Kama Uchaguzi Mkuu Ungefanyika Leo...

maggid

JF-Expert Member
Dec 3, 2006
1,084
1,246
Jumapili, Septemba 12, 2010.

Na Maggid Mjengwa,


HUU ni mjadala niliouanzisha kule kwenye jukwaa la Jamii (www.jamiiforums.com). Nauendeleza hapa ili uwafikie wengi zaidi.
Ni tathimini yangu. Ni mtazamo wangu huru. Katika kuishi kwangu kuna chaguzi nilizozishuhudia kwa macho na nilizosoma vitabuni. Hivyo, ninachoandika kinatokana na uzoefu wangu wa kufuatilia kwa karibu mienendo ya chaguzi zetu.
Naam. Zikiwa zimebaki siku 45( Leo Jumatano, Septemba 15, 2010) naiona hali ifuatayo kama uchaguzi ungefanyika hii leo;

Mgombea Urais wa Chama Cha Mapinduzi, Jakaya Mrisho Kikwete angeibuka mshindi . Dk Wilbroad Slaa ( CHADEMA) angechukua nafasi ya pili na huku Profesa Ibrahim Lipumba ( CUF) akishika nafasi ya tatu. Wagombea wa vyama vilivyobaki wangekuwa wasindikizaji kwa kupata chini ya asilimia 5 ya kura zote kwa pamoja.

Hali hiyo ingeakisi pia matokeo ya uchaguzi wa wabunge na madiwani ( Bara). Tafsiri yake; Jakaya Mrisho Kikwete angeunda Serikali huku yeye na chama chake wakikabiliwa na changamoto kubwa kutokana na upinzani utakaokuwa umeongezeka nguvu ndani na nje ya bunge kutokana na ujio wa Dk Slaa kama mgombea Urais katika uchaguzi wa mwaka huu.
Ni dhahiri kuwa Chama Cha Mapinduzi baada ya Oktoba 31, kinatakiwa kijipange upya kuikabili hali mpya katika uwanja wa kisiasa. Viashiria vya jamii inayotaka mabadiliko vimeshaonekana. CCM itakuwa na mawili ya kuchagua; kuchukua jukumu la kuyaongoza mabadiliko hayo au kusubiri kuzamishwa na mkondo wa maji ya mabadiliko hayo.
CCM ianze sasa kufikiria namna itakavyounda Serikali miaka ijayo kwa kushirikiana na vyama vingine. Ifikirie pia uwezekano wa kuwapo Serikali ya Mseto hata Tanzania bara. Ndio, kutoa fursa kwa chama au vyama pinzani vitakavyokuwa na idadi kubwa ya wabunge kushiriki kuunda serikali ya Umoja wa Kitaifa.

Na hakika miaka mitano mpaka kumi ijayo, tutakuwa na Tanzania tofauti na ya sasa. Na mtaziona ishara. Kauli za ' Kidumu Chama Cha Mapinduzi! Na CCM Daima! Zitaonekana na wapiga kura kuwa ni za waliopitwa na wakati. Hiki ni kizazi kipya na dunia imebadilika.
Kwa hali ilivyo kwa sasa, CCM wanajivunia:

Kuwa ni chama kikongwe, kikubwa na kilichotawala kwa muda mrefu. Kuna hata wanaokipigia kura chama hicho ' Kwa mazoea tu'. Na katika nchi zetu hizi; kukiondoa chama kilicho madarakani, Chama kilichopigania uhuru au kinachotokana na chama kilichopigania uhuru ni kazi ngumu sana. Kwa anayetaka kufanikiwa katika hilo, anahitaji kwenda ilipo mizizi ya chama hicho. Ni vijijini. Na huko vijijini kwa leo hii chama wanachokijua ni CCM. Naam. Ndio ' Zimwi' wanalolijua.
Mwanakijiji atatembea kwa miguu kilomita kumi kwenda kuhudhuria mkutano wa CCM. Atakwambia amepewa taarifa ya mkutano na Balozi wake wa Nyumba Kumi. Hivyo basi, CCM wanajivunia mtandao wao wa kichama kuanzia ngazi ya Balozi wa Nyumba Kumi, shina, tawi na kuendelea. Na hata mtandao wa Kiserikali.
Na hakika, mara zote ni vema na ni busara kusema yaliyo kweli na tunayoyaamini, hata kama ukweli mwingine unahuzunisha, ni vema ukasemwa. Kuufumbia macho ni sawa na kuogelea kwenye mapovu wakati maji yapo.

Udhaifu wa CCM:
Pamoja na kuwa ni chama kikongwe na chenye uzoefu, wakati mwingine inashangaza kuona katika maeneo kadhaa kinavyoshindwa kusoma alama za nyakati. Kura za maoni ni mfano wa udhaifu wa CCM kushindwa kubaini kuwa kwa utaratibu mpya ulijiojiwekea katika kupata wagombea walisahau umuhimu wa kuyapitia na kuyachuja majina ya wanachama wake waliotangaza nia ya kugombea na kuchukua fomu kabla ya kuyapeleka kwa wanachama wake kupigiwa kura za maoni.
Badala yake, CCM iliacha wanachama waamue halafu bado chama nacho kikaingilia kati kuamua tena. Kuna adhabu ya chama kutoka kwa wanachama wake inakuja kutoka katika baadhi ya majimbo. Kwa utaratibu uliotumika sasa, wanachama wa CCM huko tuendako wanaweza kujikuta wakiwapigia kura za maoni wagombea wenye fedha chafu zinazotokana na shughuli haramu. Na kinachojitokeza zaidi sasa ni kubadilika kwa mwenendo wa wapiga kura. Kidogo kidogo wapiga kura wameanza kuangalia zaidi watu na si chama. Ni kwenye ngazi ya udiwani na ubunge. Hizi ni dalili mpya za kubadilika kwa mwenendo wa wapiga kura. Kwamba mtu kwanza, ilani ya chama baadae.

CHADEMA: Ujio wa Dk Slaa:
Sio tu umewashangaza CCM na mgombea wake urais, bali pia unaonekana kuwashangaza CHADEMA wenyewe wanaoonekana kutokujiandaa na namna Dk Slaa alivyopokewa na wananchi. Na kama ilivyotabiriwa na Mwalimu, CHADEMA inaonekana kuwa ndio chama cha upinzani chenye nguvu na chenye nafasi ya kuipoka CCM mamlaka ya kuongoza dola endapo CCM kama chama haitafanya juhudi za makusudi za kufanya mabadiliko ya kimsingi yatakayoonekana na wapiga kura.

Udhaifu wa CHADEMA
Unajidhihirisha kwenye eneo la oganaizesheni na kifedha. Bado CHADEMA haina uwakilishi mpana katika ngazi za mashina na matawi. Dk Slaa anaweza kutua na helikopta Pawaga, Iringa. Lakini, mara ile akiruka, huku nyuma hakuna watendaji wa CHADEMA wa kufanya kazi ya CHADEMA. Kuna taarifa pia za wagombea wake ubunge na udiwani wa CHADEMA kukosa nguvu za kifedha kuendesha kampeni . Taarifa hizo zilizoripotiwa kwenye vyombo vya habari haziwezi kupuuzwa tu. Hapa inahusu udhaifu katika maandalizi. Kuna wagombea wa CHADEMA watakaoanguka katika chaguzi kwa tatizo hilo.

Zitto Kabwe:
Huyu ni kada nyota ndani ya CHADEMA. Hata hivyo, ‘sarakasi' zake za kisiasa huenda zinachangia kukidhohofisha chama chake kuliko kukipa nguvu. Majuzi hapa aliripotiwa na magazeti kutamka hadharani kuwa anajiandaa kugombea urais 2015. Zitto Kabwe anaacha maswali; Kulikoni ndani ya CHADEMA? Je, Dk Slaa ni mgombea wa ‘msimu' tu? Au ndio sababu Zitto Kabwe hakuhudhuria Mkutano wa ufunguzi wa kampeni za CHADEMA pale viwanja vya Jangwani?

Inachojivunia CHADEMA:
Bado ni chama kinachoonyesha kuwa na mvuto kama kitajipanga vema. Kesi iliyofunguliwa Mahakamani dhidi ya Dk Slaa kuhusiana na masuala binafsi ya mahusiano inaonyesha kumtangaza na kujenga zaidi Dk Slaa kwa wapiga kura wanaotia shaka wakati uliotumiwa kuibuliwa kwa suala hilo. Kuna watakaompigia Dk Slaa ' Kura za Kumhurumia'.

Umakini wa CHADEMA:

CHADEMA imekuwa ikijinadi kama chama makini machoni mwa wapiga kura. Hata hivyo, taarifa zilizoripotiwa kuwa Naibu Katibu Mkuu , CHADEMA, Zanzibar Hamad Yussuf huenda akaondolewa kwenye timu ya kampeni ya Dk Slaa kwa kuwa amekuwa kero inaonyesha namna timu ya kampeni ya CHADEMA ilivyoshindwa kubaini mapema, Hamad Yussuf alikuwa kero kwa wapiga kura. Maana, kwa utamaduni wa Watanzania, namna Naibu yule Katibu Mkuu alivyokuwa akimfananisha Dk Slaa na Bwana harusi na kauli nyingine pale viwanja vya Jangwani ilikuwa ni ' matusi' hata kama kuna waliotaka kupewa tafsiri sahihi ya neno hilo. Ni heri kwa CHADEMA wameamka na kubaini kero hiyo ndani ya nyumba yao.

Kauli na Ishara:

Kama hakuna aliyelifikiria hili ndani ya CHADEMA, basi, hata kama CCM wanaimba ' Wapinzani tuwalete , tuwakatekate' , hilo ni kosa ambalo halipaswi kujibiwa na kufanya kosa lingine, Ni pale viongozi wa CHADEMA wanapotamka maneno ya Kiingereza; " People's…. Power! Huku wakiamrisha wafuasi wao kusokota ngumi . Kitendo hicho kinatoa ishara mbaya kwa mpiga kura wa kawaida. Bado kuna Watanzania wengi waliopokea maelekezo ya tangu enzi za Mwalimu kuwa; "Tujiadhari na wanaotaka kutusababishia vita na mapigano katika nchi." Kukunja ngumi ni ishara ya kujiandaa kupigana. Kuna kura zinazokimbia kutoka CHADEMA kwa ngumi hizo.

CUF: Chama cha Wananchi
Katika hali ya kushangaza, CUF ( Bara) safari hii kinaonekana zaidi kuwa ' jokeli' katika karata za kisiasa. Profesa Ibrahim Lipumba bado anaonekana kuwa na nguvu katika kanda ya Pwani na mikoa ya kusini. Lakini, nguvu hizo haziwezi kulinganishwa na za katika uchaguzi mkuu uliopita. Profesa Lipumba aliyeanza kuwania Urais tangu 1995 sasa anaonekana zaidi kuwa ni mtu anayepita ' kuwaaga' Watanzania kuliko kuomba kura zao.
Na kuna wakati, CUF wanaonekana kama ' Chama Rafiki' na CCM kuliko chama cha upinzani. Na laiti ' urafiki' huo wa kisiasa ungekuwa kati ya Profesa Lipumba na Dk Slaa, basi, mgombea Urais wa CCM angekuwa na kibarua kigumu zaidi, lakini si kwa sasa, siku 45 kabla ya Oktoba 31. Ninapoandika fikra hizi huru. Urafiki huo wa CCM na CUF unaweza pia kumgharimu mgombea wa CCM, Rais Kikwete na kujikuta akigawana kura na Profesa Lipumba na si kura za upinzani kugawanywa. Hilo linaweza kutokea na kuwashitua CCM.


CHANZO: Raia Mwema
========================================================
NAANDIKA haya kutokana na uzoefu wangu wa kufuatilia kwa karibu mienendo ya chaguzi zetu. Kwa chaguzi nilizozishuhudia kwa macho na nilizosoma vitabuni. Naam. Zikiwa zimebaki siku 48 ( Leo Jumapili, Septemba 12, 2010) naiona hali ifuatayo kama uchaguzi ungefanyika leo hii;
Mgombea Urais wa Chama Cha Mapinduzi, Jakaya Mrisho Kikwete angeibuka mshindi . Dr Wilbroad Slaa ( CHADEMA) angechukua nafasi ya pili na huku Profesa Ibrahim Lipumba ( CUF) akishika nafasi ya tatu. Wagombea wa vyama vilivyobaki wangekuwa wasindikizaji kwa kupata chini ya asilimia 5 ya kura zote kwa pamoja.
Hali hiyo ingeakisi pia matokeo ya uchaguzi wa wabunge na madiwani ( Bara). Tafsiri yake; Jakaya Mrisho Kikwete angeunda Serikali huku yeye na chama chake wakikabiliwa na changamoto kubwa kutokana na upinzani utakaokuwa umeongezeka nguvu ndani na nje ya bunge kutokana na ujio wa Dr Slaa kama mgombea Urais katika uchaguzi wa mwaka huu.
CCM wanajivunia:
Kuwa ni chama kikongwe, kikubwa na kilichotawala kwa muda mrefu. Kuna hata wanaokipigia kura chama hicho ' Kwa mazoea tu'. Na katika nchi zetu hizi; kukiondoa chama kilicho madarakani, Chama kilichopigania uhuru au kinachotokana na chama kilichopigania uhuru ni kazi ngumu sana. Kwa anayetaka kufanikiwa katika hilo, anahitaji kwenda ilipo mizizi ya chama hicho. Ni vijijini. Na huko vijijini kwa leo hii chama wanachokijua ni CCM. Naam. Ndio ' Zimwi' wanalolijua. Mwanakijiji atatembea kwa miguu kilomita kumi kwenda kuhudhuria mkutano wa CCM. Atakwambia amepewa taarifa ya mkutano na Mjumbe wake wa nyumba kumi. Hivyo basi, CCM wanajivunia mtandao wao wa kichama kuanzia ngazi ya Balozi wa Nyumba Kumi, shina, tawi na kuendelea. Na tayari CCM ina wabunge kumi waliopita bila kupingwa na madiwani zaidi ya 100 kwa mujibu wa gazeti la NIPASHE la leo Jumapili.
Udhaifu wa CCM:
Pamoja na kuwa ni chama kikongwe na chenye uzoefu, wakati mwingine inashangaza kuona katika maeneo kadhaa kinavyoshindwa kusoma alama za nyakati. Kura za maoni ni mfano wa udhaifu wa CCM kushindwa kubaini kuwa kwa utaratibu mpya ulijiojiwekea katika kupata wagombea walisahau umuhimu wa kuchuja majina ya wagombea kwanza ili kubaini wale ambao wangewaletea shida. Badala yake, waliacha wanachama waamue halafu bado chama nacho kikaingilia kati kuamua tena. Kuna adhabu ya chama kutoka kwa wanachama wake inakuja kutoka katika baadhi ya majimbo. Na kinachojitokeza zaidi sasa ni kubadilika kwa mwenendo wa wapiga kura. Kidogo kidogo wameanza kuangalia zaidi watu na si chama kwenye ngazi ya udiwani na ubunge. Hizi ni dalili mpya.
CHADEMA:
Ujio wa Dr Slaa:
Sio tu umewashangaza CCM na mgombea wake urais, bali pia unaonekana kuwashangaza CHADEMA wenyewe wanaoonekana kutokujiandaa na namna Dr Slaa alivyopokewa na wananchi.
Udhaifu wa CHADEMA
Unajidhihiri kwenye eneo la oganaizesheni na kifedha. Bado CHADEMA haina uwakilishi mpana katika ngazi za mashina na matawi. Dr Slaa anaweza kutua na helikopta Pawaga Iringa, lakini mara ile akiruka, huku nyuma hakuna watendaji wa CHADEMA wa kufanya kazi ya CHADEMA. Kuna taarifa pia za wagombea wake ubunge na udiwani kukosa nguvu za kifedha kuendesha kampeni . Taarifa hizo zilizoripotiwa kwenye vyombo vya habari haziwezi kupuuzwa tu. Hapa inahusu udhaifu katika maandalizi. Kuna wagombea wa CHADEMA watakaoanguka katika chaguzi kwa tatizo hilo.
Zitto Kabwe,
Ni kada nyota ndani ya CHADEMA lakini ‘sarakasi' zake za kisiasa huenda zinachangia kukidhohofisha chama chake kuliko kukipa nguvu. Majuzi hapa aliripotiwa na magazeti kutamka hadharani kuwa anajiandaa kugombea urais 2015. Zitto Kabwe anaacha maswali; Kulikoni ndani ya CHADEMA? Je, Dr Slaa ni mgombea wa ‘msimu' tu? Au ndio sababu Zitto Kabwe hakuhudhuria Mkutano wa ufunguzi wa kampeni za CHADEMA? Kuna watakaouliza.
Inachojivunia CHADEMA:
Bado ni chama kinachoonyesha kuwa na mvuto kama kitajipanga vema. Kesi iliyofunguliwa Mahakamani dhidi ya Dr Slaa kuhusiana na masuala binafsi ya mahusiano inaonyesha kumtangaza zaidi Dr Slaa kwa wapiga kura wanaotia shaka wakati uliotumiwa kuibuliwa kwa suala hilo. Kuna watakaompigia Dr Slaa ' Kura za Kumhurumia'.
Umakini Wa CHADEMA:
CHADEMA imekuwa ikijinadi kama chama makini machoni mwa wapiga kura. Hata hivyo, taarifa zilizochapwa leo ( MWANANCHI) kuwa Naibu Katibu Mkuu , CHADEMA, Zanzibar huenda akaondolewa kwenye timu ya kampeni ya Dr Slaa kwa kuwa amekuwa kero inaonyesha namna timu ya kampeni ya CHADEMA ilivyoshindwa kubaini mapema kuwa Naibu huyo alikuwa kero kwa wapiga kura. Maana, kwa utamaduni wa Watanzania namna Naibu yule Katibu Mkuu alivyokuwa akimfananisha Dr Slaa na Bwana harusi na kauli nyingine pale viwanja vya Jangwani ilikuwa ni ' matusi' hata kama kuna waliotaka kupewa tafsiri sahihi ya neno hilo. Ni heri kwa CHADEMA wameamka na kubaini kero hiyo ndani ya nyumba yao.
Kauli na Ishara:
Kama hakuna aliyelifikiria hili ndani ya CHADEMA, basi, hata kama CCM wanaimba ' Wapinzani tuwalete , tuwakatekate' , hilo ni kosa ambalo halipaswi kujibiwa na kufanya kosa lingiine, Ni pale viongozi wa CHADEMA wanapotamka maneno ya kiingereza; " People's…. Power! Huku wakiamrisha wafuasi wao kusokota ngumi . Kitendo hicho kinatoa ishara mbaya kwa mpiga kura wa kawaida. Bado kuna Watanzania wengi waliopokea maelekezo ya tangu enzi za Mwalimu kuwa; " Tujiadhari na wanaotaka kutusababishia vita na mapigano katika nchi." Kukunja ngumi ni ishara ya kujiandaa kupigana. Kuna kura zinazokimbia kutoka CHADEMA kwa ngumi hizo.
CUF: CHAMA CHA WANANCHI
Katika hali ya kushangaza, CUF ( Bara) safari hii kinaonekana zaidi kuwa ' jokeli' katika karata za kisiasa. Profesa Ibrahim Lipumba bado anaonekana kuwa na nguvu katika kanda ya pwani na mikoa ya kusini. Lakini nguvu hizo haziwezi kulinganishwa na za katika uchaguzi mkuu uliopita. Kuna wakati, CUF wanaonekana kuwa zaidi ' Chama Rafiki' na CCM kuliko chama cha upinzani. Na laiti ' urafiki' huo wa kisiasa ungekuwa kati ya Profesa Lipumba na Dr Slaa, basi, mgombea Urais wa CCM angekuwa na kibarua kigumu zaidi, lakini si kwa sasa, siku 48 kabla ya Oktoba 31. Ninapoandika fikra hizi huru.
Maggid
Iringa
 
Maggid,
Naheshimu sana uandishi wako, lakini haujabainisha conclusions zako zinatokana na utafiti upi. Ni kweli wote tuna mazoea kuwa CCM hushinda kila uchaguzi kama ilivyokuwa Kenya kuzoea kuwa KANU hushinda kila uchaguzi Kwa hiyo ukisema kuwa ni dhana tu kwamba Kikwete ataongoza katika ushindi tutaelewa. Kuna dynamics katika uchaguzi wa mwaka huu ambao na wewe unakiri kuwa wapinzani wanaongezeka nguvu. Huoni kuwa uwezekano wa kuongezeka nguvu za wapinzani unaweza pia kusababisha uwezekano wa Kikwete kupoteza kiti?
 
Jasusi,
Ahsante sana. Nimefuatilia kwa karibu kampeni za mwaka huu tangu Agosti 28 na kipindi kabla ya kampeni. Tunaelewa kuwa takribani asilimia 79 ya wapiga kura wa Tanzania wako maeneo ya mashambani. Na huko ndiko CCM inapotegemea sana kuchota kura zake. Ndio maana ya kuandika; kwa chama au vyama vya upinzani kufanikiwa kukiondoa chama kilicho madarakani katika nchi zetu hizi , ni lazima wafike iliko mizizi ya wapiga kura wake. Nina bahati ya kutembea vijijini. Ukweli huko vijijini hali ni tofauti na sehemu za mijini. Na nilichoandika ni kama uchaguzi mkuu ungefanyika leo. Bado tuna mwezi na nusu umebaki. Katika siasa lolote laweza kutokea.
 
Maggig

Sasa naona kwa nini ulianzisha gazeti halafu baadaye ukaliacha life lenyewe, sababu tu, ya mazoea yako ya kuandikia Raia Mwema, Rai na blog mbalimbali. Mimi pia nimeshindwa kuelewa conclusions zako zimetokana na nini zaidi ya mazoea yako mwenyewe. Nina hakika nikipitia archives zako nitakuta makala hii. Kuna hatari ya kuanza kurudia rudia uliyowahi kusema.

Kwa mawazo yangu:

-Vijijini ndipo CCM ina hali mbaya zaidi kwa sababu ndipo penye shida zaidi (Tanzanian poverty is mostly a rural phenomenon), ndiyo maana hata majimbo ya upinzani tuliyo nayo ni ya vijijini si mjini.

-Uchaguzi ukifanyika leo, CCM haina uhakika wa kushinda, bado iko kwenye shock, lakini in two weeks to come, it might be a different story kwa sababu rafu za CCM dakika za mwisho tunazijua.

Mwisho, ningependekeza swali lako lingekuwa, "Ikiwa uchaguzi ungefanyika kwa uhuru na kwa haki, nani angeshinda?" It does not matter when.
 
Maggig

Sasa naona kwa nini ulianzisha gazeti halafu baadaye ukaliacha life lenyewe, sababu tu, ya mazoea yako ya kuandikia Raia Mwema, Rai na blog mbalimbali. Mimi pia nimeshindwa kuelewa conclusions zako zimetokana na nini zaidi ya mazoea yako mwenyewe. Nina hakika nikipitia archives zako nitakuta makala hii. Kuna hatari ya kuanza kurudia rudia uliyowahi kusema.

Kwa mawazo yangu:

-Vijijini ndipo CCM ina hali mbaya zaidi kwa sababu ndipo penye shida zaidi (Tanzanian poverty is mostly a rural phenomenon), ndiyo maana hata majimbo ya upinzani tuliyo nayo ni ya vijijini si mjini.

-Uchaguzi ukifanyika leo, CCM haina uhakika wa kushinda, bado iko kwenye shock, lakini in two weeks to come, it might be a different story kwa sababu rafu za CCM dakika za mwisho tunazijua.

Mwisho, ningependekeza swali lako lingekuwa, "Ikiwa uchaguzi ungefanyika kwa uhuru na kwa haki, nani angeshinda?" It does not matter when.

Baija Bolobi,
Ahsante sana.
Nahofia unachanganya mambo. Nilichoandika ni mawazo yangu na wewe umekuja na mawazo yako. Changia hoja iliyowasilishwa badala ya kutoka nje ya hoja husika. Nilichoandika sihitaji Masters ya Research Methodologies . Na kama utaweka hapa ukumbini makala ya nyuma yenye kufanana na hiyo niliyoandika, basi, nitaacha kabisa kuandika na nitajitoa uwanachama wa JF. Kama ni mwuungwana nataraji utaniomba radhi ukishindwa kufanya hivyo.
 
Baija Bolobi,
Ahsante sana.
Nahofia unachanganya mambo. Nilichoandika ni mawazo yangu na wewe umekuja na mawazo yako. Changia hoja iliyowasilishwa badala ya kutoka nje ya hoja husika. Nilichoandika sihitaji Masters ya Research Methodologies . Na kama utaweka hapa ukumbini makala ya nyuma yenye kufanana na hiyo niliyoandika, basi, nitaacha kabisa kuandika na nitajitoa uwanachama wa JF. Kama ni mwuungwana nataraji utaniomba radhi ukishindwa kufanya hivyo.
=======

Ukimaliza kuwaomba radhi wana JF kwa kuweka conclusion zako binafsi zisizo na laudable premises, nitafuata katika kukuomba radhi.
 
Baija Bolobi,
Yawezekana wewe ukawa ni ama Msukuma au Mnyamwezi ( Ni watani zangu hao). Kama si hivyo, umefafana nao kidogo kitabia. Hivi si wewe uliyeandika kuwa una hakika kuwa ukipitia archives ungekutana na makala yenye kufanana na niliyopost hapo juu. Na uungwana umekushinda. Nifanyeje? Mimi sitaendelea kulumbana nawe. Vinginevyo uje na jipya.
 
Baija Bolobi,
Ahsante sana.
Nahofia unachanganya mambo. Nilichoandika ni mawazo yangu na wewe umekuja na mawazo yako. Changia hoja iliyowasilishwa badala ya kutoka nje ya hoja husika. Nilichoandika sihitaji Masters ya Research Methodologies . Na kama utaweka hapa ukumbini makala ya nyuma yenye kufanana na hiyo niliyoandika, basi, nitaacha kabisa kuandika na nitajitoa uwanachama wa JF. Kama ni mwuungwana nataraji utaniomba radhi ukishindwa kufanya hivyo.

Duuuh, kwa kweli hawa watani wa jadi kwa hasira na kuzira tu ... haki ya nani tena hamna anayewazidi! lol... Huchelewi kuta hapo Mjengwa kesha kata waya wa kompyuta kutaka kujinyonga kwa kuchokozwa tu mtandaoni :) Ananikumbusha jamaa mmoja pale Mkwawa alikuwa akikuta mtu katumia sukari yake alikuwa anatishia kujinyonga. Kamba zote tuliondoa bwenini na kubakiza toilet paper... jamaa kwa hasira alichukua hiyo toilet paper kama nyenzo yake ya kujitia kitanzi!!! Hapa namwona mtani wangu Maggid akifanya tishio kama lile... :))

Back to matter at hand;
Maggid, unaweza kuelezea vipi uhusiano wa wapiga kura wa vijijini kwa mwaka 2005 ambapo ndiko kulipatikana wabunge wa upinzani na maono yako kwa mabadiliko yaliyopo sasa kwa kutokuwepo wabunge wa upinzani waliowengi kwenye majimbo ya mjini (haswa Dar)?!

Shukrani.
 
Mkuu Majid.M.
Mimi nakuheshimu sana lakini kitendo chako cha kukurupuka huko na kuanza kuwaza tu kua JK atashinda siwezi kukubaliana nacho manake huna details za kutosha,na wewe kabisa unajua kuwa wananchi wamechoshwa na serikali ya JK now watu wanataka wabadiliko na Slaa ndio kimbilio la wengi.kinachotakiwa sasa hivi ni kuendelea kuwaelimisha wenzetu watanzania ambao wanaridhika na ma tshirt na kofia za CCM ili waweze kuelewa haki yao na part gani wanatakiwa waplay for now.we fikiria mwenyewe mwananchi wa kijijini kapewa kofia then anakuja kusafa for 5 years huku mtu(fisadi) alieiba hela anaambiwa azirudushe tu then anasehewa. Wewe tena unakuja na mawazo yako unasema huyu JK atarudi tena, nani atamrudisha?? Kama umetumwa tuambie watu tushajichokea tunataka mabadiliko na Slaa ndie atashinda regardless uchaguzi utafanyika lini.
 
Kamanda Maggid,
Kitu kingine ambacho nimekiona kuwa ni peculiar hapo juu ni kule kujikita kwako kuelezea kiundani zaidi issues za Chadema (haswa mapungufu) kulinganisha na jinsi ambavyo umeelezea CUF au CCM. Je, hili ni kutokana na mapenzi yako zaidi kwa Chadema au kuona nguvu iliyonayo Chadema kwa sasa, au ni kutokana na kutoridhishwa kwako na Chadema?! Waweza kunisaidia tafadhali lipi kati ya haya liko upande wako. Shukrani.
 
Wakuu zangu,
Mimi nakubaliana sana ma Maggid kwa sababu huyu bwana ni mmoja kati ya wafuatiliaji wa uchaguzi huu kwa kufuatana na misafara mingi ya wagombea inayofanyika. Ni mmoja kati ya watu waliokuwa karibu na pengine hata kupenda siasa za Bongo hivyo kufika vijiweni iwe mijini au vijijini na kukusanya mawazo ya watu. Ni rahisi sana kwa mtu kama huyu kutueleza hali halisi kama anavyoina yeye. Na huu mtazamo wake na inabidi sisi wananchi tulitupie jicho swala hili vizuri zaidi.

Labda nishereheshe moja tu kwamba wengi wanaompinga Maggid itakuwa mapenzi yao kwa chama. Wale wa CCM hawatafurahishwa na uchambuzi wa Maggid lakini walioko nje wanauona sawa na wenye kupenyeza hadi pale panapowauma CCM.. Vile vile kwa Chadema na CUF vyama hivi vimeweza kupiga hatua ktk baadhi ya sehemu lakini wameshindwa zaidi kujinadi kutokana na mfumo mzima uliopo na sii zaidi uzembe wa vyama hivi.

Na kikubwa zaidi ya yote ni tofauti baina ya vyama ktk majukumu yao ndani ya uchaguzi huu hata kama kuna hitilafu. Utaona kwamba Mapungufu au makosa ya CCM hayapewi mjadala mkubwa zaidi ya yale yanayotokea Chadema au CUF kwa sababu CCM wanaweza kujipanga wote dhidi ya kashfa fulani kwa pamoja hata kama kuna ukweli mkubwa against them.. Chadema na CUF wao huvurugana na kuifanya habari kubwa kama hiyo ya Zitto na huyo Naibu katibu mkuu kutoka Zanzibar..


Na hakika CCM wanawapiga magoli vyama vingine kwa kuwatumia watumishi wa Umma kama Mabalozi wa nyumba kumi, makatibu tarafa na wengineo kama ni wanaCCM hali haikutakiwa kabisa kuwa hivyo. Ukitazama kama pale alipozungumzia Chadema kufika maeneo na Helikopta kisha wakiondoka kunabakiwa patupu hakuna mwakilishi wa chama zaidi ya diwani au mbunge ambaye hana fedha za kuendesha kampeni baada ya mkutano huo... Hata kama hakuna ukweli katika hili lakini bado huwezi kushindana na chama ambacho kinatumikiwa na balozi wa nyumba kumi, shina, tawi na kuendelea.

Kusema kweli Dr.Slaa amekuja na mabadiliko makubwa sana ktk ushindani ngazi ya rais lakini pekee hawezi kuleta mabadiliko ya ushindi ikiwa Chadema watashindwa kuelewa mapungufu yao na kuweza kuyafanyia kazi ipaswavyo. hakuna chama kilichokuwa kalmili hata hjivyo vya Marekani au Uingereza hupwaya ktk baadhi ya maeneo ya mikakati yao ya Uchaguzi mkuu. Na mara zote yule atakaye dharau kama vile MCcain alivyodharau kuhusiana na Sarah Pallen ndivyo alivyojikuta akishindwa na Obama pamoja na kwamba watu wengi wanafikiria tu uwezo wa Obama na kupuuza mapungufu ya McCain.

Hakuna kiongozi aliyewahi kushinda uchaguzi pasipo mgombea wa Upinzani kuwa na Mapungufu. Hivyo ni mapungufu ya mwengine ndiyo humpa ushindi mwingine zaidi ya mshindi kuwa na nguvu isiyowezekana kushindwa.
 
Maggid hao si walewale bendera fuata upepo. Hana lolote huyo wala usipoteze muda wako kumuuliza alitumia vigezo gani.

Ukweli utajiweka huru 31.10, wala hilo halihitaji Maggid na wenzake wenye mtazamo finyu kama yeye
 
Mimi sina mapenzi wala ushabiki na CCM lakini naweza kuona wazi kwamba Maggid yuko sawa.

CCM kushindwa uchaguzi on the ground ni sawa na CHADEMA kushindwa hii poll ya JF.
 
Mimi sina mapenzi wala ushabiki na CCM lakini naweza kuona wazi kwamba Maggid yuko sawa.

CCM kushindwa uchaguzi on the ground ni sawa na CHADEMA kushindwa hii poll ya JF.
acha woga,we unamuogopa majig kwa vile ana blog? Jk hatoki mwaka huu pamoja na kampeni zao chafu,wewe unafikiri hata Slaa akishinda atashinda na %100? Mimi namfananisha na yule miss aliyeulizwa swali. Propaganda zake za kushinda kwa JK ni sumu kwa watu ambao washaanza kufumbuka macho hapa mkulu harudi magogoni nia harudi. Full stop. Chadema ni chama ambacho kipo tayari kuongoza nchi na hakikurupuki.
 
acha woga,we unamuogopa majig kwa vile ana blog? Jk hatoki mwaka huu pamoja na kampeni zao chafu,wewe unafikiri hata Slaa akishinda atashinda na %100?

Mimi nilishasema hayo aliyosema Maggid kabla hata yeye hajatoa hii post, sasa sioni swala la uoga linatoka wapi.
 
kwenye hizi kura za maoni za JF umempigia nani?

Nimempigia Slaa, na nime mu endorse watu wampigie kura kwenye uchaguzi kuongeza competition Tanzania upinzani uongeze asilimia ya kura gradually, lakini nakubali Slaa hawezi kushinda urais. Wala CHADEMA haiwezi kupata majority ya wabunge.
 
Jasusi,
Ahsante sana. Nimefuatilia kwa karibu kampeni za mwaka huu tangu Agosti 28 na kipindi kabla ya kampeni. Tunaelewa kuwa takribani asilimia 79 ya wapiga kura wa Tanzania wako maeneo ya mashambani. Na huko ndiko CCM inapotegemea sana kuchota kura zake. Ndio maana ya kuandika; kwa chama au vyama vya upinzani kufanikiwa kukiondoa chama kilicho madarakani katika nchi zetu hizi , ni lazima wafike iliko mizizi ya wapiga kura wake. Nina bahati ya kutembea vijijini. Ukweli huko vijijini hali ni tofauti na sehemu za mijini. Na nilichoandika ni kama uchaguzi mkuu ungefanyika leo. Bado tuna mwezi na nusu umebaki. Katika siasa lolote laweza kutokea.

Maggid;ni nadharia tu isiyokuwa na back up hata moja ya kisayansi inayoonyesha kuwa CCM itashinda maana itapata kura nyingi sana vijijini,wangejua hayo hawa CCM wasingemuongezea Rais JK masaa na siku za kampeni na kumfanya kuwa labda ndiye Rais wa kwanza aliyepo madarakani hapa duniani kukampeni muda mrefu zaidi hata ya wapinzani wake wasiowahi kukanyaga Ikulu!

Maggid;Nijuavyo mimi,Rais aliyepo madarakani huwa anapita tu majimboni kuwakumbusha wapiga kura nini kakifanya kwao kwenye hiyo miaka 5 aliyomaliza;tofauti yake sasa JK ndiye anayeeongoza kwa kutoa ahadi kama vile hakuwa Rais wa TZ muhula uliopita.Nakukumbusha tu kuwa kimkakati wapinzani ndiyo walipaswa kutoa ahadi watafanya nini wakichaguliwa lkn JK alitakiwa aseme katufanyia nini miaka hii 5 tuliyomchagua;vijijini pia wamekwisha mshtukia!

Maggid;ona ukweli huu,Slaa kaleta muamko kwa watz kwa kila mahali kama vile Mrema mwaka 1995 lkn tofauti yao ni"new-generation";Mbeya vijijini wapiga kura wake wapo scattered vijijini na dhahiri Tambwe Shitambala anasubiri tu kuapishwa,Busanda sio mjini na CCM walishinda kwa rafu;Arfi kaleta mabadiliko kwa wapiga kura wa vijijini kule Rukwa;nakukumbusha tena Kyerwa na Karagwe zipo Kagera Vijijini;Nakukumbusha hata Njombe Magharibi sio mjini na CCM likely wamekubali kama wamepoteza jimbo au Jimbo analoliwania Lissu kule Singida lipo mjini?Watz mwaka huu wamechoka na CCM na "inaweza"kwenda na maji maana ni huko huko vijijini wanapokabana koo na Dr Slaa na Lipumba!

Siasa ipo dynamics sio kwa vile CCM kila mwaka inapata kura nyingi vijijjini basi ndiyo itakuwa hivyo milele;KANU ya Kenya ipo hoe hae,MCP ya Banda ilikufa,ZANU-PF ya Mugabe inashinda kwa mabavu,UNIP ya Kaunda imetoweka au hata Rais wa sasa wa Mexico Felipe Calderon na chama chake cha "leftist"waliponyakua madaraka toka chama cha PRI waliokuwa madarakani kwa miaka zaidi ya 80 kabla hawajapoteza uchaguzi,au unamkumbuka Abdolouye Wade wa Senegal alitumia muda gani kushinda u-Rais!

Maggid;CCM safari yakuelekea"kuzimu"inaonekana ipo wazi kabisa hasa kwa uongozi wa kibabaishaji kama huu wa JK,Makamba,Chenge,AR na wengine maana CCM ya sasa sio iliyoachwa na MWL Nyerere!
 
mkuu nyani, hakuna member wa JF ambae atapiga kura kwa mkwere hapa, wote tunampa slaa, hata maggid kura yake tunayo kwa slaa, ila sasa kwenye field ndo pana utata, sababu tuko wachache, labda tupeane jukumu la kila member hapa atafute watu kumi tu ambao wamejiandikisha kupiga kura, wawe ndugu au marafiki, ambao tunakuwa na uhakika wa kura zao kwa slaa! tukiwa na uhakika wa kura zetu wenyewe, hata ccm wakiiba, tuna haki ya kufanya fujo, hata kupigana ili haki ipatikane...,
 
Back
Top Bottom