Kamanda Kamuhanda: Siwezi kujiuzulu

unaweza kusoma kitu fulani hapa kama hayati nyerere alivyosema; "ukishaonja nyama ya mtu vigumu kuacha." mwisho wa nukuru. Nilipokuwa nasikia kauli hiyo sikujua nyerere alikuwa anamaanisha nini kwa vile nilikuwa bado mdogo sana.

Kamuhada ameua songea watu wanne mwaka huu, na kisha kuhamishiwa iringa ameanza kuvuta kiti chake cha u-rpc kwa kuua mwandishi wa habari mauaji ya kinyama yeye akishuhudia amebaki gari kando yake.

Leo anakuja kwa kujiamini na bila wasiwasi kwamba hawezi kujiuzuru alikuwa anatekeleza kazi yake.

Ukiona dalili za kuzeeka vibaya na kushia kustaafu kutokuwa na maisha ya raha na starehe huku ukiwazia tamu ulizozimwaga, basi ujue mambo kama hayo si ya umri wa sasa tunaouona, ila ni jambo alilolizoea na ndio maana anajiamini na hana wasiwasi kwa mauaji yake.

Kiongozi mwenye dhamiri ya kujali maisha ya binadamu angeona aibu na kusikitikia tukio lile linalolaaniwa na watanzania na dunia nzima na hata kuisababishia serikali kupata matatizo kwa wahisani kama umoja wa nchi za ulaya uliyvotolea kauli jana.
hivi mbwa akikung´ata utamshitaki mbwa au mwenye mbwa? Hivi kosa ni la mbwa au mwenye mbwa kumuachia angáte wapita njia? Ukiona mbwa anangáta halafu mwenye mbwa hata hamzuii wala hashtuki jua mbwa kafunguliwa na huyo mwenye mbwa ili angáte! Kumaliza tatizo pressure lazima iwekwe kwa mwenye mbwa kwanza then mbwa ndio tutamaliza tatizo!
 
Duh! Hawa wauawaji wanazo guts kweli kweli. Yaani haoni kosa katika mlolongo wa makosa aliyofanya siku ile? Ni mwendawazimu au mhalifu aliyekubuhu pekee anayeweza kusema maneno kama hayo tukio lile ovu alilosimamia Kamuhanda. Pia kudai eti alikuwa "kazini" kulinda usalama wa raia na mali zao hilo nalo ni tusi juu kidonda.

Inawezekana tu Tanzania kwa hisani ya Kikwete. Sote tunajua wakuu wake hasa wa kisiasa hawawezi kumwajibisha maana kuna kazi waliyompa dhidi ya CHADEMA na kwa mujibu wa "adidu zao za rejea" jamaa yuko kwenye mstari.

Lakini haki itapatikana kwa sababu ukweli unasimama kama ulivyo, KAMUHANDA NI MUUAJI WA MWANGOSI. KAMUHANDA ALIPASWA KUWA MSHTAKIWA NAMBA MOJA KTK HIYO KESI. Muda huu hakupaswa kuwemo miongoni mwa raia maana ana mikono yenye damu huyu
 
Tz tuna matatizo mengi: uandishi na waandishi wa habari ni tatizo kubwa hasa pale wanaposahau kuwa wao ni waandishi na si watu wajipendekezao. Tatizo jingine ni serikali. Kwa kuwa walio juu hawako tayari kuwajibika, waliochini hawawezi kuwajibika. Sasa tuna tatizo kubwa la uwajibikaji upande wa uongozi na uandishi. Waandishi aidha hawajui maswali ya kuuliza au wanaridhika na vijibu uchwara. Waandishi hawaulizi maswali ya wananchi bali maswali yao. Naamini walimu wa uandishi wanaelewa hili na wanapaswa kuangalia walikazie kwenye mafunzo yao na kisha waache kujipendekeza
 
Ushauri kwa kamanda Kamuhanda, ahakikishe SSM inaendelea kutawala katika kipindi chote cha kustaafu kwake. Akifanya kosa akashindwa kuisaidia ssm kuendelea kubaki madarakani angalau mwaka 2015, basi akae akijua "we will bring him to justice OR we will bring justice to him".
Hana uchaguzi katika hili, ni bora ahakikishe SSM inaendelea kukaa madarakani kwa faida yake.
 
hivi mbwa akikung´ata utamshitaki mbwa au mwenye mbwa? Hivi kosa ni la mbwa au mwenye mbwa kumuachia angáte wapita njia? Ukiona mbwa anangáta halafu mwenye mbwa hata hamzuii wala hashtuki jua mbwa kafunguliwa na huyo mwenye mbwa ili angáte! Kumaliza tatizo pressure lazima iwekwe kwa mwenye mbwa kwanza then mbwa ndio tutamaliza tatizo!

Hapa Mzalendoasilia umenena
 
kama sijakosea kwa Idara za usalama habari ya kujiuzulu au kug"atuka haipo kwa mujibu wa taratibu zao za kazi ila akipewa mission akaitekeleza vibaya anahukumiwa na mahakama so kamuhanda achunguzwe mission aliyopewa ilikua kuua? kama ilikua bahati mbaya anahunkumwa kwa uzembe nadhan (sins uhakka) hata chadema katiak maazimio yao wano uwezo wa kumshinikiza Rais au IGP kumchukulia huyo kamanda hatua kama kosa lipo lakini c kumtaka ajiuzuru.Kubwa ni kwanza tujue MISSION ilikua nn? may be aliambiwa UA.ndo maana nashauri wassitwe JESHI LA POLIS bali waitwe POLIS SERVICE kwa maana wanahudumia Raia sio jesh kwa Rai
 
Haya ni matokeo ya kuwa na DHAIFU, vinginevyo alistahili kufukuzwa kazi siku nyingi.
 


“Kwa hiyo, siwezi kujiuzulu kwa sababu tukio hilo la kifo lilitokea wakati wa kutimiza wajibu wa kutii sheria bila shuruti,” alisema Kamanda Kamuhanda.

Alipoulizwa kuhusiana na kuwajibika kutokana na mauaji hayo alisema, hawezi kuwajibika kwa sababu hana makosa.

“Niwajibike kwa kosa lipi?, kuna kosa mtu anaweza akawajibika, lakini kama huna kosa huwezi kuwajibika, haiwezekani watu waliofanya makosa wenyewe kwa kuandamana bila uhalali wasiwajibike halafu mimi niwajibike, haiwezekani.

“Kwa hiyo, hicho ndicho kilichokuwa kinafanyika, kilichofanyika ndiyo utii wa sheria bila shuruti, wangetii sheria bila shuruti yote yasingetokea,” alisema.


This is even more shocking. Kamuhunda ana-confirm kwamba mauji ya Daudi Mwangosi yalikuwa yamepangwa. Hapo kwenye red ndipo tunapata confirmation kwamba sasa polisi wanaua! Kama umefanya kosa hawekupeleki mbele ya vyombo vya sheria, wao wanakuua on the spot!

Adhabu ya kifo inatolewa na nani? Na ni mambo gani yanayofanya mtu ahukumue adhabu ya kifo? Daudi Mwangosi alifanya kosa gani, na hilo kosa (kama lipo) adhabu yake ni kuuliwa kinyama na polisi? Increadible!

Kamuhunda is obviously killer on our street, na anasema wazi kabisa yeye anaua! It will be interesting kusikia kauli ya IGP.
 
Hii ndio Tanzania bana hakuna kujiuzuru mtu hapa dah hii nchi kweli.hatari sana maana kwa namna hii hatutafika popote pale hata maendeleo ni ngumu sana kuja kama hakuna watu watao kuwa wanawajibika
 
kwa nini waandishi wa habari huwa mnawaauliza hawa mnaowauliza maswali mwongozo? kwa nini usimuulize ni makosa gani ambayo yanapaswa mtu akawajibika kama alivyosema kuna makosa ya kuwajibika?

Hiyo ni jeuri ya kulindwa na ccm hasa waziri nchimbi.Hii inaonyesha wazi kuwa huu ni mpango ambao ulikuwa umepangwa.Huyu kamanda nasita na kuchela kusema ni mbumbu wa sheria.hata kama ni utii paipo shuruti, ni wapi katika hilo sheria inaruhusu kutoa uhai wa mtu kwa majibizano?na kama hata alikuwa hakutii sheria hivyo ilipasa polisi kumuua?na je yeye kama mwangosi ndo aliyetoa amri ya kuandamana bila kibali au alikuwa nachukua habari kwnye tukio hilo?je raia kufa mikononi mwa polisi bila ulizi wa maisha yake si kosa la kiutendaji katika taaluma ya kipolisi?huyu kamanda mbona anawatukana watanzania! na nani anamtumikia?kama aliapa kiapo cha kutumikia katiba , je haoni katiba iko wazi kutetea na kulinda maisha ya mwanadamu?hawa ndo makamanda amao kiapo chao hawakijui na pia hawajui wanamtumikia nani.kama ni watanzania wanasema umkosea vyema akasikiliza lakini kama natumikia watawala waliomtuma, ndo maana mjeuri na kiburi.
 
Ninaamini kuna tatizo. Kwanza kesi ipo mahakamani, hivyo kwa polisi aliyesoma asingeliweza kusema lolote kwani ni kitendo cha kuingilia mwenendo wa kesi. Pili, nchi yetu ina wengi waliokata tamaa licha ya kuwepo maendeleo mazuri katika baadhi ya mambo ya msingi.

Huyu polisi ni miongoni mwa watu wanaoiabisha serikali kwa kujua au kwa kutojua. Sijui Curriculum Vitae yake. Ukilitizama suala hili kwa logic utagundua kuwa, kama yeye alifanya sawa kuwa ni utii wa sheria, basi kinachojiri moja kwa moja ni "G2573, Pasificus Simon," Amefanya kazi nzuri na hastahili kushitakiwa. Polisi wanatakiwa kujua sheria. Hii inaweza kuathiri kesi na matokeo ya kesi yatazingatia maoni ya Askari mzito aliyeyatoa wakati wa kesi labda wakili asinzie.

Huenda waliokuwa wanamaliza sekondari bila kujua kusoma na kuandika wapo wengi na walianza zamani. Ni lazima serikali ichukue hatua. Kujiuzuli kwa huyu jamaa na wenzake akiwemo Mwema na Nchimbi si dhambi. Kutaiongezea heshima kubwa serikali pamoja na wao wenyewe. Kama kweli wanakipenda chama wajiuzulu kwani wanaendelea kuwa mwiba kwa serikali. Watu hata hawajasahau kifo husika, ndugu bado hawajafanya arubaini, yeye anadai kuwa ameua kihalali. Shame to him. Isaidieni serikali yenu. Mjiuzulu mtaheshimika baadae
 
Anacheza na moto huyu...hajui mambo huwa yanabadilika. Akijiingiza kwenye malumbano na vyombo vya habari sasa hivi atalazwa chini chali.
 
Hiyo ni jeuri ya kulindwa na ccm hasa waziri nchimbi.Hii inaonyesha wazi kuwa huu ni mpango ambao ulikuwa umepangwa.Huyu kamanda nasita na kuchela kusema ni mbumbu wa sheria.hata kama ni utii paipo shuruti, ni wapi katika hilo sheria inaruhusu kutoa uhai wa mtu kwa majibizano?na kama hata alikuwa hakutii sheria hivyo ilipasa polisi kumuua?na je yeye kama mwangosi ndo aliyetoa amri ya kuandamana bila kibali au alikuwa nachukua habari kwnye tukio hilo?je raia kufa mikononi mwa polisi bila ulizi wa maisha yake si kosa la kiutendaji katika taaluma ya kipolisi?huyu kamanda mbona anawatukana watanzania! na nani anamtumikia?kama aliapa kiapo cha kutumikia katiba , je haoni katiba iko wazi kutetea na kulinda maisha ya mwanadamu?hawa ndo makamanda amao kiapo chao hawakijui na pia hawajui wanamtumikia nani.kama ni watanzania wanasema umkosea vyema akasikiliza lakini kama natumikia watawala waliomtuma, ndo maana mjeuri na kiburi.

huyu kamanda ni mshirikina. Kapanda hadi hapo kwa kuroga na kutambika ambako huko walimpa hadi ujasiri wa kulala juu ya kaburi usiku wa manane, vinginevyo hangekuwa na ujasiri huo wa kuua watu watano deliberately na kuendelea kuwa na kiburi. Wachawi hawana hoja wao ni upumbafu mtupu umewajaa kama huyu memba wao anachokifanya.
Ni lazima tumuombee atubu, kinyume chake amechagua moto wa milele.
 
Back
Top Bottom