Kama zombe alifikishwa mahakamani kwanini hawa walioua arusha wasipelekwe?

DENYO

JF-Expert Member
Sep 14, 2010
698
57
Naomba wanajf -great thinkers mnisaidie -kama zombe na wenzake walifikishwa mahakmani kwa kuua kwanini hawa walioua arusha wasifikishwe mahakamani -ili mahakama iseme walipaswa kuua au la? Kwa kuwa hakuna mwenye idhini ya kutoa uhai wa mwenzie kwanini hawa wa arusha ambao wamekiri kupitia kauli ya chagonja kwamba waliua kweli -kwanini wasifikishwe mahakamani kujibu kosa la kuua? Mahakama ndio chombo pekee cha kusema.

Nisaidieni hawa askari walioua wako rumande au wako wapi??? Manake hata nyumbani ukimkuta jamaa analamba mkeo ukiua lazima ukamatwe -sasa hawa waliokusudia wako wapi? Wamekamatwa? Au ndio kusema kama alivyosema kamishina chagonja kwamba wanatetea serikali kwahiyo anataka umma uamini kwamba waliua kwa magizo? Kwahiyo askari wataendelea kupeta bila hata kupelekwa mahakamni kama akina zombe???? What a double standadrd is this???
 
ni mambo mengi uwa yanafanyika ktk nchi hii kama maigizo,hakuna sheria inayofuatwa lakini cha ajabu wakibanwa wao utasikia tufuate sheria lakini ya kwao sheria haipo naomba uelewe kuwa malipo ya wauaji yapo tu kwani kwa kina zombe imekuwaje?ditopile yupo wapi?aliyeua zanzibar naye yupo wapi?suala la hao askari lisikupe shida kwani si muda mrefu watatajana mitaani nadhani kesi itaishia hapo.

kuwa na subira denyo ijapokuwa inauma yana mwisho.
 
Back
Top Bottom