Jamaa mmoja katika bar alisema hivi:- Jamaa: mhudumu nipe kinywaji na kila mmoja mpe kinywaji humu ndani mana wakati mimi nakunywa beer basi lazima kila mtu apate yake...... Mhudumu kwa haraka haraka akagawa vinywaji,,,,,, Jamaa akasema tena: mhudumu nipe supu nakila mtu humu ndani mpe supu mana wakati mimi napata supu basi lazima kila mtu apate supu,,,,,,, Mhudumu akagawa supu tena safari hii wote wakapiga makofi..... Kisha jamaa akasema: mhudumu nipe bili na kila mtu humu ndani umpe bili maana wakati mimi nalipa bili yangu basi lazima na kila mtu alipe bili yake,,,,,,,,, Jee kama ni wewe ungeliweza kulipa?