palalisote
JF-Expert Member
- Aug 4, 2010
- 8,335
- 1,455
Kwanza huyo mtuhumiwa na wenzie hawakukamatwa na cocain kama anvyo sema , wao walikamatwa na heroin. Pili thamani ya heroin waliyokamatwa nayo ni billioni 2.8 ambayo ni sawa na kilo 18 (Kilomoja ni wastani wa million 156 source:http://www.idmu.co.uk/heroin-price-trends.htm ). Tatu wote si watanzania na hakuna ushahidi wowote kuwa dennis ni mchungaji. Kamanda Nzowa anatakiwa atupe ushaidi kututhibitishia ni mchungaji otherwise wameshindwa kumtaja huyo mchungaji na kubaki kutapatapa.
KATIKA PICHA HAPA CHINI: RAIA wanne wa kigeni, Dennis Okechukwu na Paul Obi wote wa Nigeria, Stani Hycenth wa Afrika Kusini na Shoaib Muhammad Ayaz kutoka Pakistan wakitoka kusomewa mashitaka ya kula njama na kuingiza nchini dawa za kulevya aina ya heroin zenye thamani ya sh. bilioni 2.8, katika Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu mjini Dar es Salaam, leo. (Picha kwa hisani ya Chachandudaily.blogspot.com).