Dijovisonjn
JF-Expert Member
- Nov 14, 2011
- 466
- 125
Siku nikipata nafasi ya kuwateulia watanzania rais kutoka katika vyama vyetu vya siasa nitawateua wafuatao:-
1) kutoka CCM nitamteua Edward Lowasa kuwa rais.
Yeah kweli kabisa na nipo serious kuwa CCM cjamuona mtu wa kuwa rais wangu tofauti na EL, wengi najua hapa watanichukulia kwa mitazamo yao tofauti watakayoona kwa sababu ndugu EL alihusishwa na kashfa za ufisadi haswa richmond, lakin pamoja na hayo yote hakuna kiongozi makin na mwenye maamuzi ya haraka ndani ya ccm kama EL nakumbuka katika kipindi chake cha uwaziri mkuu serikalini kulikuwa na adabu wafanyakazi walifanya kazi migomo ilikuwa michache tofauti na sasa kweli mshikaji alikuwa mchapa kazi na mpaka leo najiuliza ni kwa nini haswa aliiruhusu richmond ila sipati majibu, pamoja na kashfa zake zoote alizonazo binafsi bado sijaona mwanaccm yeyote yule anayefaa kuwa rais wangu tofauti na EL.
Labda kwa mbaaali namuona ndugu Membe kama mtu anayefaa kuchukua nafasi ya EL kwa sababu binafsi namuona Membe kama waziri makini na anayejua mambo nadhani Membe anastahili kuwa chaguo namba mbili kwangu. Lakin wote hawa watakuwa viongozi wazuri zaidi kama wataukwepa ule mchezo wa kuform serikali (executive) kwa kuwatumia maswahiba wao!
2) kutoka CHADEMA nitamteua Dr Slaa kuwa rais.
Nisipomteua Dr Slaa binafsi nitakuwa siitendei haki nafsi yangu, Dr Slaa kwanza kabisa ana ushawishi mkubwa sana kuliko kiongozi yeyote yule ndani ya CHADEMA, anaonekana kama mzalendo (sina uhakika kama ni mzalendo kweli au anaigiza kuwa mzalendo) na mwenye uchungu na Tanzania, binafsi naamini mafanikio ya CHADEMA ya leo ni kutokana na uwepo wake, naamini kama akiwa raisi kwa kiwango fulani tunaweza kupiga hatua mbele kimaendeleo.
Mbali na Dr Slaa ndani ya CHADEMA binafsi namuona mbunge wa Ubungo ndugu John Mnyika kama mtu sahihi anayefaa kuwa rais kama dr akimaliza muda wake, kwanza kabisa binafsi naamini Mnyika ndiye mbunge bora wa bunge hili la tisa, kwanza ni kijana anayejua mambo mengi sana pia ni mtu asiyeongea ili mradi ameongea tu na kitu alichowahi kunifurahisha zaidi ni kipindi kile alipokuwa na likitabu la bajeti ya Zambia, pia kuwa na blog yake anayoitumia kuwaelezea wananchi mambo mbalimbali yanayohusu kazi zake. Binafsi namkubali sana Mnyika na naamini kama sio Dr Slaa Mnyika atafaa zaidi kuwa rais wa watanzania kutoka CHADEMA.
3) kutoka CUF sijamuona wa kumteua!
kabla CUF hawajamfukuza ndugu Hamad Rashid, Hamad Rashid ndiye mtu niliyekuwa namuona anafaa kuwa rais wa watanzania kutoka CUF lakin baada ya kumtimua, CUF imeniacha bila chaguo lolote lile, binafsi sioni sura ya mtu kuwa rais wa watanzania kutoka CUF labda ngoja nisubiri atajitokeza badae.
4) kutoka vyama vingine vya siasa bado sijaona kabisa labda ngoja nisubiri naamini ipo siku nitamuona.
1) kutoka CCM nitamteua Edward Lowasa kuwa rais.
Yeah kweli kabisa na nipo serious kuwa CCM cjamuona mtu wa kuwa rais wangu tofauti na EL, wengi najua hapa watanichukulia kwa mitazamo yao tofauti watakayoona kwa sababu ndugu EL alihusishwa na kashfa za ufisadi haswa richmond, lakin pamoja na hayo yote hakuna kiongozi makin na mwenye maamuzi ya haraka ndani ya ccm kama EL nakumbuka katika kipindi chake cha uwaziri mkuu serikalini kulikuwa na adabu wafanyakazi walifanya kazi migomo ilikuwa michache tofauti na sasa kweli mshikaji alikuwa mchapa kazi na mpaka leo najiuliza ni kwa nini haswa aliiruhusu richmond ila sipati majibu, pamoja na kashfa zake zoote alizonazo binafsi bado sijaona mwanaccm yeyote yule anayefaa kuwa rais wangu tofauti na EL.
Labda kwa mbaaali namuona ndugu Membe kama mtu anayefaa kuchukua nafasi ya EL kwa sababu binafsi namuona Membe kama waziri makini na anayejua mambo nadhani Membe anastahili kuwa chaguo namba mbili kwangu. Lakin wote hawa watakuwa viongozi wazuri zaidi kama wataukwepa ule mchezo wa kuform serikali (executive) kwa kuwatumia maswahiba wao!
2) kutoka CHADEMA nitamteua Dr Slaa kuwa rais.
Nisipomteua Dr Slaa binafsi nitakuwa siitendei haki nafsi yangu, Dr Slaa kwanza kabisa ana ushawishi mkubwa sana kuliko kiongozi yeyote yule ndani ya CHADEMA, anaonekana kama mzalendo (sina uhakika kama ni mzalendo kweli au anaigiza kuwa mzalendo) na mwenye uchungu na Tanzania, binafsi naamini mafanikio ya CHADEMA ya leo ni kutokana na uwepo wake, naamini kama akiwa raisi kwa kiwango fulani tunaweza kupiga hatua mbele kimaendeleo.
Mbali na Dr Slaa ndani ya CHADEMA binafsi namuona mbunge wa Ubungo ndugu John Mnyika kama mtu sahihi anayefaa kuwa rais kama dr akimaliza muda wake, kwanza kabisa binafsi naamini Mnyika ndiye mbunge bora wa bunge hili la tisa, kwanza ni kijana anayejua mambo mengi sana pia ni mtu asiyeongea ili mradi ameongea tu na kitu alichowahi kunifurahisha zaidi ni kipindi kile alipokuwa na likitabu la bajeti ya Zambia, pia kuwa na blog yake anayoitumia kuwaelezea wananchi mambo mbalimbali yanayohusu kazi zake. Binafsi namkubali sana Mnyika na naamini kama sio Dr Slaa Mnyika atafaa zaidi kuwa rais wa watanzania kutoka CHADEMA.
3) kutoka CUF sijamuona wa kumteua!
kabla CUF hawajamfukuza ndugu Hamad Rashid, Hamad Rashid ndiye mtu niliyekuwa namuona anafaa kuwa rais wa watanzania kutoka CUF lakin baada ya kumtimua, CUF imeniacha bila chaguo lolote lile, binafsi sioni sura ya mtu kuwa rais wa watanzania kutoka CUF labda ngoja nisubiri atajitokeza badae.
4) kutoka vyama vingine vya siasa bado sijaona kabisa labda ngoja nisubiri naamini ipo siku nitamuona.