Kama ni Demokrasia ya JF.. Piga kura yako: Wengi wape

Bila ya shaka mmeanza kuona pembeni kuna sanduku la Kura. Swali la Msingi ni kuwa Kuendelea na habari binafsi za ngono za viongozi ambazo hazihusishi uvunjaji wa sheria au kuingilia utendaji wao wa kazi hapa JF. Chukua msimamo na kura za wengi basi ndio wapewe na uamuzi wao uheshimiwe. Kwa vile JF ni eneo la demokrasia ambapo panastahili kuwa na heshima yake basi tuamue suala hili kwa kupiga kura na uamuzi wowote wa walio wengi uheshimiwe.

M. M

Mwanakijiji,

Ni kura gani hiyo inaandaliwa utafikiri na ile tume ya uchaguzi ya Saddam?

Huwezi kuja ghafla na kuwaambia wana JF piga kura, wewe ni nani? Ni tume ya uchaguzi? Ni mmiliki wa JF?

Kura ina maana kubwa mno kuliko unavyodhani Mwanakijiji. Demokrasia sio tu maana ya watu kupiga kura, badala yake ni process nzima kuanzia uamuzi wa kupiga kura, utayarishaji wa maswali , njia ya kutumia kura na namna ya kuhesabu hizo kura.

Nafikiri Mwanakijiji ukipewa power utakuwa dikteta mkubwa sana.

Kinachotokea hapa ni kwamba hutaki kukubali kwamba kwenye ile issue ya JK ulifanya makosa na sasa unatafuta kila njia ili uonyeshe ulikuwa right.

Come on brother! Grow up, endelea mbele, maisha sio kung'ang'ania jambo moja mpaka ushinde. Hakuna binadamu anayekuwa right wakati wote, kuna wakati inabidi kukubali kushindwa na ku move on.
 
Mtanzania kula tano hapo.

Mimi pia nashangazwa na huu mchemsho mpya wa Mwkjj, iweje wewe yeye aandae kura ya maoni kuhusu uendeshaji wa JF yeye nani MOD au Invisible? mbona anachukua mamlaka yasiyo yake.. hapo ndipo sisi wahafidhina tunapata wasiwasi juu ya hii kura kama itakuwa free and fair au walau i reflect matakwa ya wengi.

Nafahamu kuwa mwanachama anaweza endesha kura ya maoni kama alivyofanya Mchambuzi lakini kwenye masuala yasiyo husiana na uendeshaji wa JF kama kuna jambo kama hilo basi linatakiwa lianzishwe na Invisible au any of the MODS.

Kwenye hili Mwkjj unataka kuwa polisi, hakimu, mwendesha mashtaka, bwana jela nk hivi kweli haki ipo hapo?

No wonder time to time umekuwa ukitumia msemo "nitaiondoa" "nitaihamisha" nakawa najiuliza where the hell r u getting those powers.. sasa unafikiri utamshawishi nani wakati wewe "Mwenyekiti wa tume ya uchaguzi" ushasema wazi msimamo wako.

Acha kutuletea mazingaombwe, tumestuka.....
 
Jamani msije mkamfanya Mwanakijiji akakimbia kama Mchambuzi.

Maana Mkuu alimkoma Nyani kisawasawa sasa Nyani kaamua kumgeuka,
ha ha ha
 
Halafu kura za maoni hazikai kwenye front page zina sehemu yake. Hapo ulipolazimisha kuiweka kura yako mwkjj inaleta udhia kwa wengine na huko ndio kuburuzana kwenyewe tunako kuzungumzia.
 
neno demokrasia msilitumie vibaya. hivi mtu anaendekeza ngono katika maslahi ya jamii bado mnatafuta kura?.jaalia hapa jf kuna wazinifu kama yeye, hivi kweli unadhani watamsaliti mzinifu mwenzao? com on guys, uhalifu hauingizwi kwenye demokrasia na hakuna asiejua kwamba swala la kuendekeza ngono ya nje ya ndoa kwa mila za kitanzania na za kiimani ni uhalifu. sipigi kura kwa sababu hili suali lipo very clear kwamba halikubaliki, na maadam halikubali na linafanywa na viongozi wa siasa lazima liwekwe kwenye ukumbi wa siasa ,liko wazi .kulipeleka kwenye udaku sijui vibweka ni kuwafichia hawa wakubwa madhambi yao kwani ni wachache sana wanaotupa jicho kwenye udaku.nilikwambieni kwamba huu ukumbi unahitaji usahau uchadema na uccm na u cuf ndio uweze kuleta mabadiliko kwa jamii.zinaa itabaki kuwa ni dhambi tena ni kashfa na pia ni adui wa maendeleo.kama anaeifanya ni mwanasiasa , iwekwe kwenye ukumbi wa siasa. khalas
 
gamba, I ain't no mchambuzi... you should know that by now.. I can take any punch!

Sasa kamanda mbona poll "umeiondoa" kinyemela? walau basi ungetufahamisha wadau sababu zilizopelekea "uamuzi" wako huo mkuu, au ndio matokeo yalianza kwenda kinyume na "matarajio" ukaamua kuingia mitini na "masanduku" ya kura! Zanzibar style lol!
 
Sasa kamanda mbona poll "umeiondoa" kinyemela? walau basi ungetufahamisha wadau sababu zilizopelekea "uamuzi" wako huo mkuu, au ndio matokeo yalianza kwenda kinyume na "matarajio" ukaamua kuingia mitini na "masanduku" ya kura! Zanzibar style lol

ha ha ha. kwenye soka hii tunaiita "man to man"
kwenye mapambano ya hoja hii inaitwaje?
 
Sasa kamanda mbona poll "umeiondoa" kinyemela? walau basi ungetufahamisha wadau sababu zilizopelekea "uamuzi" wako huo mkuu, au ndio matokeo yalianza kwenda kinyume na "matarajio" ukaamua kuingia mitini na "masanduku" ya kura! Zanzibar style lol!


poll yenyewe ilianza kuonesha kuelemea upande "wetu" sasa watu wakaanza kulalamika kuwa poll iko biased.. labda huko mbeleni we'll figure out a way of getting into some decisions.. hapa JF..
 
Back
Top Bottom