Kama Uchaguzi Mkuu Ungefanyika Leo...

Let's call a spade a spade.Mjengwa hana tofauti na Michuzi.Hawa ni wakereketwa wa Kikwete.Mjengwa aliwahi kuandika makala moja ya ajabu sana huko Raia Mwema akitetea safari za Kikwete.Na juzijuzi tu eti kamsifia Kikwete kwa "moto alioanzisha ndani ya CCM kudhibiti uchakachuaji"

Aliandika (namnukuu)
"Kama wengine, nimekuwa nikifuatilia kinachoendelea katika nchini sasa. Ninachoandika hapa ni fikra zangu huru katika kujaribu kuchambua kile ninachokiona. Naam. Mambo hayaendi kama yanavyotakiwa yaende kutokana na mazoea. Rais na Mwenyekiti wa Chama Cha Mapinduzi, Jakaya Kikwete amewasha moto ndani ya chama chake.

Kwa ninayeangalia kutoka nje nakiona kivuli katika moto aliouwasha Kikwete. Ndiyo, hata moto una kivuli chake. Yawezekana kabisa, kuwa huu ukawa ni mwanzo wa mwisho wa tufani iliyowakumba Watanzania wengi kwa muda mrefu. Kila baya jema, walitwambia wahenga.

Watanzania tuna kitu tunahisi tumekipoteza. Huenda watakaonielewa zaidi ni Watanzania wa kizazi changu; kizazi cha Azimio. Tumezaliwa na kukulia katika kipindi kinachotufanya tujisikie tuna kitu tumekipoteza katika wakati wetu huu. Si kingine, bali ni kile ambacho Wafaransa wangeweza kukiita "L'esprit Mwalimu" – Ari ya Mwalimu.

Nataka niamini, kuwa anachokifanya Rais Kikwete, hususan, ndani ya CCM, ni kurudisha misingi ya Chama Cha Mapinduzi na hivyo basi, "Ari ya Mwalimu".

Inahusu kujenga misingi ya usawa na haki katika jamii"

Kuhusu safari za Kikwete,Mjengwa aliandika (namnukuu tena)
"Na wengi waliojaribu kuonyesha upande ulio chanya juu ya safari hizo wamekuwa wakiandamwa. Kuna wakati ni lazima tuelezane ukweli. Hata kama Rais aliye madarakani ana kasoro zake ambazo tumekuwa tukiziainisha, lakini bado ana mambo ambayo amefanikiwa sana katika uongozi wake.

Mojawapo ni namna alivyofanikiwa, kupitia ziara zake za kikazi za nje ya nchi, kujenga ushawishi kwa asasi za kiserikali na zisizo za kiserikali za nchi alizotembelea. Amefanikiwa kuzifanya nchi na asasi hizo kuisikiliza Tanzania kama mshirika wake wa kimaendeleo.

Kuna mifano mingi hai ya mafanikio ya ziara za Rais Kikwete nje ya nchi; mradi wa kutokomeza Malaria nchini ambapo Rais mwenyewe, sio tu amesaidia kuwajengea imani wanaotusaidia, bali yuko mstari wa mbele katika kuongoza mapambano hayo.

Juzi hapa Shirika la Ndege la Uturuki limeanzisha safari za ndege kuja Tanzania. Ni kufuatia ziara ya Rais Kikwete aliyoifanya Uturuki miezi kadhaa iliyopita. Rais amesaidia kuwajengea imani kwetu Waturuki, kuwafanya wafahamu zaidi umuhimu wa kuwa na ushirikiano nasi.

Lakini hilo la ndege ya Uturuki kutua Dar es Salaam halina maana ya Waturuki na watu wa mataifa mengine kuja kufanya utalii na biashara nchini mwetu tu. Limetatua pia kero ya muda mrefu ya mahujaji wa Kitanzania kusafiri kwenda kuhiji Mecca.

Ni fursa pia kwa Watanzania kuutumia usafiri huo wa gharama nafuu katika kufanya biashara na Uturuki, na nchi nyingine za Mashariki ya Kati, Ulaya na Marekani.

Hapo juu ni mifano miwili tu kati ya mingi ya mafanikio yatokanayo na ziara za Rais Jakaya Kikwete nje ya nchi. Ukiwa ni mtu wa hulka ya kubeza tu, mwishowe nawe utabezwa! Hilo la mwisho ni la hasara zaidi kwa anayebezwa na jamii kwa ujumla."

Mjengwa anadai hapa (namnukuu)
....Na kama utaweka hapa ukumbini makala ya nyuma yenye kufanana na hiyo niliyoandika, basi, nitaacha kabisa kuandika na nitajitoa uwanachama wa JF....
.Hivi hizo makala mbili tu hapo si uthibitisho tosha kuwa wewe ni mnazi sugu wa Kikwete?Unapozungumzia "moto aliowasha ndani ya CCM" na kumlinganisha na Baba wa Taifa (huko aliko anatetemeka kwa tusi hilo) halafu kwa makusudi unakwepa kuzungumzia upande wa pili wa shilingi-yaani huwezi kuzungumzia failures za CCM pasipo kumhusisha Mwenyekiti wa Taifa wa chama hicho-inaleta tafsiri gani kama sio unazi.

In same manner,unatetea utalii wa Kikwete huko nje ya nchi na kutoa mifano dhaifu ya kampeni za malaria na kuanzishwa kwa safari za ndege za Turkey,lakini kwa makusudi unakwepa kubainisha kuwa kazi hizo zingeweza kabisa kufanywa na mabalozi wetu,kama sio waziri wa mambo ya nje.Kwani trade centres zetu zinafanya kazi gani?

Haihitaji hata short course ya uandishi wa habari kutambua msimamo wako pale Raia Mwema.Kamwe hujawahi kumlaumu Kikwete hata iweje.Na japo utajitetea kuwa huo ni mtazamo wako na kutukumbusha uhuru wa kutoa mawazo yako binafsi,wasomaji wako pia tungependa kukukumbusha kuwa mawazo mufilisi yana-deserve kukabiliwa haraka iwezekanavyo kwa vile yakiachwa yanaweza kujenga kupata status ya kuwa facts.

Hebu tuonyeshe hapa where we dare to speak openly ni lini uliwahi kuandika chochote kinachomkosoa Kikwete?

Utafiti wako wa kijiweni kuhusu matokeo ya uchaguzi wa mwaka huu hauna tofauti na vitisho vya majini ya Sheikh Yahya.Or is it majini yanayomlinda Kikwete yamevamia JF?
 
Mlalahoi,
Mkuu mimi nadhani huo ni mtazamo wa Maggid na pengine hata iwe ushabiki wake lakini bado ni mawazo yake na kaelezea sababu zake. Mimi nadhani la muhimu hapa ni kutazama mapungufu yetu, tuachane na utabiri wake hata kama amekosea muhimu ni Chadema kutokuwa na mapungufu ambayo wajinga wengi wanaweza kuyatumia. na hata kuzigawa kura za Wananchi.

Huko Marekani kuna kikosi cha watu wanaitwa Tea Party hawa jamaa wamekamia kumwondoa Obama na wanafanya damage kubwa sana kiasi kwamba wajinga wengi wanawakubali.. Sasa kinachofanyika Marekani ni kujibu mapigo kwa kurekibisha kauli zao.. Obama na team yake kurekebisha makosa kama yapo na kuendelea kuonyesha uwezo mkubwa wa mabadiliko yaliyokusudiwa dhidi ya kashfa zinazotungwa kila kukicha.
 
Kuna wimbo wa bahati bukuku siukumbuki vizuri ila una maneno yafuatayo
...... alipoianza safari walimtia moyo,alipokaribia mafinikio waliibua vikwazo,alipooneshwa kushindwa wakalitoa unabii, nilisema hafiki mbali katika elimu yake/ndoa yake n.k

hapa mjengwa kikubwa anachotaka kujenga ni sifa tu mbele za watu pindi matokeo yanapotoka kuwa nililiona hili mapema kabla hata uchaguzi na nililisema watu wakanibishia. Watu wa jamii hii sio wa kuwaamini sana maana pamoja kuwa wanaweza kuonesha kutaka mabadiliko lakini ni kikwazo wao wenyewe. Wanahitaji mabadiliko huku wakitabiri kuwa haiwezekani mabadiliko yakaja leo au kesho tunasafari ndefu, akija mtu ambaye anaonesha wazi kuleta mabadiliko wao huibua vikwazo kwa sababu wanataka unabii wao utimie!! Ndio maana ukisoma makala nyingi hapa nyumbani kila mwandishi anajitahidi kadri awezavyo kuonesha anauwezo wa kuona mbali maneno kama "nimeshawahi kusema huko nyuma kwenye moja ya makala zangu" inaonesha waandishi jamii ya mjengwa wanavyoweza kutabiri.
Nisikulaumu sana ila nini malengo ya kusema ccm ingeshinda chadema itafuatia na cuf, hasa wakati huu, lengo ujekusema uliliona mapema kabla ya wenzio siyo kweli mjengwa umepotoka hukuwa wa kwanza japo umeingia kwenye list! Ungetujuvya pia unaona ccm itashinda kati ya asilimia ngapi? Ili tukupime usahihi wa mazoea yako pia! Kwa imani hii mjengwa umekubali kufanana na watu wakijiji wanao amini ktk ccm japo wewe umejivika kuwa msemaji wao! Big up! Ulichokiandika hapa hata usingekiandika haina maana kuwa msimamo wako ungebadilika ila sababu unataka ujiko ndio maana ukaandika! Anyway kazi nzuri inapendeza machoni pa wakubwa heko!
 
NAANDIKA haya kutokana na uzoefu wangu wa kufuatilia kwa karibu mienendo ya chaguzi zetu. Kwa chaguzi nilizozishuhudia kwa macho na nilizosoma vitabuni. Naam. Zikiwa zimebaki siku 48 ( Leo Jumapili, Septemba 12, 2010) naiona hali ifuatayo kama uchaguzi ungefanyika leo hii;
Mgombea Urais wa Chama Cha Mapinduzi, Jakaya Mrisho Kikwete angeibuka mshindi . Dr Wilbroad Slaa ( CHADEMA) angechukua nafasi ya pili na huku Profesa Ibrahim Lipumba ( CUF) akishika nafasi ya tatu. Wagombea wa vyama vilivyobaki wangekuwa wasindikizaji kwa kupata chini ya asilimia 5 ya kura zote kwa pamoja.
Hali hiyo ingeakisi pia matokeo ya uchaguzi wa wabunge na madiwani ( Bara). Tafsiri yake; Jakaya Mrisho Kikwete angeunda Serikali huku yeye na chama chake wakikabiliwa na changamoto kubwa kutokana na upinzani utakaokuwa umeongezeka nguvu ndani na nje ya bunge kutokana na ujio wa Dr Slaa kama mgombea Urais katika uchaguzi wa mwaka huu.
CCM wanajivunia:
Kuwa ni chama kikongwe, kikubwa na kilichotawala kwa muda mrefu. Kuna hata wanaokipigia kura chama hicho ‘ Kwa mazoea tu’. Na katika nchi zetu hizi; kukiondoa chama kilicho madarakani, Chama kilichopigania uhuru au kinachotokana na chama kilichopigania uhuru ni kazi ngumu sana. Kwa anayetaka kufanikiwa katika hilo, anahitaji kwenda ilipo mizizi ya chama hicho. Ni vijijini. Na huko vijijini kwa leo hii chama wanachokijua ni CCM. Naam. Ndio ‘ Zimwi’ wanalolijua. Mwanakijiji atatembea kwa miguu kilomita kumi kwenda kuhudhuria mkutano wa CCM. Atakwambia amepewa taarifa ya mkutano na Mjumbe wake wa nyumba kumi. Hivyo basi, CCM wanajivunia mtandao wao wa kichama kuanzia ngazi ya Balozi wa Nyumba Kumi, shina, tawi na kuendelea. Na tayari CCM ina wabunge kumi waliopita bila kupingwa na madiwani zaidi ya 100 kwa mujibu wa gazeti la NIPASHE la leo Jumapili.
Udhaifu wa CCM:
Pamoja na kuwa ni chama kikongwe na chenye uzoefu, wakati mwingine inashangaza kuona katika maeneo kadhaa kinavyoshindwa kusoma alama za nyakati. Kura za maoni ni mfano wa udhaifu wa CCM kushindwa kubaini kuwa kwa utaratibu mpya ulijiojiwekea katika kupata wagombea walisahau umuhimu wa kuchuja majina ya wagombea kwanza ili kubaini wale ambao wangewaletea shida. Badala yake, waliacha wanachama waamue halafu bado chama nacho kikaingilia kati kuamua tena. Kuna adhabu ya chama kutoka kwa wanachama wake inakuja kutoka katika baadhi ya majimbo. Na kinachojitokeza zaidi sasa ni kubadilika kwa mwenendo wa wapiga kura. Kidogo kidogo wameanza kuangalia zaidi watu na si chama kwenye ngazi ya udiwani na ubunge. Hizi ni dalili mpya.
CHADEMA:
Ujio wa Dr Slaa:
Sio tu umewashangaza CCM na mgombea wake urais, bali pia unaonekana kuwashangaza CHADEMA wenyewe wanaoonekana kutokujiandaa na namna Dr Slaa alivyopokewa na wananchi.
Udhaifu wa CHADEMA
Unajidhihiri kwenye eneo la oganaizesheni na kifedha. Bado CHADEMA haina uwakilishi mpana katika ngazi za mashina na matawi. Dr Slaa anaweza kutua na helikopta Pawaga Iringa, lakini mara ile akiruka, huku nyuma hakuna watendaji wa CHADEMA wa kufanya kazi ya CHADEMA. Kuna taarifa pia za wagombea wake ubunge na udiwani kukosa nguvu za kifedha kuendesha kampeni . Taarifa hizo zilizoripotiwa kwenye vyombo vya habari haziwezi kupuuzwa tu. Hapa inahusu udhaifu katika maandalizi. Kuna wagombea wa CHADEMA watakaoanguka katika chaguzi kwa tatizo hilo.
Zitto Kabwe,
Ni kada nyota ndani ya CHADEMA lakini ‘sarakasi’ zake za kisiasa huenda zinachangia kukidhohofisha chama chake kuliko kukipa nguvu. Majuzi hapa aliripotiwa na magazeti kutamka hadharani kuwa anajiandaa kugombea urais 2015. Zitto Kabwe anaacha maswali; Kulikoni ndani ya CHADEMA? Je, Dr Slaa ni mgombea wa ‘msimu’ tu? Au ndio sababu Zitto Kabwe hakuhudhuria Mkutano wa ufunguzi wa kampeni za CHADEMA? Kuna watakaouliza.
Inachojivunia CHADEMA:
Bado ni chama kinachoonyesha kuwa na mvuto kama kitajipanga vema. Kesi iliyofunguliwa Mahakamani dhidi ya Dr Slaa kuhusiana na masuala binafsi ya mahusiano inaonyesha kumtangaza zaidi Dr Slaa kwa wapiga kura wanaotia shaka wakati uliotumiwa kuibuliwa kwa suala hilo. Kuna watakaompigia Dr Slaa ‘ Kura za Kumhurumia’.
Umakini Wa CHADEMA:
CHADEMA imekuwa ikijinadi kama chama makini machoni mwa wapiga kura. Hata hivyo, taarifa zilizochapwa leo ( MWANANCHI) kuwa Naibu Katibu Mkuu , CHADEMA, Zanzibar huenda akaondolewa kwenye timu ya kampeni ya Dr Slaa kwa kuwa amekuwa kero inaonyesha namna timu ya kampeni ya CHADEMA ilivyoshindwa kubaini mapema kuwa Naibu huyo alikuwa kero kwa wapiga kura. Maana, kwa utamaduni wa Watanzania namna Naibu yule Katibu Mkuu alivyokuwa akimfananisha Dr Slaa na Bwana harusi na kauli nyingine pale viwanja vya Jangwani ilikuwa ni ‘ matusi’ hata kama kuna waliotaka kupewa tafsiri sahihi ya neno hilo. Ni heri kwa CHADEMA wameamka na kubaini kero hiyo ndani ya nyumba yao.
Kauli na Ishara:
Kama hakuna aliyelifikiria hili ndani ya CHADEMA, basi, hata kama CCM wanaimba ‘ Wapinzani tuwalete , tuwakatekate’ , hilo ni kosa ambalo halipaswi kujibiwa na kufanya kosa lingiine, Ni pale viongozi wa CHADEMA wanapotamka maneno ya kiingereza; “ People’s…. Power! Huku wakiamrisha wafuasi wao kusokota ngumi . Kitendo hicho kinatoa ishara mbaya kwa mpiga kura wa kawaida. Bado kuna Watanzania wengi waliopokea maelekezo ya tangu enzi za Mwalimu kuwa; “ Tujiadhari na wanaotaka kutusababishia vita na mapigano katika nchi.” Kukunja ngumi ni ishara ya kujiandaa kupigana. Kuna kura zinazokimbia kutoka CHADEMA kwa ngumi hizo.
CUF: CHAMA CHA WANANCHI
Katika hali ya kushangaza, CUF ( Bara) safari hii kinaonekana zaidi kuwa ‘ jokeli’ katika karata za kisiasa. Profesa Ibrahim Lipumba bado anaonekana kuwa na nguvu katika kanda ya pwani na mikoa ya kusini. Lakini nguvu hizo haziwezi kulinganishwa na za katika uchaguzi mkuu uliopita. Kuna wakati, CUF wanaonekana kuwa zaidi ‘ Chama Rafiki’ na CCM kuliko chama cha upinzani. Na laiti ‘ urafiki’ huo wa kisiasa ungekuwa kati ya Profesa Lipumba na Dr Slaa, basi, mgombea Urais wa CCM angekuwa na kibarua kigumu zaidi, lakini si kwa sasa, siku 48 kabla ya Oktoba 31. Ninapoandika fikra hizi huru.
Maggid
Iringa
Jumapili, Septemba 12, 2010.
mjengwa

Hivi wana-CCM wakisema kidumu chama cha mapinduzi, ule mkono wanarusha juu uwa sio ngumi?! Source yako ni nipashe tu na sample ndogo sana ya wabunge 10, na madiwani 100!! Jaribu kuonana/ kuwasiliana na Synovate na Redet ili kupata upepo kwani Synovate ufanya utafiti huu kila kota na hii ni kota ya tatu!!
 
Nimempigia Slaa, na nime mu endorse watu wampigie kura kwenye uchaguzi kuongeza competition Tanzania upinzani uongeze asilimia ya kura gradually, lakini nakubali Slaa hawezi kushinda urais. Wala CHADEMA haiwezi kupata majority ya wabunge.

Kiranga acha uongo, Mungu anakuona. Wenzio wameanguka kwa ajili ya uongo!!!
 
sisomi blog lako tena. Sisi tunaenda mbele wewe jamaa unaturudisha nyuma. Kama umetumwa si unayo blog?? Andika kule .
 
CCM kushindwa uchaguzi on the ground ni sawa na CHADEMA kushindwa hii poll ya JF.

twende mbele turudi nyuma huu ndio ukweli japokuwa wengi wetu tunatamani sana CCM ianguke lakini kwa vile wao ndio wameshika serikali ndio maaana tunaona jinsi wanavyotumia kila mbinu kuhakikisha wanashinda uchaguzi.
 
sisomi blog lako tena. Sisi tunaenda mbele wewe jamaa unaturudisha nyuma. Kama umetumwa si unayo blog?? Andika kule .

Mkulu Abiziani, hebu onesha ustahimilivu na ukomavu wa kimtizamo basi. Hizi sasa si hasira za mkisi hizi...! Kutosoma blog yake au kutotembelea hakutonizuia mimi, mwingine au yeye kufikisha mawaidha yake hapa JF, maana kuna baadhi bado wataweza ku-copy alichoandika na kukiweka hapa na utaishia kukisoma!! Tukubali kutokubaliana!
 
Maggid

huo utafiti wako sample gani na ukubwa wake, methodology ipi,. umesahau wanavijiji wa sasa ni tofauti na wa zamani kuna shule za kata pamoja ni bomu lakini zimewafumbua macho vijijini kiidogo, wanajua shida ni nini, wanajua EPA ni nini, wanajua mafisadi ni akina nani, wanajua wakichagua chadema mfuko wa cement watanunua 5,000. nk. ombi langu ukafanye hiyo research yako upya. usi conclude kwa kumsikiliza makamba na kinana
 
Mkuu Maggid,
Duh anona hapo mzee umegusa sio. Mimi ningekushauri kitu kimoja kwenda na wakati wakati unafanya chambuzi zako au Tafiti zako, Halafu conclusion zako ziwe na vision na sio mazoea kama nilivyo ona ulichofanya Maggid.

Sioni wala sishangai jinsi watu wanavyo kushambulia kwa kuwa we are tired, we need CHANGE, sasa wewe naona unafagilia hizi ahadi toka tumeanza vyama vingi kwa mara ya pili kupitia uchaguzi wa 1995.
Angalia katika nchi yeyote ile hata wakati ule wa campaign za akina Obama, walikuwa wanajalibu kusisitisa kuwa mabadilko ni muhimu sana kufanyika ili nchi iweze kupiga hatua.
Ila kwetu tafsiri ya MABADILIKO ni mwisho wa Dunia au umwagaji damu utaanza. Sasa hii ni siasa au UPUUZII?

Jaribu kuangalia au kufanya tafiti kati ya viongozi wote waliopita au changuzi zote zilizo pita kitu kikubwa kwa CCM ni kujaza ma billboards kwote ili mradi hata yule asiye jua afanye nini ataweza kweli kukipa CCM Kura, Je sasa hivi yupo tayari kutoa kura yake kwa kuwa kuna mabillboard mji mzima?

We need change either to give Chadema or CUF chances to save Poor Tanzanian.

Pia huku vijijini wewe Maggid ungekuwa mstari wa mbele kuwaambia wananchi hao kuwa fanyeni MABADILIKO. na sio kuzipokea ahadi wakati wa campaign.

KUMBUKA JK ndiyo awamu yake ya mwisho hakuna atakaye kuja muuliza uliahidi hiki na kile mbona hujatimiza? Atakaye kuja ataahidi yake mwishowe hakuna kitakacho fanyika na mwisho wake ni umaskini mpaka tunapoteza hiki kizazi cha dot com.

Kiukweli WATANZANIA WAMECHOSHWA SANA NA UTAWALA WA JF.

Jamani tujaribu kuwapa elimu watu wetu huko mataani hawajui lolote wanaishia kupewa hizo elfu tano kwenda kwenye mikutano ya CCM tu nasi tuna furahi kweli tumejaza watu pale haijawahi kutokea.

Nawasilisha.

'WE NEED CHANGES'
 
Mkuu Maggid, pamoja na uelewa wako wa mambo ya chaguzi zinavyokwenda na tathmini yako 'nzuri' tunaomba utufanyie katathmini kengine juu ya madhara ya kauli za Dr. Sheikh Yahaya kwa mgombea wa urais wa CCM. Hatuombi mabaya, lakini je tatizo la afya ya Rais linawezaje kuathiri matokeo ya uchaguzi huu na uongozi endapo mgombea huyo wa CCM atafanikiwa kupita?
 
Mkuu Maggid,
Kiukweli WATANZANIA WAMECHOSHWA SANA NA UTAWALA WA JF. '

Mkuu nadhani ulitaka kusema JK na sio JF.. au siyo?
Kuhusu bandiko la Maggid, mimi binafsi nina maswali mengi kuliko majibu na hoja zake. Pamoja na kuwa amejaribu kuwa sincere na kwa ufupi kuzungumzia vyama vyote, lakini bado ameshindwa kabisa kuthibitisha hiyo dhana yake ya kwamba uchaguzi ukifanyika leo Kikwete atashinda na kufuatiwa na Dr Slaa na kisha Prof Lipumba. Kwahiyo ninaweza kusema kwa usahihi kabisa kuwa aliyoandika ni mabunio yake kutoka kichwani na au moyoni mwake tu...
Mtazamo wake una kinzana sana na hali iliyokuwa imeanza kujijenga. CCM ilianza kupoteza umaarufu wake tangu mwaka 1999, na hali hiyo haikuwahi kusimama au kurudi nyuma, bali imekuwa ikiendelea na hivi karibuni hali imekuwa mbaya zaidi. Sababu zifuatazo zimepelekea hali hiyo:
(1) Kifo cha baba wa taifa. Kwenye uchaguzi wa raisi wa mwaka 1995, ndugu Augustine Lyatonga Mrema aliwasha moto uliokitikisa chama cha CCM na mgombea wake Benjamin William Mkapa. Mzee Nyerere alikuwa bado hai na ndiye aliyesimama na kumpigia kampeini Mr Clean na kulizima moto wa Mrema. Leo yule mzee hayupo tena! Je ni nani atasimama na kuzima moto mpya wa Dr Slaa? Udhaifu mkubwa wa CCM unaanzia hapo... kukosekana kwa mtu mwenye ushawishi kutoka CCM.

(2) UDHAIFU NDANI YA CHAMA. CCM sasa hivi sio siri ni chama dhaifu. Kwa mara ya kwanza chama kilionesha udhaifu mkubwa uliopelekea mvurugano na mfarakano ndani ya chama na baadhi ya viongozi waandamizi kutukanana na kutuhumiana waziwazi. Hali hiyo ilifuatiwa na kukimbiwa na baadhi ya ya makada wake (ref Pendazoe) ambao ni muhimu na wengine waliobaki humo ni kwasababu ya kukosa ujasiri wa kujitoa lakini wapo kimia hawafurahishwi na mambo mengi ya chama. Sababu za matatizo hayo ni 1. MTANDAO 2. UFISADI

(3) RICHMOND. Mojawapo ya uthibitisho wa UFISADI ni Richmond. Kashfa ya uwekezaji wa Richmond ilipelekea serikali kuvunjwa na waziri mkuu kujiuzuru. Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania liligawanyika kwa sababu ya Richmond. Kashfa hiyo haikuwa ndogo na habari zake hazikukomea Dar es Salaam na Dododma tu, bali zilisambaa na kuwafikia wananchi wote na nje ya nchi. Wananchi wengi hawana imani na Rais na CCM kama inasimama kwa ajiri ya maslahi ya nchi.

(4) ARDHI na MIGODI. UFISADI wa ardhi imekuwa kero kubwa kwa wananchi wengi huko vijijini. Huko Arusha ardhi ilitaka kuchukuliwa kwa ujanja na wananchi walicharuka na kuamua kuhami ardhi yao kwa kutumia siraha za jadi. Vijana wenye nguvu walihamia porini wakingoja yeyeote atayekuja kugawa ardhi yao wapambane naye. Hata huko Dodoma juzi wananchi wa huko walilalamika sehemu kubwa ya ardhi yao kuchukuliwa na waziri mkuu mstaafu, bwana Sumaye. Huko Tanga wanakijiji wanalalamika pia kuwa Rais mstaafu (BW Mkapa) amejitwalia sehemu kubwa ya ardhi na amekuwa akiwatumikisha kwa ujira kidogo. Vilevile, mgodi wa Kiwira huko Mbeya ulichukuliwa kifisadi na Bunge likapiga kelele hadi mwekezaji akautema na ukarudishwa serikalini. Kigamoboni wananchi wanatarajia kuhamishwa kutoka kwenye makazi yao kupisha ujenzi wa makazi mapya ambapo mtu/watu wengine watakuja kuishi pale...orodha ni ndefu. Yote haya hayawezi kuwaacha wananchi masikini wakikenua meno kwa furaha na kuendelea kuimba zidumu fikra sahihi za Kikwete...

(5) WAFANYAKAZI. Mfarakano wa Rais Kikwete na wafanyakazi wa serikali, mashirika ya umma na sekta binafsi, ni tatizo jingine ambalo Rais ameshindwa kabisa kulimaliza na kurejesha maelewano mazuri. Hivi sasa wafanyakazi wanamngoja kumwadhibu kwenye sanduku la kura, na hata kama uchaguzi ungefanyika leo Kikwete asingeweza kupata kura za wafanyakazi zaidi ya 5 - 10%.

(6) UVUMILIVU UMETOWEKA. Sasa ni wazi wa-Tz wengi wameanza kukata tamaa na viongozi wa nchi yetu. Kwa mara ya kwanza katika nchi hii tumeweza kuona raisi akipopolewa kwa mawe na wananchi wenye hasira(vijijini) huko Mbeya. Kitu hiki ni kipya katika nchi yetu. Je hii ina maana gani? Je dalili ya wananchi kuchoshwa na ahadi za uongo za watawala na chama cha ccm? ..hii ni wazi kuwa wananchi wamechoka sasa na hawapo tayari kuendelea kudanganywa na ahadi nono za watawala.

(7) DHURUMA ktk UWEKEZAJI. Chanzo kingine cha kero ni uwekezaji unaofanyika hapa nchini. Uwekejai huo umekuwa ukiambatana na dhuruma kwa wananchi wanaoishi karibu na maeneo ya uwekezaji. Mfano mgodi wa Bozwagi, wananchi hawakulipwa vizuri pesa zao pamoja na ukweli kwamba waliondolewa kwa nguvu ktk maeneo yao ili kupisha mwekezaji. Hii inaonesha kuwa wawekezaji wamekuwa wakithaminiwa zaidi kuliko wananchi kwa maslahi ambayo hayaonekani kwao..mgogoro wa Bzwagi uliendelea kwa muda mrefu na sikumbuki kama ulihitimishwa vyema. Kule Mara kuna mwekezaji katika machimbo ya dhahabu Buhemba, bado kuna matatizo na watu wameendelea kulalamika. Sumu ya kuoshea dhahabu imekuwa ikimwagwa kwenye mto wa maji wanayotumia binadamu, na watu wamedhurika lakini serikali imeshindwa kumdhibiti mwekezaji. Imefikia hatua watu wanapigwa risasi na kujeruhiwa au kufa na serikali imekuwa ikiota matende kuchukua hatua kulinda raia. Haya yamewakera sana wananchi na sidhani kama ni wajinga kiasi hawatachukua hatua zozote kwenye box la kura 2010

(8) UGONJWA wa RAIS. Rais ni binadamu kama sisi na hivi yeye pia huugua. Hata marais waliomtangulia walikuwa wakiugua. Lakini tofauti kubwa ni ugonjwa wa kuanguka unaomkabiri Dr Kikwete. Huu ni ugonjwa mpya kwa rais .. ni tatizo ambalo haliwezi kupuuzwa. Ni tatizo ambalo lina wasikitisha na kuwaogofya wananchi. Tatizo hili lina tafsiri tofauti tofauti kutoka sehemu moja hadi nyingine, lakini tafsiri hizo sio nzuri. Mtu akisema kuwa Kikwete ana kifafa! Anaanguka kifafa.. inaogofy na kuondoa imani ya watu anaowaongoza. Ugonjwa huo unaogopewa na unachukuliwa ni ugonjwa mbaya ambapo mgonjwa wa kifafa hata hawezi kuchumbia au kuaminiwa kuongoza watu katika jamii mbalimbali za Tz. Watu wanaweza kuwa wanakwenda kwenye mikutano ya Kikwete kumwangalia kama mgonjwa na siyo kuonesha mapenzi yao kwake.

(9) NGUVU YA HOJA. Ukilinganisha uwezo wa Dr Kikwete (samahani wengi hawapendi, lkn ndio ukweli kuwa alishazawadiwa) na Dr Slaa kuna tofautoi kubwa. Tofauti hii inaendelea kujidhirisha zaidi kadiri kampeini zinavoendelea kuelekea uchaguzi mkuu. Sera za Dr Slaa zina nguvu ya hoja, zinatia matumaini na zinatekelezeka ukilinganisha na zile za Dr Kikwete ambazo nyingi ni ahadi ambazo kwakweli ni kubwa kuliko ukweli. Dr Kikwete hawezi kujenga hoja zenye mantiki ili aweze kushindana na Dr Slaa.
Kwa sababu hizo tisa nina mashaka kama Dr Kikwete anaweza kushinda tena katika uchaguzi, hata kama kura ingepigwa leo. Na kadiri muda unavokwenda na Dr Slaa anavyozidi kuzungukia watu na kuuza sera zake kwa wapiga kura ndio hali ya CCM inavozidi kudidimia chini zaidi. Huenda ni sahihi kuanza kusahau habari ya Kikwete kuwa raisi wa Tanzania kama uchaguzi utakuwa fair. Na mimi hayo ni mawazo yangu tu nipo tayari kukosolewa.

 
Mkuu Majid.M.
Mimi nakuheshimu sana lakini kitendo chako cha kukurupuka huko na kuanza kuwaza tu kua JK atashinda siwezi kukubaliana nacho manake huna details za kutosha,na wewe kabisa unajua kuwa wananchi wamechoshwa na serikali ya JK now watu wanataka wabadiliko na Slaa ndio kimbilio la wengi.kinachotakiwa sasa hivi ni kuendelea kuwaelimisha wenzetu watanzania ambao wanaridhika na ma tshirt na kofia za CCM ili waweze kuelewa haki yao na part gani wanatakiwa waplay for now.we fikiria mwenyewe mwananchi wa kijijini kapewa kofia then anakuja kusafa for 5 years huku mtu(fisadi) alieiba hela anaambiwa azirudushe tu then anasehewa. Wewe tena unakuja na mawazo yako unasema huyu JK atarudi tena, nani atamrudisha?? Kama umetumwa tuambie watu tushajichokea tunataka mabadiliko na Slaa ndie atashinda regardless uchaguzi utafanyika lini.

Nashangaa wewe na majina yako ya bandia na sishangai ukawa upo ulaya au amerika kask unabeba mabox na hata hiyo kura hutaipiga (labda hapa jf) lakini unabishana na Majjid ambaye kila siku yupo field anakula vumbi na wabombea. Tunajua kuwa ni ukereketwa na mapenzi yako kwa chama yanayokusukuma lakini ukweli unabaki palepale. kumbuka mpaka sasa hivi CCM wana vipi 10 vya wabunge na karibia mamia ya madiwani, upinzani hawana hata kimoja. Hebu jitokeze na ujiweke wazi kuwa wewe ni nani na upo wapi. otherwise keep quite na si kuleta porojo hapa na punguza jazba.
 
Maggid,

Ndio maana watu wengi wanaogopa kuandika mawazo yao hapa JF ambayo yanapingana na baadhi ya mitazamo. JF siku hizi ina Banyamurenge wengi kweli, hawakawiii kurusha ngumi.

Tusubiri Novemba mosi kujua ukweli wote.
 
Nashangaa wewe na majina yako ya bandia na sishangai ukawa upo ulaya au amerika kask unabeba mabox na hata hiyo kura hutaipiga (labda hapa jf) lakini unabishana na Majjid ambaye kila siku yupo field anakula vumbi na wabombea. Tunajua kuwa ni ukereketwa na mapenzi yako kwa chama yanayokusukuma lakini ukweli unabaki palepale. kumbuka mpaka sasa hivi CCM wana vipi 10 vya wabunge na karibia mamia ya madiwani, upinzani hawana hata kimoja. Hebu jitokeze na ujiweke wazi kuwa wewe ni nani na upo wapi. otherwise keep quite na si kuleta porojo hapa na punguza jazba.
mkuu ngwendu.nadhani hata wewe hili sio jina lako kamili na mimi sijaleta jazba hapa najaribu kumuweka sawa huyu kijana wetu,kuhusu uhalisia wangu mimi sasa hivi nimejiajiri na nipo Tanzania na nimejiandikisha na kura yangu itaenda kwa Rais mteule wa watanzania DR Slaa na mbunge wetu J.Mnyika. Sasa nina mashaka na wewe kama unnataka mabadiliko aua unataka nchi yetu iendelee kuhujumiwa.thanks.
 
Baija Bolobi,
Yawezekana wewe ukawa ni ama Msukuma au Mnyamwezi ( Ni watani zangu hao). Kama si hivyo, umefafana nao kidogo kitabia. Hivi si wewe uliyeandika kuwa una hakika kuwa ukipitia archives ungekutana na makala yenye kufanana na niliyopost hapo juu. Na uungwana umekushinda. Nifanyeje? Mimi sitaendelea kulumbana nawe. Vinginevyo uje na jipya.
===========

Ndugu yangu Maggid
Kwa bahati mbaya sikuwahi kujibu hoja yako hapo juu na baada ya kurudi nimekuta wengi wamekujibu. Kipekee nampongeza sana MLALAHOI (Bandiko namba 21) kwa kumkoma nyani. Maggid akitaka kudanganya au kuonyezi mapenzi yake kwa CCM huwa anaanza kwa kudai "haya ni mawazi huru yasiyo na itikadi ndani yake", lakini kimsingi, hata Makao Makuu ndogo ya Lumumba kuna watu wanakumind kuwa unanyemelea nafasi zao kwa jinsi unavyojiweka karibu sana na Kikwete. Ukitaka ukweli wa CCM, huwezi kuupata katika vijiwe kwa sababu huko ni sisi tunaomwaga uwongo wa kuwafanya watu wasinzie. Ukweli umo humu ndani, tunamolazimishwa kukabidhi simu wakati wa vikao na kusaini viapo tusivyoviamini. Tunajua kuwa chama chetu hakipendwi, lakini hakuna hata mtu mmoja kwa sasa mwenye uwezo wa kuaminika ndani ya CCM na mbele ya wananchi.

Ndugu yangu Maggid, sie wenzio tunaenda vijijini kama wewe. Na wala usijidanganye kuwa watu wa vijijini bado ni wale wale wa 2005. Hivi sasa mradi mkubwa wa ulaji tulio nao ni kuhakikisha kila mmoja anadai hali ni mbaya ili tupate fedha za kwenda kuhonga.

Ebu angalia majimbo ambayo wabunge wetu wamepita bila kupingwa - maofisa wetu wanalia kwa kukosa ulaji. Hata rufaa zilizotupwa na TUME, wengi wa maofisa wetu wameasi chama na kusaidia ili wapinzani warudi kusudi maofisa wapate ulaji maana kwa kweli uchaguzi ni mwaka wa mavuno kwa maofisa wetu.

Nimalize kwa kukupongeza kuendelea kuwa mwaminifu kwa JK (siyo kwa CCM), lakini angalia ndugu yangu, anakuja na timu mpya, na usishangae ahadi unayosubiri hutaiona.
 
acha woga,we unamuogopa majig kwa vile ana blog? Jk hatoki mwaka huu pamoja na kampeni zao chafu,wewe unafikiri hata Slaa akishinda atashinda na %100? Mimi namfananisha na yule miss aliyeulizwa swali. Propaganda zake za kushinda kwa JK ni sumu kwa watu ambao washaanza kufumbuka macho hapa mkulu harudi magogoni nia harudi. Full stop. Chadema ni chama ambacho kipo tayari kuongoza nchi na hakikurupuki.

Mimi nashindwa kuelewa kwanini baadhi yetu sisi wachangiaji tunashindwa kumuelewa maggid. Ni vema sisi wachangiaji tuwe tunaheshimiana kwa kuchangia kwa hoja na kuacha ubishi usio na maana wala tija kwa nchi yetu. Maggid ametoa mawazo yake ni vema tuyaheshimu. Ameelezea hali halisi inayoiona kwa sasa. Sasa kilichobaki kwetu wachangiaji ni kukubaliana au kutokubaliana naye kwa hoja. Kuandika kuwa Jk hatoki mwaka huu pasipo kueleza kwanini atatoka ni kupotosha maana ya mjadala. Baadhi yetu tunapenda kuweka mbele mapenzi na matakwa yetu kuliko uhalisia wa masuala yenyewe yaliyopo. Kwa kuwa hatuipendi CCM na JK wake tunataka tuifanye hii dhana hii kuwa ndio ukweli. Kwa mtaji huu hatuwezi kupiga hatua katika kuleta mabadiliko. Ikiwa mtu unataka ushindi ni lazima umheshimu mpinzani wako na umuelewe udhaifu wake na wewe mwenyewe ujipange namna utakavyoweza kupambana. CCM ni imara vijijini hilo halina ubishi na huko ndiko watakakopata kura nyingi. Kwamba CCM watapata kura nyingi vijijini haina maana kuwa CCM inapendwa sana vijijini. Ukweli ni kuwa huko vijijini wengi wa watanzania wenzetu wanadhani kuwa CCM ni kila kitu na wanaiona CCM kuwa ni NYERERE na wanashangaa kuona kuwa kuna baadhi wanataka kupambana na NYERERE. Kwa hiyo hapa ni suala la uelewa na kampeni kuwaelewesha wananchi hasa huko vijijini.

Ni lazima upinzani ujipange kwelikweli huko vijijini ndipo uote ndoto ya kuiangusha CCM. Katika mpambano huu wa sasa kuelekea uchaguzi mkuu mimi nauona sawa na askari 1000 wakiwa na bunduki za SMG na helmet wakiwa wamejipanga (pamoja na kupiga kelele kuwa leo tunashinda) wakikabiliana jeshi lenye askari 1000 lakini likiwa na zana imara vikiwemo vifaru, ndege za kivita, makombora na kadhalika. Je, vile viaskari 1000 vingine vye bunduki za SMG na vilivyovaa helmet (huku vikijitapa kuwa leo tunashinda) ni kweli vitashinda dhidi ya askari wengine 1000 wenye tanks na ndege za kivita? For Sure that will be fools' courage.
 
Back
Top Bottom