Kama wewe ungefanya nini

......Cha kushangaza shule kuna mambo mengi inatokea wanasoma na kijana mwingine ambaye wanakuwa karibu sana naye kila ukiulizia na umeanza kuhisi mahusiano kati yao. Mpenzi wako anakwambia kuwa usiwe na wasiwasi siwezi kutembea na mtu kama yule mie.

Sawa, kuwa na uhusiano na mtu mwingine hasa mashuleni ni mambo ya kawaida kabisa, ila hiyo sentensi ya mwisho ndiyo ambayo unatakiwa kuitilia shaka. Mwongo! hio ni defence mechanism! Huyo ana uhusiano wa kimapenzi na mhusika

......Inapita muda mawasiliano yanaendelea na inakuja kufikia huyu bwana wanatengana mwingine anahamia mikoani na mwingine anabaki.Huyu bwana nakuja mkutanoni dar na hawajaonana , Huku huyu mpenzi wangu anagundua kuwa huyu bwana alikuja na anamwambia umekuja bila kuonana , maana yake nini lakini..

...Maana yake ni kwamba ni utovu wa nidhamu kwa rafiki wa 'mkeo' kufika Dar na kutomtafuta mtu 'wake' wa karibu ambae ni mpenzio. Ingekuwa ni rafiki wa kawaida tu wa mpenzio, asingelaumu namna hiyo unayoielezea hapa. Kwa hiyo mpenzio alishtushwa na tabia hii! Swali kwako Sospeter..huyu rafiki wa mpenzio ana tabia ya kukupigia simu mara kwa mara hata kukujulia hali tu? Kama jibu ni ndio, basi huyu ni rafiki wa kawaida wa mkeo. Hama jibu ni hapana, huyu ni mpenzi wa mpenzio! Rafiki wa kawaida huwa habagui, anapiga simu kwa wote muda wowote!


....... Baada ya hapo ujumbe kama huu unatumwa “ Nimekumiss sana mpenzi wangu" kutoka kwa mwanaume akitaja na jina la mpenzi wangu” .

Brother,
Hivi mpaka hapa unahitaji elimu gani ili kuelewa kuwa huyu jamaa ni mpenzi wa demu wako? Please Wake up! Kama una moyo mpige kibuti haraka sana.
Inaonesha mwanamke anakutumia!


..... na mwanamke anajibu , wewe tu umeni tupa kabisa, na jamaa anasema nikija nitakutafuta hata usiku , ni wewe tu. Na mara kwa mara anakuwa anampigia simu ukimwuuliza anasema ni mawasiliano tu.


....Kama jamaa ana nia njema aje kwako huo usiku anaotaka, sio kumtoa mpenzio usiku.


.... Ila hii ya kutembelewa hata usiku ni kali na imeniweka mahali patata. sielewi.

Na utakaa hapo "PATATA" hadi lini? Usisubiri kufa kaka, amka.

Sasa hii inanikatisha tamaa kabisa.

Usiishie kukata tamaa, chukua hatua


Je nishaurini jamani , huyu dada nampenda na natarajia ndoa na yeye.

Hakuna ndoa hapo. When one door is closed, there are many more open! Seek for 'em!
 
cha msingi muulizie huyo binti kitu gani humridhishi hasa kwenye mapenzi yenu kinachomfanya atoke nje ya penzi lenu. Hapo sasa ndio utajua umfanye nn huyo jamaa.
 
Una mpenzi wako unayempenda sana na unamtimizia kila kitu na umekaa naye takribani miaka kama mitano hivi . Halafu ilitokea amekwenda shule kusoma na ukamsaidia kwa hali na mali na jinsi ulivyoweza. Cha kushangaza shule kuna mambo mengi inatokea wanasoma na kijana mwingine ambaye wanakuwa karibu sana naye kila ukiulizia na umeanza kuhisi mahusiano kati yao. Mpenzi wako anakwambia kuwa usiwe na wasiwasi siwezi kutembea na mtu kama yule mie. Shule inamalizika ukiwa unamsaidia kwa kila kitu . Inapita muda mawasiliano yanaendelea na inakuja kufikia huyu bwana wanatengana mwingine anahamia mikoani na mwingine anabaki.Huyu bwana nakuja mkutanoni dar na hawajaonana , Huku huyu mpenzi wangu angundua kuwa huyu bwana alikuja na anamwambia umekuja bila kuonana , maana yake nini lakini. Baada ya hapo ujumbe kama huu unatumwa “ Nimekumiss sana mpenzi wangu kutoka kwa mwanaume akitaja na jina la mpenzi wangu” na mwanamke anajibu , wewe tu umeni tupa kabisa, na jamaa anasema nikija nitakutafuta hata usiku , ni wewe tu. Na mara kwa mara anakuwa anampigia simu ukimwuuliza anasema ni mawasiliano tu. Kwa kuwa mtu unampenda , unaamini. Ila hii ya kutembelewa hata usiku ni kali na imeniweka mahali patata. Kumpenda nampenda na nimeweka kweli pendo kwake mbele . Sasa hii inanikatisha tamaa kabisa.

Je nishaurini jamani , huyu dada nampenda na natarajia ndoa na yeye , huyu bwana ana mke na watoto wake . Sasa waungwana nipeni jawabu hapo sielewi.


Pole sana mkuu Sospeter, haya mambo yanachanganya sana

Ulifanikiwa kujua kama demu wako anamegwa

https://www.jamiiforums.com/mahusia...zi-wako-kafanya-tendo-la-ndoa-kwingineko.html

Na je mbaya wako umemchukulia hatua gani au bado unatafuta ushahidi

https://www.jamiiforums.com/mahusiano-mapenzi-urafiki/27292-mbaya-wangu-ni-huyu.html
 
cha msingi muulizie huyo binti kitu gani humridhishi hasa kwenye mapenzi yenu kinachomfanya atoke nje ya penzi lenu. Hapo sasa ndio utajua umfanye nn huyo jamaa.

Pretty, maswali yanamna hiyo yanatakiwa siku za mwanzo kabla mambo hayajaharibika. Akimuuliza sasa hatapata jibu sahihi
 
Pretty, maswali yanamna hiyo yanatakiwa siku za mwanzo kabla mambo hayajaharibika. Akimuuliza sasa hatapata jibu sahihi
solution ni kumuacha huyo binti maana sio mwaminifu. Akioa ajue anatafuta matatizo. Nyota njema.........................
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom