Kamati Kuu ya CHADEMA Kukutana Kesho Kupitisha Wagombea BAVICHA

Uchaguzi unafanyikia wapi na saa ngapi na wakina nani wanatakiwa kupiga kura. Kama mpaka leo hawajatoa majina rasmi ya wagombea je, wanaotoka mbali watafika kwenye eneo la tukio saa ngapi?
 
Cdm ingependeza sana kama mngempa mwanadada ili muonekane kuwa mnajali
CHADEMA Hawagawi vyeo, Uliwashauri vizuri wakamgawia yule mama..........aaaagggrrrrr.....nimeikumbuka sura yake tu nikapata kichefuchefu
 
Wakuu Salaam.

Kamati Kuu ya dharura ya CHADEMA kukaa kesho kwa mujibu wa Katiba kwaajili ya kupitisha Wagombea nafasi mbalimbali katika Baraza la Vijana CHADEMA(BAVICHA).

Siku ya kesho ndio mtapata nafasi ya kujua idadi kamili ya Wagombea pamoja na majina yao.Uchaguzi unatarajiwa kufanyika Siku ya Jumamosi tarehe 28 Mei 2011 kama ilivyotangazwa hapo awali.

Kaeni Mkao wa Kula.

Kutoka Makao Makuu ya Chama

Regia E Mtema
Waziri Kivuli-Kazi na Ajira

Mh. Kamanda wangu, Mbunge wangu na Waziri wangu, nashukuru kwa taarifa na ni maombi yangu tuwapate viongozi safi wa BAVICHA watakao endana na kasi ya CHAMA na hivyo kuwa chachu ya mabadiliko nchini...Tuko pamoja mkuu...
 
Jana tulipata taarifa kuwa leo kamati kuu ya chadema inakaa kwa dhararula ili kujadili na kupitisha majina ya wagombea wa uongozi wa BAVICHA.
Kwa yeyote mwenye taarifa ya maendeleo ya kikao hicho tafadhali atujulishe.
 
Kamati kuu itoke na resolution moja,kwa kuwa mwenyekiti na katibu mkuu antokea kaskazini basi mwenyekiti wa vijana asitoke huko,jina la Saanane liondolewe.Muondoeni huyo Dikteta,jeuri
 
Napenda kutanguliza shukrani kwa kutupa taarifa lakina napenda nifikishe kutoridhishwa kwangu na namna hiyo kamati kuu inavyofanya kazi, kesho ni ijumaa ambapo itachuja baadhi ya majina na keshokutwa ndo uchaguzi, Hamjawatendea haki kabisa wale watakaoondolea kwa sababu haiingi akilini mtu anachujwa bado siku moja, Hili ni kosa kubwa na mnatakiwa next time mrirekebishe, mlitakiwa mfanye huo mchujo angalau wiki mbili kabla, Chadema ni chama makini ila ka hili mmekosa umakini na mmetusononesha baadhi ya wafuasi wenu.
 
Wakuu Salaam.

Kamati Kuu ya dharura ya CHADEMA kukaa kesho kwa mujibu wa Katiba kwaajili ya kupitisha Wagombea nafasi mbalimbali katika Baraza la Vijana CHADEMA(BAVICHA).

Siku ya kesho ndio mtapata nafasi ya kujua idadi kamili ya Wagombea pamoja na majina yao.Uchaguzi unatarajiwa kufanyika Siku ya Jumamosi tarehe 28 Mei 2011 kama ilivyotangazwa hapo awali.

Kaeni Mkao wa Kula.

Kutoka Makao Makuu ya Chama

Regia E Mtema
Waziri Kivuli-Kazi na Ajira

Mwendo ni ule ule, uchaguzi ukigubikwa na ufedhuli ambao CHADEMA
imejidhihirisha kwamba haiko tayari kuuvumilia, mpelekee habari hizi DR
kwamba kama kawaida asisite kuusitisha mara moja, aimuogope mtu yeyote
katika kufanikisha dhamira ya uchaguzi huru na wa haki.

Muwaambie na hao wagombea kwamba, wasitegemee kuitumikia hiyo nafasi,
kwa matakwa yao binafsi au ya kakikundi fulani, wajiandae kutumia matakwa
ya UMA, CHADEMA wote hapo mnafahamu vizuri UMA unataka nini, ushahidi
mnao kwamba wakati wote hata kwa maneno tu, mlipoonyesha kwamba
mko upande wa UMA, UMA uliwafuata na kuwakubali kwa miikio mikubwa sana,

Yeyote atakaye kwenda kinyume UMA utamkataa, sababu tayari mmekwishauaminisha
kwamba Mnakifanya kile wanachokitaka wao.

Nawatakia Mchakato mwema
 
Mchane na Grayson mmoja wapo ndo anatakiwa ashinde coz wataweza kutuongoza vijana, mchange hana mda wa majungu wala umbea ni mtu wa kazi mwanzo mwisho, Sio siri nitafurahi sana km atashinda.
 
Mbona mmeanza kampeni sasa?
Waachieni wenyewe wafanye kampeni wakati firimbi itakapo pulizwa ingawa wengine walishaanza kutroti kabla ya firimbi na wengine wamekwisha kuonekana ni opportunist nadhani itakuwa ni kazi ya wapiga kura kuwa makini wasije wakaifanya CDM kuwa CCM kwa kuchagua viongozi bomu maana hata CCM ya nyundo na jembe na wakati wa chaguzi za Ubunge kwa Nyumba na Jembe ili kuwa CCM kweli kweli!

Vijana na wapiga kura wote kuweni makini chama ni viongozi waliomakini na wasio tanguliza maslahi ya tumbo na familia zao mbele ya maslahi ya Umma na chama kwa ujumla.

Nawatakia kila la heri katika zoezi hili.
 
TAARIFA KWA UMMA KUHUSU ORODHA YA WAGOMBEA NA UTARATIBU WA UCHAGUZI WA BARAZA LA VIJANA WA CHADEMA (BAVICHA) NGAZI YA TAIFA


Taarifa inatolewa kwa umma kuhusu orodha ya wagombea waliorudisha fomu na utaratibu wa uchaguzi wa Baraza la Vijana wa CHADEMA (BAVICHA) ngazi ya taifa kama ifuatavyo:

ORODHA YA WALIORUDISHA FOMU ZA KUGOMBEA:

Nafasi ya Mwenyekiti (Wagombea 10)
Aidan Sadik P.,
Benard A. Mao,
Benard Saanane,
Deogratias Kisandu,
Edwin Soko,
Greyson Nyakarungu,
Habib Mchange,
John Heche,
Masood S. Suleiman
Mtela Mwampamba.

Nafasi ya Makamu Mwenyekiti (Bara) (Wagombea 5) :
Emanuel Somoin,
Gwakisa B. Mwakasendo,
Joseph Patric,
Juliana Shonza
Julieth V. Rushuli.

Nafasi ya Makamu Mwenyekiti (Zanzibar) (Wagombea 3)-
Sharim S. Khamis,
Zainab B. Bakari
Ally Akalipo Ally.

Nafasi za Ujumbe: Wawakilishi wa BAVICHA kwenye Mkutano Mkuu wa chama-nafasi 20 (Wagombea 39) na wawakilishi wa BAVICHA kwenye Baraza Kuu la chama-nafasi 5 (Wagombea 32).

Wagombea waliorudisha fomu kwa nafasi za Katibu Mkuu, Naibu Katibu Mkuu, Mratibu wa Uhamasishaji, Mweka Hazina watatangazwa katika ratiba ya baadaye.

MIKUTANO YA UCHAGUZI:

Mwenyekiti, Makamu Mwenyekiti na Wawakilishi wa BAVICHA kwenye baraza kuu na mkutano mkuu watachaguliwa na Mkutano Mkuu wa BAVICHA utakaofanyika tarehe 28 Mei 2011 kama ilivyotangazwa awali. Wagombea husika wanakumbushwa kufika kwenye mkutano mkuu kwa gharama zao.

Katibu Mkuu, Naibu Katibu Mkuu, Mratibu wa Uhamasishaji na Mwekahazina watapendekezwa na Kamati ya Utendaji ya BAVICHA kwa mujibu wa ratiba itayopangwa baadaye na uteuzi wao utathibitishwa na Kamati Kuu ya chama hivyo wataalikwa katika vikao vya baadaye.

UCHUJAJI NA USIMAMIZI WA UCHAGUZI:Kwa mujibu wa katiba ya chama uchaguzi husika kwa kuwa ni wa kitaifa mkutano wake utasimamiwa na wazee wastaafu wa chama wakati katibu mkuu ndiye msimamizi wa uchaguzi katika taratibu zote kuanzia hatua ya awali.Aidha ngazi ya uchujaji itakuwa ni Kamati Kuu ya chama ambayo itafanya uteuzi wa wagombea katika kikao chake cha tarehe 26 Mei 2011 kwa kuwa ndiyo yenye wajibu wa kuyasimamia mabaraza kwa mujibu wa katiba na kanuni.

TARATIBU ZA KAMPENI: Kampeni za uchaguzi zitafanywa kwa kuzingatia kanuni za chama, maadili ya uongozi/viongozi (rejea kanuni za chama vifungu vya 10.1, 10.2 na 10.3) pamoja na muongozo juu ya uendeshaji wa uchaguzi ndani ya chama uliopitishwa na Baraza Kuu la Chama tarehe 13 Disemba 2007 unafafanua mambo yanayopaswa kufanywa na yasiyopaswa kufanywa wakati wa kampeni na uchaguzi ndani ya chamakwa lengo la kujenga mshikamano na umoja ndani ya chama na kufanya uchaguzi uwe huru na wa haki.

Wagombea wote wanahimizwa kuzingatia taratibu za kampeni za uchaguzi ambazo nakala yake inapatikana pia kwenye mtandao wa chama www.chadema.or.tz kutokana na umuhimu wa uongozi wa vijana kwa mustakabali wa chama na taifa kwa ujumla.

Kauli mbiu ya BAVICHA-Vijana; Nguvu ya Mabadiliko


John Mnyika (Mb)
Mwenyekiti wa Kamati ya Taifa ya Vijana
0784222222

Asante kwa taarifa.
Ila hiyo red huwa haipokelewi
 
UCHAGUZI WA BAVICHA KIZUNGUMKUTI.

-UCHAGUZI WA BAVICHA NI KIZUNGUMKUTI....nasema ni kizungumkuti kwa sababu unawagawa vijana wa chadema katika mapande manne mpaka sasa na hii inatokana na VIONGOZI WA JUU kupigana vikumbo katika nafasi ya MWENYEKITI WA TAIFA KATIKA UCHAGUZI UNAOKUJA waliorudisha fomu wengi wao wanabebwa na MAFISADI WA CHAMA.

1. BERNAD SAANANE

2.JOHN HECHE

3.EDWIN SOKO

watajwa hapo juu ni wateule wa mwenyekiti wa chama FREEMAN HAIKAEL MBOWE ndiye anapanga taratibu za kuhakikisha miongoni mwa vijana hao mmoja anakuwa mwenyekiti wa BAVICHA ili iwe rahisi kwake kupambana na MAHASIMU wake mbele ya safari, ngoma nzito hiyo kazi ipo watachakachuana mpaka wataota mbigili, sijui itakuaje maana HECHE aliwapiga vita sana akina HALIMA MDEE, LUCY OWENYA, SUZAN LIYMO, ANNA KOMU ili kuwepo na uchaguzi wa huru na wahaki viti maalum ubunge 2010 inasemekana alizunguka nchi nzima kuwa maliza na alfanikiwa maana timbwili timbwili kila mtanzania alilisikia na kuliona mwaka jana, sasa je atasalimika na ho ni wajumbe wa kamati kuu ya chadema? tusubiri.........yetu sie mijicho..............na misikio....................

1.HABIB MCHANGE.

2.GREYSON NYAKARUNGU.

3.MASOOD S. SULEIMAN.

-WATAJWA hapo juu hawa ni madogo wa KABWE ZUBIRI ZITTO yeye alipigania miongoni mwa vijana hawa mmoja awe ndie mwenyekiti wa BAVICHA sijui watasuguana namna gani, suala la ukanda linaweza wasaidia itategemea watakavyojieleza katika mkutano wa uchaguzi wao hiyo 28 may 2011 siku ya jumamosi, najua wabunge wengi wapya wachadema wanamsaidia HECHE KUCHUKUA HIYO NAFASI maana alisaidia pia kutetea japo kisirisiri ila kwa fitina kubwa iliyomtingisha FREEMAN HAIKAEL MBOWE mpaka sasa hajui hatma yake ya baadae maana KABWE ZUBERI ZITTO KESHA SEMA 2015 atagombea urais ndani ya CHADEMA.

-HALIMA MDEE/LUCY OWENYA/JONH MNYIKA/ wameunda timu yao ya kuhakikisha GREYSON NYAKARUNGU jina halipiti ndani ya kamati kuu kwani alihongwa na FISADI NIMROD MKONO asigombee musoma vijijini na zengwe linaendelea kwa kasi kubwa maana kikao kilichokaliwa cha siri siku mbili zilizopita kimepanga siku ya kikao cha kesho kuamsha moto wa ukweli juu ya kijana huyo.

-BERNAD SAANANE ni kijana lakini inaonekana hakubaliki na vijana wengi wa CDM maana anaonekana ni mgeni na MBOWE ana siri kubwa na kijana huyo watamalizana wenyewe hawa CDM, CV YAKE IMEJAA UZUSHI mwingi ambao akipatikana kijana aliyesoma India anaweza kuweka wazi baadhi ya mambo aliyoyaeleza.

-chadema hamna jipya mshatokota.
 
UCHAGUZI WA BAVICHA KIZUNGUMKUTI.

-UCHAGUZI WA BAVICHA NI KIZUNGUMKUTI....nasema ni kizungumkuti kwa sababu unawagawa vijana wa chadema katika mapande manne mpaka sasa na hii inatokana na VIONGOZI WA JUU kupigana vikumbo katika nafasi ya MWENYEKITI WA TAIFA KATIKA UCHAGUZI UNAOKUJA waliorudisha fomu wengi wao wanabebwa na MAFISADI WA CHAMA.

1. BERNAD SAANANE

2.JOHN HECHE

3.EDWIN SOKO

watajwa hapo juu ni wateule wa mwenyekiti wa chama FREEMAN HAIKAEL MBOWE ndiye anapanga taratibu za kuhakikisha miongoni mwa vijana hao mmoja anakuwa mwenyekiti wa BAVICHA ili iwe rahisi kwake kupambana na MAHASIMU wake mbele ya safari, ngoma nzito hiyo kazi ipo watachakachuana mpaka wataota mbigili, sijui itakuaje maana HECHE aliwapiga vita sana akina HALIMA MDEE, LUCY OWENYA, SUZAN LIYMO, ANNA KOMU ili kuwepo na uchaguzi wa huru na wahaki viti maalum ubunge 2010 inasemekana alizunguka nchi nzima kuwa maliza na alfanikiwa maana timbwili timbwili kila mtanzania alilisikia na kuliona mwaka jana, sasa je atasalimika na ho ni wajumbe wa kamati kuu ya chadema? tusubiri.........yetu sie mijicho..............na misikio....................

1.HABIB MCHANGE.

2.GREYSON NYAKARUNGU.

3.MASOOD S. SULEIMAN.

-WATAJWA hapo juu hawa ni madogo wa KABWE ZUBIRI ZITTO yeye alipigania miongoni mwa vijana hawa mmoja awe ndie mwenyekiti wa BAVICHA sijui watasuguana namna gani, suala la ukanda linaweza wasaidia itategemea watakavyojieleza katika mkutano wa uchaguzi wao hiyo 28 may 2011 siku ya jumamosi, najua wabunge wengi wapya wachadema wanamsaidia HECHE KUCHUKUA HIYO NAFASI maana alisaidia pia kutetea japo kisirisiri ila kwa fitina kubwa iliyomtingisha FREEMAN HAIKAEL MBOWE mpaka sasa hajui hatma yake ya baadae maana KABWE ZUBERI ZITTO KESHA SEMA 2015 atagombea urais ndani ya CHADEMA.

-HALIMA MDEE/LUCY OWENYA/JONH MNYIKA/ wameunda timu yao ya kuhakikisha GREYSON NYAKARUNGU jina halipiti ndani ya kamati kuu kwani alihongwa na FISADI NIMROD MKONO asigombee musoma vijijini na zengwe linaendelea kwa kasi kubwa maana kikao kilichokaliwa cha siri siku mbili zilizopita kimepanga siku ya kikao cha kesho kuamsha moto wa ukweli juu ya kijana huyo.

-BERNAD SAANANE ni kijana lakini inaonekana hakubaliki na vijana wengi wa CDM maana anaonekana ni mgeni na MBOWE ana siri kubwa na kijana huyo watamalizana wenyewe hawa CDM, CV YAKE IMEJAA UZUSHI mwingi ambao akipatikana kijana aliyesoma India anaweza kuweka wazi baadhi ya mambo aliyoyaeleza.

-chadema hamna jipya mshatokota.

We huna jipya wala la maana tofauti na kujaribu kuleta Uchochezi ndani ya chama, hii habari yako mimi binafsi naitafsi kama upuuzi na upumbavu maana unaongelea mambo ya kusadikika ambayo hayana ushahidi wowote au naweza kuita unafanya uchochezi!

Nadhani ungeweza kuongea mambo ya kujenga au kukosoa kwa kutupa kasoro na wasifu wa wagombea maana wote wana haki ya kugombea kama wana-CDM; hayo unayoongea hayana nafasi tena maana kila mtu na kila mwana chama pia ana haki ya kumpigia kampeni anayemwona anafaa kwa muono wake na kwa mtazamo wake.
 
Mchange anafaa kwa sababu ni Muislam,Greyson pia ni kutoka kanda nyingine. Saanane hafai kwa sababu chama kitaonekana kimedhamiria kukumbatia uchagga.

Hata akichaguliwa atakuwa na makundi,atalipa visasi kwa watangulizi wake na wapinzani wake hasa hawa wabunge vijana ambao hawajamuunga mkono. Anaweza kuwalipizia kisasi kwenye uchaguzi wa ubunge 2015. Nimesoma nae india namjua
.

Pia kuna mdau huku anaitwa Sizinga,mtetezi wangu nilipofungiwa na mods huku wengi mkiwa kimya.Ilikuwa ni njama ya kumlinda huyu jamaa nisimwage dataz zake,na siku hiyo kwenye uchaguzi nakujaHata kama ana CV nzuri,hatutaki tena tuonekane chama cha wachagga.

Kwenye masters yake ya international Relations hana first class, nimesikia mtu mmoja akiwa anasema huyu jamaa ana first class kwenye international Relation,huo ni uzushi.


Ukweli ni kwamba kwenye uchumi ana First class.Kwani masters moja ilikuwa haimtoshi hadi akaenda kujiharibia CV? Nitamwaga dataz zote. Uchafu wake wa Kuvuruga chaguzi za watu wa kenya tutauweka hapa. Kwanza inabidi mumwangalie sana kwenye uchaguzi huu,hasa kesho. Hizo ndizo mbinu zake
 
safi sana CDM tuansubir kiongoz imara wa vijana acha na hao mazuzu kutoka chama cha magamba wanaotaka kuleta story za makundi ndani ya chama
 
Back
Top Bottom