Mnene amejengewa nyumba na rostam na mpaka sasa anasomesha mtoto wake chuo kikuu. Mheshimiwa diwani wetu wa chadema kwenye vikao vya council anapokea posho anayotoa RA ili kuweza vikao vya madiwani vipitishe matakwa yake kwa remote wakati yeye anakula raha jijini.

Sasa kabla ya kupitisha mgombea wenu kesho mheshimiwa kashindye muhakikishe mmesafisha jambo hilo kwani walimu wote wanajuwa kuwa alikuwa kibaraka wa rostam kufanya kampeni za ccm 2010 sasa wapiga kura wenu watakuwa na imani nae vipi kwasababu wanamtambua kama CCM na kwataarifa nilizo nazo hadi sasa wamekorofishana na DC igunga kwa kuwa wanajuwa kilichofanyika mwaka jana. Na siku chache baada ya kujiuzulu RA, Bashe alivyokuja igunga alimtumia Kashindye kuwapelekea wenyeviti wa kata salamu kutoka kwa rostam na kuwajulisha kuwa yupo nao pamoja fungu alilopewa alimficha boss wake DC na badala yake akatumia gari la ukaguzi na mafuta ya serikali bila kumgawia boss wake fungu.

TUPO NJIA PANDA wanaigunga kwa maana kwamba tutapata bora mbunge kwa maslahi yake mbunge na kuongeza fungu la posho kwenye chama au tunapata mbunge ili kuweza kuwatumikia wanaigunga? NITOE NJIA PANDA KESHO
 
Kwa mujibu wa habari za uhakika ni kwamba chadema itashika nafasi ya
tatu katika uchaguzi huo,....na kama chadema isipo simamisha mgombea
basi cuf itashinda lakini kwa kua vyama vya upinzani vinaenda kugawana
nusu ya nyama huko igunga,basi mzee kafumu ataingia mjengoni kwa mbwembwe sana.

chadema wanayo nafasi ya kushinda ila wako mtegoni mpaka sasa, CUF msijisumbue sana bora muwaunge mkono ccm kwani Dr. Kafumu ameyavulia nguo maji na hana budi kuyaoga mpaka ameacha budget ya wizara yake haijapita yupo kwenye mchakato. DANGER, mzimu wa rostam unasumbua igunga bado.
 
Mheshimiwa Regia nakubali CDM mko serious lakini jambo dogo tu huwa tunamalizwa na CCM, mimi ni mzaliwa wa igunga na nimeishi igunga muda mrefu sana kwahiyo nafuatilia kwa karibu mchakato wa igunga tangu kujiuzulu kwa rostam, nawajua wafuasi wa CCM na CDM. weakness ya CDM Igunga hakuna uongozi imara wa CDM, nasema hivyo kwasababu mwenyekiti wa wilaya Majimoto, Kashindye na Pili mnene (amekuwa mwenyekiti wa wanawake wa chadema wilaya tangu kujiuzulu kwa rostam kabla ya hapo alikuwa ccm) walikuwa wakala wa rostam uchaguzi wa 2010.

Majimoto alijitoa kugombea ubunge kwa kupewa fungu na rostam, Kashindye alteuliwa kuhamasisha kura za uraisi kwa jakaya kwa kauli mbiu aliyokuwa anawambia wanaigunga vijijini kuwa DR. SLAA ni fisadi wa mapenzi ili wanawake wasimpigie kura. Pili Mnene amejengewa nyumba na rostam na mpaka sasa anasomesha mtoto wake chuo kikuu. Mheshimiwa diwani wetu wa chadema kwenye vikao vya council anapokea posho anayotoa RA ili kuweza vikao vya madiwani vipitishe matakwa yake kwa remote wakati yeye anakula raha jijini.

Sasa kabla ya kupitisha mgombea wenu kesho mheshimiwa kashindye muhakikishe mmesafisha jambo hilo kwani walimu wote wanajuwa kuwa alikuwa kibaraka wa rostam kufanya kampeni za ccm 2010 sasa wapiga kura wenu watakuwa na imani nae vipi kwasababu wanamtambua kama CCM na kwataarifa nilizo nazo hadi sasa wamekorofishana na DC igunga kwa kuwa wanajuwa kilichofanyika mwaka jana. Na siku chache baada ya kujiuzulu RA, Bashe alivyokuja igunga alimtumia Kashindye kuwapelekea wenyeviti wa kata salamu kutoka kwa rostam na kuwajulisha kuwa yupo nao pamoja fungu alilopewa alimficha boss wake DC na badala yake akatumia gari la ukaguzi na mafuta ya serikali bila kumgawia boss wake fungu.

TUPO NJIA PANDA wanaigunga kwa maana kwamba tutapata bora mbunge kwa maslahi yake mbunge na kuongeza fungu la posho kwenye chama au tunapata mbunge ili kuweza kuwatumikia wanaigunga? NITOE NJIA PANDA KESHO
Unaongea sana kama kasuku kila kitu wewe unakijua ah waache wana Igunga wachague wanayemtaka kwani tatizo lako nini mbona unaumia sana kuna nini, kwani kuhama chama ni dhambi kwa taarifa yako karibu asilimia 80 ya wapinzani walikuwa CCM hata hao unaowaona viongozi wa CDM walikuwa huko huko.
 
Kamati Kuu ya CHADEMA inatajiwa kufanya kikao chake kesho katika jimbo la Igunga.Kikao hicho ni maalum kwaajili ya kupitisha jina la mgombea Ubunge katika uchaguzi mdogo unaotarajiwa kuanza tarehe 7 Sept 2011.

Vile vile kikao hicho kinatrajiwa kupitisha mkakati na bajeti ya uchaguzi huo katika kuhakikisha kuwa jimbo hili linachukuliwa na CHADEMA.Dalili zote za awali zinaonesha kuwa jimbo hili kuchukuliwa na CHADEMA.Kutoka njiani Manyoni tukiwa tunaelekea Igunga.Nawasilisha.

Dada yangu Mh. Regia Mtema naandika huku nikibubujikwa na machozi ya furaha hasa baada ya kuniakikishia ushindi huko Igunga, sidhani kama kuna Mwanaigunga anayewaza kuwachagua CCCM, matatizo yaliyopo katika nchi hii hayawezi kutatuliwa na CCM tena na hilo Igunga wanalijua fika hivyo tunategemea kumsimamisha mtu ambaye atawatendea haki wanaigunga maana ni lazima tu CDM inashinda hiyo haina ubishi.

Hongera sana Mh. Regia kazi yako inaonekana, wakabeni koo hao Magamba.
 
Naskia NAPE yupo nyumbani kwa Mkurugenzi wa usimamizi wa uchaguzi ambaye pia ni Mkurugenzi wa Halmashauri ya Wilaya Igunga.

Lengo ni kupanga mkakati wa kuiba kura na kumtangaza mgombea wa CCM kwamba ndiye atakuwa mshindi siku ya kutangaza matokeo.
 
Tumbili, ccm hadi sasa wanajenga mazingira ya kuiba kura maana wanaamisha watendaji wanaoonekana kutopokea maelelekezo yao au wasio tayari kuwa remoted kutoka juu, amini nawaambia kuwa kuna uwezekano mkubwa saaaana wa kumwamisha mkurugenzi mtendaji wa wilaya ndugu Protas Magayane kabla ya uchaguzi huu mdogo.

Juzi kamati ya ulinzi na usalama ya mkoa ilikutana kuweka mikakati ya ccm kubaki na jimbo na amri kutoka kwa Jk ni kuwa hata kwa kupindua matokeo halali wafanye kwa gharama yoyote ilimladi jimbo libaki ccm!
 
Back
Top Bottom