Mzee Mwanakijiji
Platinum Member
- Mar 10, 2006
- 33,475
- 39,988
Jina la Michael Kamuhanda nilipolisikia tu nilihisi kama nimewahi kulisikia tena siku si nyingi. Nina uhakika na wengine wamelikumbuka pia kuwa ndiye aliyekuwa Kamanda wa Polisi wa Ruvuma ambapo mapema mwaka huu (Februari) wananchi 4 waliuawa napolisi walipokuwa wakijaribu kuandamana kwenda ofisi ya Mkuu wa Mkoa. Natamani wamlete Dar-es-Salaam pia ili watu waelewe tatizo tulilonalo. Nikimuita ni mhalifu sijui kama nitakuwa nimetia chumvi sana... haiwezekani ndani ya mwaka mmoja kamanda unasimamia mauaji ya raia kisa wanataka kuandamana tu! Hivi hana mbinu nyingine zozote kichwani mwake zaidi ya kuwa trigger happy!