Kama yamekushinda ondoka kwa heshima

Mkulima wa Kuku

JF-Expert Member
Jan 13, 2011
1,270
533
Nimepata bahati ya kutembelea nchi kadhaa hapa ulimwenguni. Wenzetu wana shida zao kama sisi tulivyo na za kwetu. Kinachotofautisha wenzetu ambao tunasema wanashida na sisi ni kuwa hata kama wanalia kuna shida kuna mambo ya msingi hakuna anayeweza kuyachezea. Kwa mfano miundombinu katika ujumla wake. Ukifika kwenye mji kama Harare nimepata muda wa kuuzunguka kwa miaka mingi karibu wote. Sijaona Squatter area hata moja. Wabongo wenzangu wanaoifahamu Harare watakubaliana nami. Mpango mji ukiwekwa hakuna yeyote atakayeuvuruga kwa namna yoyote. Ukijenga kibanda ukasema unataka uongeze kwenye nyumba yako kesho asubuhi kinavunjwa kwa sababu ya mipango mji. nafasi za wazi zote ziko vilevile tangu mkoloni.

Mheshimiwa Mkulu wetu anakimbiliaga sana kwenda kusuluhisha migogoro ya wenzake kule nje, lakini ya kwake imemshinda...gogoro la umeya Arusha ameliachia na linazidi kukua huku kila siku mara Kenya, mara Somalia mara kule.

Ushauri wangu wa bure kwa JK ni kuwa kama nchi imemshinda awaachie wengine kuliko uharibifu huu tunaouona sasa hapa Bongo.
Nawasilisha.
 
Mimi naona umewakilisha katika mlango mdogo sana wa Kikwete kushindwa kuongoza nchi. Nionavyo mimi rais wetu inabidi ajiuzulu kwa sababu kuu tatu:
1.0 Kishindwa kisimamia uchumi wa nchi hadi saizi serikali ipo hoi kimapato wakati matumizi yanazidi kuongezeka kila kukicha. Hii baada ya muda ni dalili ya serikali kufilisika maana itafikia hatua itashindwa kukopesheka. Kuna kipindi cha Mkapa tulishawahi kuambiwa tufunge mikanda kwa sababu nchi inalipa madeni. Tulikuwa tunapewa takwimu sahihi na kinacholipwa lakini siku hizi ukimya ndiyo umetalawala.
2.0 Kushindwa kukemea maovu na kibaya zaidi hata yale aliyoyasema hadharani, mathalani alitangaza zoezi la kujivua gamba lakini mpaka leo bado jambo hilo limezua mgogoro mkubwa mpaka saizi kisa ni udhaifu wa mheshimiwa kusimamia mambo ya chama. Hili haliishii hapa, litakuwa linakwenda mbali zaidi hata katika mambo nyeti serikalini.
3.0 Suala la ajira kwa vijana. Nchi imekuwa ikikabiliwa na tatizo la ajira kwa vijana kuliko kipindi chochote kile. Mfumo usio rasmi haupewi kipaumbele katika kukuza soko la ajira.
Yapo mambo mengi sana ya kuonyesha JK nchi imemshinda, mengine mtajazia nilipokomea.
Nawasilisha.
 
Mie nadhani vasco anataka kuiacha nchi imeingia vitani alafu akimbilie nje
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom