Kamati Kuu CHADEMA yawavua Uanachama Madiwani 5 walioingia muafaka Arusha

Katika kipindi cha uchaguzi mkuu uliopita kulikuwa na tetesi kuwa baadhi ya wagombea wa ubunge walipokea fedha ila kuachia ushindi kwa kulegeza msimamo na hivyo baadhi ya majimbo kuchukuliwa na magamba na kwa kuliona hilo chadema waliona siyo vyema kufanya kazi kwa kushutumiana
baadhi ya maeneo waliunda timu kabisa kama walivyofanya mkoani mbeya kwa Shitambala na kujaribu kuwasafisha wagombea wake na kuwapa moyo wasonge mbele na kuendelea kukijenga chama lakini ukweli ulibaki pale pale kuwa kuna baadhi ya wagombea hugombea kwa masilahi yao binafsi na siyo masilahi ya Chama na ndicho kilichotokea na baadhi yao kurudi ccm na kuacha kashfa nyingi baada ya kupokea ujira wao na kuwafanya wapenda Demokrasia wengi wapoteze imani na wanasiasa.

Tukiachana na hilo nataka tuangalie namna ya mgogoro wa Arusha ulivyoshughulikiwa kwanza yalifanyika maamuzi ya awali na kutoa picha halisi hali ingekuwaje kama mambo yangekwenda vile yalivyokuwa yanapelekwa nimeshuhudia jinsi Chadema kilivyokuwa kinajitahidi kushughulikia suala hilo kwa umakini na uvumilivu wa hali ya juu kwa kuepusha mgawanyiko kwenye chama na hata kutoa fursa zaidi ya mara tatu kwa wasaliti hao kujirekebisha ili kukinusuru chama wakati wananchi tayari tulishakerwa na wao lakini Madiwani hao wasaliti hawakusikia na kuendelea hata na mchezo mchafu wa kupiga kampeni haramu ndani ya chama kwa kuwatumia badhi ya viongozi wa Chadema na ccm kwa wakati mmoja huku wasaliti hao waliokuwa wanadai wanataka kuwatumikia wananchi waliowachagua huku wakisahau kuwa umaarufu na ushindi wao ulipatikana pale walipoingia ndani ya Chadema baada ya wananchi kuchoka na ccm na ndiyo maana wananchi wa Arusha wana msemo unaosema UKIWEKA TOTH PICK KAMA MGOMBEA WA CDM. NA CCM WAWEKE MTU BORA KUCHAGUA TOTH PICK KULIKO MGOMBEA MTU WA CCM MAANA KUICHAGUA CCM NI KUCHAGUA MAAFA YA KUDUMU. Hivyo basi wasaliti walioonekana chadema hawakuwa watu bora sana kuliko wagombea wengine bali walipita kutokana quality ya chama na siyo quality ya mgombea na ndiyo maana wananchi wa Arusha tumekuwa tukifuatilia sana sakata hili kwa karibu kuona viongozi watachukua maamuzi gani baada ya kutoa fursa za kutosha kwa wasaliti hawa na nimeshukuru kwa wale ambao wamegundua makosa yao kwa kukoseshwa au kurubniwa na kurudi kwenye mstari na ninapenda kutoa angalizo hapa naomba kwa viongozi wa chadema waendelee kuwaangalia kwa karibu sana kama kweli wamejirekebisha au wanalinda udiwani wao na kesho wakuja kutugeuka tena na ninaishukuru kamati kuu wamefanya kile ambacho wengi tulikitaka na tulikuwa tayari kurudia kupiga kura hata kama tutalazimika kupiga kura mara 200 tuko tayari ili kuungana na msimamo wa viongozi wetu Mbunge Godbless Lema na viongozi kitaifa ambao walidhalilishwa, kupigwa na kuumizwa na baadhi ya wananchi kupoteza maisha yao na wengine kupata ulemavu wa kudumu na bado haikutosha wakafunguliwa kesi mahakamani kwa ajili tu ya kutetea kile kinachoaminika kuwa ni haki lakini wasaliti wachache wanakuja kuuza haki kwa bei nafuu kwa madai ya kutaka kuwajibika kwa wananchi waliowachagua!

Na kwa taarifa zilizopo kutoka kwa hawa wasaliti wenyewe wanajiandaa kuita waandishi wa habari ili kujinadi kuwa wamejiuzulu kwa masilahi ya chama na kulinda mshikamano kitu ambacho siyo kweli tunajua kuwa wamefukuzwa na chama ma sisi mitaani tutaendelea kuwaona ninyi ni wasaliti wa demokrasia ya kweli na tunawataka sasa muende mkamtumikie yule aliyewapa ile ishu na kutuletea vumbi na moshi kwenye chama.

Hongereni kamati kuu ya Chadema kwa kufanya maamuzi magumu na sahihi kwa masilahi ya Taifa na kurudisha imani ambayo ilianza kutoweka miongoni mwetu tunawatakia uchaguzi mwema wa marudio na wananchi wa Arusha tutawaonyesha hili kwa vitendo kwa kuwaunga mkono katika uchaguzi mdogo natumaini tutashinda kuliko hata awali na kurudisha viti vyote bila wasiwasi.


Mungu ibariki Chadema

Mungu ibariki Arusha

Mungu ibariki Tanzania
 
Haya ni maamuzi magumu sana, ambayo hakuna chama chochote isingeweza kuyachukua. Viva chadema! CCM has to learn from chadema.
 
Safi sana CHADEMA safisha uchafu wote, hao madiwani hawana nidhamu kabisa. Potelea mbali bora JESHI DOGO LENYE NIDHAMU KULIKO JESHI KUBWA LISILO NA NIDHAMU.... Mapambano bado yanaendelea.
<br />
<br />
watapata sababu ya kurejea/kwenda kwenye chama cha magamba hao madiwani
 
Big up CDM - you have shown the way ya 'kujivua gamba'
Nafurahia UMAKINI wenu japo itanilazimu kusafiri ili kurudia kupiga kura yangu ya diwani -demokrasia ni ghali.

Ni funzo kwa wale wengine wanaotingisha kiberiti - tunaye diwani mmoja Mwanza City council - kaa chonjo, here we mean business siyo sawa na huko ulikotoka 'CDM we dare walk the talk'

BYE BYE MAMLUKI
 
Naipongeza cc ya cdm kwa hatua hiyo huo ndio ukomavu wa kisiasa ambao taifa linauhitaji!
Nimeona Mh Zitto anawasiwasi na maamuzi hayo hebu angalia hapa alivyo sema kule twitter:

CDM cc has relieved 5 councillors party membership. It is very sad decision. At times organisations are forced to act, rightly or wrongly.
 
Kamati kuu Chadema leo tarehe 7/8/2011 majira ya saa saba usiku imefikia maamuzi magumu baada ya kuwafuta uanachama madiwani wasaliti watano ambao ni kama ifuatvyo , John Bayo kata ya Elirai , Estomih Malah ( Kimandolu ) , Charles Mpanda (Kaloleni) na Rehema Mohamed wa viti maalumu. Hawa ni wale baadhi ya madiwani walioingia kihuni bila kufuata utaratibu wa Chama .

Kutokana na uamuzi huu Tume ya Uchaguzi italazimika kupanga tarehe ya uchaguzi mdogo.

Sahau habari ya uchaguzi, Hawa watakwenda mahakamani kupinga kufukuzwa, na kesi haitaisha hadi 2015.

Mie nashangaa, huyu Malla ndie nguzo ya Chadema Arusha mjini na hata mchakato wa uchaguzi uliopita alikuwa agombee yeye kabla ya cdm M/makuu kumleta Lema. tunangojea kuona reaction ya wana-Arusha juu ya maamuzi haya, lakini naona sinema ndio kwanza imeanza!
 
safi sana ......hiki ndicho nilichokitaka......wakafie mbali kabisa ....
 
Kwa siasa za Arusha hiyo itakuwa ngumu kidogo, anywayz tusubiri tuone.......Kwa upande wangu napongeza the principled stand iliyochukuliwa na CDM.

Kwa wana Arusha wengi, permanent interest yetu ni maendeleo. CCM iliwakatisha tamaa wakaonesha kuichoka kwa kubadili wawakilishi. Sasa na hawa wawakilishi wapya nao agenda yao kuu ikiwa ni migogoro isiyokwisha hayo maendeleo yatatokea wapi?

Mkumbuke tunachotaka ni MAENDELEO hatutazami nani atayaleta!!!
 
Sahau habari ya uchaguzi, Hawa watakwenda mahakamani kupinga kufukuzwa, na kesi haitaisha hadi 2015.<br />
<br />
Mie nashangaa, huyu Malla ndie nguzo ya Chadema Arusha mjini na hata mchakato wa uchaguzi uliopita alikuwa agombee yeye kabla ya cdm M/makuu kumleta Lema. tunangojea kuona reaction ya wana-Arusha juu ya maamuzi haya, lakini naona sinema ndio kwanza imeanza!
<br />
<br />
 
Sahau habari ya uchaguzi, Hawa watakwenda mahakamani kupinga kufukuzwa, na kesi haitaisha hadi 2015.<br />
<br />
Mie nashangaa, huyu Malla ndie nguzo ya Chadema Arusha mjini na hata mchakato wa uchaguzi uliopita alikuwa agombee yeye kabla ya cdm M/makuu kumleta Lema. tunangojea kuona reaction ya wana-Arusha juu ya maamuzi haya, lakini naona sinema ndio kwanza imeanza!
<br />
<br />
no court injection on cc's decision. Hatua nyingi zilishachukuliwa kabla ya maamuzi haya.
 
Tawariiiii. Naaaaaaaaaaaaaaaaaam , Safi sana. CDM kimetuma ujumbe mzito kwa mamluki na wasaliti ndani ya chama. Tunataka Viongozi waadilifu na watii kwa katiba ya chama.

Wakienda mahakamani haitasaidia chama hakiwataki, sasa watakwenda mahakamani kwa ajili ya nani? Wao kuwa wanachama au madiwani au naibu Meya. CDM imechukua kadi zake wao wanatakiwa kuingia kwa mgongo wa waliowatuma kukosa mwelekeo.

Ila CDM wanasonga mbele.
 
Mbowe naye amesalimika?
Yeye si ndio alisaini mkataba wa maridhiano na mh.Pinda?
 
safi sana CDM. Ngoja nianze kujipanga ili nikachukue kata mojawapo kat ya hzo...
 
let then wear again their magamba, walipokelewa vema CDM lakin bado wananuka ccm. Cdm ondoa uchafu chamani.
 
Teh teh teh,

Naona CDM wameanza kuvuana gamba, ila big up kwa CDM, atleast wao wanavua gamba KWA VITENDO sio kujizungusha zungusha na kupigizana makelele kwenye majukwaa ya siasa na vyombo vya habari kama CCM.
 
  • Thanks
Reactions: FJM
Mbowe naye amesalimika?<br />
Yeye si ndio alisaini mkataba wa maridhiano na mh.Pinda?
<br />
<br />
Bado upo usingizini bwana mdogo ehee!
Kanawe uso fasta nikutume kwenye yard ya Kinana pale Kamata ukachukue ile Vogue yangu!
 
Back
Top Bottom