Kama MWAKYEMBE na MAGUFULI wanafanya uhuni huu basi CCM imedhamiria kuwazika Watanzania!!!

Na wewe ni walewale msioona hata jambo zuri ambao kila kukicha ni kulalama tu utadhani hata kwenye familia yako unatimiza wajibu na majukumu yako sawasawa, mi nilidhani kama kweli wewe ungelikuwa muungwana; japo huoni jitihada zozote za kulipatia ufumbuzi tatizo la foleni walau ungeanza hata kwa kupongeza jitihada za upanuzi wa barabara, Eti watanzania wanapenda kushabikia...

Usiwe na mpapatiko wa moyo, nyie ndo huwa mnasubiri ama kuombea mtu aharibikiwe ndo mcheke na kusema mambo kibao!! kuondoa watu elfu moja karibu na mia tano kwenye ruti za kila siku za barabarani na kuwapitisha kwenye reli unaona ni kitu kidogo? Fly overs sawa lakini unaanzia wapi kwanza? wewe mbona una hisia za kusukuma gari ukiwa umelipanda? ni laziama uwe na pa kuanzia,achana na ujinga wa kukatisha watu tamaa hata kwa juhudi thabiti zinazooonekana bayana!

Mabasi yaendayo kasi yataleta ushindani wa kibiashara hata kama hawatazuia wasafirishaji binafsi, mwisho wa siku watayapunguza magari yao kama si kuyaondoa kabisa barabarani maana kila mtu atahitaji kuwahi kazi zake hawezi kusubiri gari ambalo lina vituo lukuki.

Hapo kwenye Bluu ndo umenidhihilishia una roho ya kwanini, kumbe suala hapa si Reli au mabasi yaendayo kasi bali unaumizwa na umaarufu na utendaji unaokubalika na wengi wa hao mawaziri wawili, chuki zingine ni za kijinga, unajieleza undani wako bila kutambua YAMTOKAYO MTU KINYWANI NDIYO YAUJAZAYO MOYO WAKE!! SHAME ON YOU...

Naona sasa unataka kunisaidia kufikiria.
 
tutajie km 1 ya barabara ya lami inatengenezwa kwa =sh ngapi

kisha miundo mbinu ya train na train imegharimu sh ngapi ili to compare na tucontrast mkuu

then tuangalie km ngapi zingehitajika kukarabatiwa na pesa kiasi gani zingeokolewa kwa "kazi ya kipuuzi "alioifanya Mwakyembe according to tu.
We need critical analysis

Mkuu unamiliki magari mangapi aka Daladala labda kakuaribia soko.

Walala hoi tunamshukuru Mwakyembe;
hatulipishwi nauli ya kugeuza na gari
Gongo la Mboto Posta 1000 bac tena
 
Sasa Ebu kwa mtaalam ambaye si Mtazania na anayefikria vizuri msomi utuambie jinsi Reli zilizoanzishwa zitakavyo discourage watu kutumia private transport. Uje kwa mifano dhahiri!!!!!!!! MF. Foleni toka Kibamba mpaka Ubungo, Mwenge mpaka Tegeta...... wakt Reli iko mabibo mpaka posta......
Mkuu nakushauri usiwe small time thinker!

Treni moja inachukua watu karibu elfu moja, hizo ni daladala ngapi na magari mangapi.
Matatizo ya usafiri jijini Dar, hayatatatuliwa na off the shelf solutions na ndio maana Magufuli na Mwakyembe wanapongezwa kwa kuwa na uthubutu wa kufikiria tofauti na wengine kwa miaka mingi.

Google hata historia ya usafiri wa umma(mass tranport) hapa mtandaoni na utashangaa wale walioendelea walianza zaidi ya miaka mia moja iliyopita kutumia njia kama hizi tunazo anza leo.
 
Hii ya treni ni hatua nzuri kwa kuanzia. Then zije hizo brt na flyovers. Kwa kuwa una wivu na Mwakyembe na Magufuli, washauri wajenge kivuko kutoka kunduchi na kuja ferry. Hapo kunduchi waweke ample parking ili tiache magari yetu kwenye usalama na tupande speed boat kuja town. Hamna haja ya mtu wa bunju kudrive kila siku kuja city centre.
maendeleo yanakuja kwa hatua mkuu.

Au wewe ni mwenyekiti wa CHAUMMA?


Sasa hapo wivu wa nini mkuu! Hawa jamaa nawakubali amechemka. Magogo outdated alafu mbwembwe kibao.....
 
Ni jambo la kusikitisha na kushangaza kuona Watanzania wanashabikia matukio haya mawili la Basi ziendazo Kasi BRT
(BRT) na uzinduzi wa
Reli kwa Jiji la Dar es Salaam. Mipango hii yote inaongozwa na watu wanaojitambulisha kuwa kuwa wachapa kazi kina Magufuli na Mwakyembe.
Ukweli kwamba ni danganya toto kwa sababu zifuatazo:


1. Tatizo la msongamano wa magari halisababishwi na kuwepo kwa gari za abiria ( public transport) bali ni private cars na maroli.
2. Msongamano huu unaletwa na kwenye junctions( nodes) mf. Ubungo mataa, Shekilango, Njia panda ya Tabata, Buguruni, Magomeni Mapipa,......
na suluhisho ni fly overs.
3. Reli hizi zinaishia pafupi sana na haziondoi au kuzuia watu binafsi kwenda na magari yao.
4. Hakuna parking Dar na watu wengi hubakia barabarani wakizunguka wkt wengine walionao wanafanya issue zilizowaletra mjini.
5. Upanuaji Barabara haupunguzi foleni bali hupunguza urefu wake na kutengeneza foleni fupi yenye mistari mingi ya magari mf. barabara ya Mwenge to Ubungo kupita Mcity.
kwa msisitizo zaidi ni sawa na kuweka maji kwnye mrija wa kunywea soda ukajaa alafu na mengine ukajaza beseni na mtoto akaulizwa maji mengi yako wapi naye akachagua mrija kisa umezidi beseni kwaurefu.

Sasa hela kubwa inayotumika kutengeneza barabara za BRT na Reli ingefanya yafuatayo kama si ufisadi:
  1. kutengeneza barabara zote mbovu za kupunguza msongamano kwemye Barabara ya Moro kwa kiwango cha lami ili kupunguza kufurika kwa magari Morogoro road mf. Barabara ya Kimara na Mbezi to Uwanja wa Ndege, Kimara na Mbezi to Tegeta........
  2. kuwekeza kwenye Fly Overs kwenye mataa yote.
  3. kuboresha na kupanua barabara hasa vituo amabvyo viko barabarani hasa mf. njia ya Tandare.


MUHIMU: wATANZANIA tunapenda kushabikia mambo bila kuyachunguza na sasa tusubiri tuone jinsi hii mipango 2 isivyo na tija bali danganya toto.

mkuu hat Roma haikujengwa siku moja. kwa sasa Mwakyembe ameonyesha njia angalau bado hajafaulu kupunguza 4len , lakini ameonyesha njia katika kutatua suala la usafiri Bongo. Tumuunge Mkono ili aendelee na uboreshaji wa hicho alichoanzisha.
 
nimemuelewa point yake, kuna baadhi ya sehemu hapa dar barabara ni mbovu sana hazifai kupitishia magari na hizi barabara zingeweza kutumika kama short cut zikapunguza foleni sana maeneo mengi kwa hiyo ni kweli wizara ya ujenzi wangeweka lami au kuzifukia fukia zikawa zimenyooka zingepunguza foleni maeneo mengi sana, hizi treni tunawapongeza kwa juhudi zao lakini zinawanufaisha baadhi tu ya wakazi bado kuna sehemu nyingi sana foleni zitakuepo..TANROADS wanapokea bajeti kubwa tu ya kutengeneza barabara hapa mjini sijui hua wanazifanyia nini hizo hela

Ni ukweli mtupu mkuu, kila baada ya muda mfupi wanafanya ukarabati na kwiba hela eti leo wanaziacha na kuja na treni na brt!!! Ushabiki bwn!!!
 
Mleta uzi si kweli wanayoyafanya Magufuli na Mwakyembe ni maamuzi yao binafsi kiasi cha kuwaita wahuni. Haya si mawazo yao binafsi!! Huu ni mchakato wa siku nyingi ambao hata Bunge limehusishwa. Iweje leo hawa wawili waonekane ni wahuni kwa kutekeleza mipango ya kitaifa? Kuna mantiki nyingi tu kwenye hoja yako ila kuwaita wahuni hawa mawaziri hujawatendea haki. Hizi point ungezitoa wakati miradi hii inajadiliwa. Vuta subira uone matokeo kama siyo mazuri basi majadilianao yataanza kuhusu nini kifanyike kurekebisha kasoro zitakazojitokeza.

Kwa kuongezea pengine kwa siku za karibuni, kuwe na "park lots" salama kwa ajili ya magari madogo binafsi nje ya jiji kama vile Ubungo, Mwenge, Mbagala, Tabata nk. Watakaoingia na magari madogo katikati ya jiji watozwe kiasi ambacho wataona ni vema kuchukua public transport au la, kulingana na shughuli walizo nazo. Hizi park lots zinaweza zikajengwa na kuendeshwa na sekta binafsi siyo lazima serikali.
TUWAPONGEZE KWA UJASIRI WALIOONYESHA. CHANGAMOTO ZILIKUWA NYINGI NA WAMEZIKABILI VILIVYO. MNYONGE MNYONGENI HAKI YAKE MPENI!!!!:A S thumbs_up:​
 
Mkuu, unalosema ni sawa. Sasa treni itafika kila sehemu? Unajua moja ya mapungufu ya reli hasa hizi zetu zenye poor technology? Is poor accessibility, lkn ujue kuwa haitapunguza foleni na haitafika mahala pote kama magari!!!!!

Bwana Paulo,kuwa makini katika kuyachanganua mambo,kama kuna sehemu zenye idadi kubwa ya watu na hasa wenye hali ya kawaida sana ni maeneo ya mbagala(Wilaya ya Temeke) na Gongo la mboto(wilaya ya Ilala) kisha kinondoni, Treni hizi za TRL na TAZARA hata kama unasema hazifiki kila sehemu kitu ambacho kwanza unadhihilisha ubazazi wako, kwani magari yanafika kila sehemu? hujashuhudia utitiri wa pikipiki kila sehemu na hasa sehemu ambako magari hayafiki?

Ikiwa treni ya TAZARA ina ruti 24 kwa siku na kwa sehemu kubwa itawahudumia watu wa Temeke walio wengi huoni mchango wake? Treni ya TRL itakuwa na ruti kama hizo na kwa sehemu kubwa watu Ilala itawahudumia huoni mchango wake?

Hapo kwenye nyekundu kwani tatizo la teknolojia ndo limeonekana kuwa tatizo zaidi kwa kuanzishwa hizi ruti? au vp ulitaka kufumba na kufumbua ziwepo treni za umeme zinazokwenda kasi ama zisizokuwa na muongozaji binadamu? Pls.. jifunze kutambua juhudi za wenzako, mi ninavyoona hapo walipoanzia sio pabaya huo ushauri wako utafuata baadaye lakini kwanza tambua jitihada za mwanzo, ndo ugomvi wangu mimi na wewe Bwana Paulo!!
 
Hii mada ni nzuri sana ingawa watu wengi wamejibu kwa Jazba bila ya kutafakari kwa kina. Labda ni aina ya watu waliosoma huu uzi. Hata hivyo mtoa hoja umekosea kidogo kwa title yako kuwaita Mwakyembe na Magufuli wanafanya uhuni. Lakini ukiachia hilo, ngoja nitoe mawazo yangu:

1. Nionavyo mimi, usafiri huu ni mzuri sana, lakini umeanzishwa kisiasa zaidi kuliko kuzingatia hali halisi na mahitaji. na kwa sababu umeanzishwa kisiasa zaidi, naamini hautaweza kupata faida walau kwa miaka mitatu ijayo. Lazima TRL na TAZARA wategemee fedha toka serikalini na mwisho wa siku, mradi utakufa natural death.

2. Mradi wa mabasi yaendayo kasi ni kiini macho kingine na unaenda pia kisiasa. Haya mabasi yatakuwa na tofauti ipi na zile Ikarus za UDA enzi zile?? Barabara zipi zitahudumiwa?? Reli ya TRL inakwenda Ubungo, Mabasi yaendayo kasi yanakwenda Ubungo. Ina maana ubungo peke yake ndio source ya foleni kubwa ya dar? Ina maana Ubungo peke yake ndio kuna watu wa kipato cha chini?? SIASA ili ionekane something had been done.

3. Naweza kupewa mfano wa nchi yoyote duniani au hata Afrika ambayo imefanikiwa kwa kupitia mpango wa mabasi yaendayo kasi?? Mimi nina mfano hai wa Afrika Kusini ambako nimeshuhudia usafiri huo na jinsi usivyokuwa na faida Johannesburg. Nipeni mifano ya sehemu zenye mafanikio. SIASA!

Nini kifanyike au kingefanyika?

1. Nakubaliana na Hoja ya mtoa mada Paul Kijoka kuwa barabara mbadala zingekuwa suluhisho kubwa kama zingeboreshwa. hakuna sababu ya wote kutumia barabara ya Ally Hasan Mwinyi toka Tegeta hadi mjini. Hakuna sababu ya wote kubanana barabara ya Morogoro kuelekea kariakoo hadi mjini. Njia za mitaani zikiboreshwa itakuwa suluhisho zuri.

2. Kuufanya Dar kuwa mji mkuu wa kibiashara na mji mkuu wa serikali ni makosa makubwa. Kila ofisi ya serikali kuanzia Ikulu hadi Benki kuu zimebanana mjini. Mahoteli makubwa mjini, maduka mjini, ofisi binafsi mjini, wamachinga mjini. Lazima kuwe na msongamano. Mapafu ya mji yanapaswa kupanuliwa. Ikulu ikienda Dodoma, wizara zikihamia Dodoma, ofisi nyingi binafsi zikienda Mwenge, Tegeta na Kimara ama Gongo la Mboto na Mbagala, basi watu tutapungua kwenda mjini na foleni ama msongamano itapungua.

HATA HIVYO

Sikubaliani na wazo la Flyovers sababu Ramani ya Dar es salaam imeshaharibiwa na ujenzi holela uliokuwa hauzingatia matakwa ya baadae. Itakuwa ni kupoteza muda na fedha.

Narudia, wazo la Mwakyembe zuri sana na treni inaweza kuwa nzuri. lakini utekelezaji wake uko kisiasa zaidi. Namwamini Mwakyembe na hata Magufuli wanaweza kufanya mambo mazuri zaidi kama wasipobanwa na serikali yao ya CCM na wakapewa ushirikiano na wenye nchi. Lakini kwa hali ilivyo sasa wanajikuta wakiingia kwenye mkumbo wa kufanya siasa kwenye mambo ya msingi yasiyohitaji siasa
 
Mmeshikwa pabaya

upande maichukia ccm with passion

halafu mna mapenzi ya dhati kwa wana ccm ambao wanatekeleza ahadi za ccm

sasa mtafanyaje?

Kwisha khabari zenu maana mmekuwa na split personalities.
 
Jamaa daladala lake lishakosa dili, pole bana, mlishazoea kutesa abiria na kauli zenu chafu
Poleni bana treni ndo suluhisho, no kuzungusha wala kukatisha rout
 
Ni jambo la kusikitisha na kushangaza kuona Watanzania wanashabikia matukio haya mawili la Basi ziendazo Kasi BRT
(BRT) na uzinduzi wa
Reli kwa Jiji la Dar es Salaam. Mipango hii yote inaongozwa na watu wanaojitambulisha kuwa kuwa wachapa kazi kina Magufuli na Mwakyembe.
Ukweli kwamba ni danganya toto kwa sababu zifuatazo:

1. Tatizo la msongamano wa magari halisababishwi na kuwepo kwa gari za abiria ( public transport) bali ni private cars na maroli.
2. Msongamano huu unaletwa na kwenye junctions( nodes) mf. Ubungo mataa, Shekilango, Njia panda ya Tabata, Buguruni, Magomeni Mapipa,......
na suluhisho ni fly overs.
3. Reli hizi zinaishia pafupi sana na haziondoi au kuzuia watu binafsi kwenda na magari yao.
4. Hakuna parking Dar na watu wengi hubakia barabarani wakizunguka wkt wengine walionao wanafanya issue zilizowaletra mjini.
5. Upanuaji Barabara haupunguzi foleni bali hupunguza urefu wake na kutengeneza foleni fupi yenye mistari mingi ya magari mf. barabara ya Mwenge to Ubungo kupita Mcity.
kwa msisitizo zaidi ni sawa na kuweka maji kwnye mrija wa kunywea soda ukajaa alafu na mengine ukajaza beseni na mtoto akaulizwa maji mengi yako wapi naye akachagua mrija kisa umezidi beseni kwaurefu.

Sasa hela kubwa inayotumika kutengeneza barabara za BRT na Reli ingefanya yafuatayo kama si ufisadi:
  1. kutengeneza barabara zote mbovu za kupunguza msongamano kwemye Barabara ya Moro kwa kiwango cha lami ili kupunguza kufurika kwa magari Morogoro road mf. Barabara ya Kimara na Mbezi to Uwanja wa Ndege, Kimara na Mbezi to Tegeta........
  2. kuwekeza kwenye Fly Overs kwenye mataa yote.
  3. kuboresha na kupanua barabara hasa vituo amabvyo viko barabarani hasa mf. njia ya Tandare.


MUHIMU: wATANZANIA tunapenda kushabikia mambo bila kuyachunguza na sasa tusubiri tuone jinsi hii mipango 2 isivyo na tija bali danganya toto.

Labda sijakuelewa, maana unaongelea mengi mara flyovers nk, fikiria kwamba kupunguza msongamano si jambo moja, kuna mengi, na hili ni moja wapo ya njia ambazo mataifa mengi yamefanikiwa kisha tunaweza kuanza la pili kama ni kuongeza barabara zaidi au kujenga hizo flyovers.

Umbumbumbu wangu ni hivi:
  • Usafri wa gari moshi una nafasi ya kupunguza wengi ambao wanapenda kutumia magari binafsi
  • Usafiri wa gari moshi utawafikisha haraka watu makazini
  • usfiri wa gari moshi nauli itakuwa nafuu kwa vile hakuna kuunga unga magari kama daladala
  • Usafiri wa gari moshi mtu unapanga unaondoka saa ngapi na kufika kazini saa unayokusudia
  • Usafiri wa gari moshi utashawishi watumia magari kuyaacha nyumbani
  • Usafiri wa gari moshi hakuna usumbufu wa kusubiria traffic lights kwa vile unajiendesha kwa kupita njia huru na kuwahisha watu makazini
Usafiri wa gari moshi unaweza kuua baadhi ya daladala binafsi na kabisa usafri wa magari yaendayo kasi ukikamilika mambo yaweza kuwa tambalare kama majuu vile.
Kinachofanyika ni sawa kama nchi zilizoendelea zilivyofanikisha kupunguza msongamano, kufikisha wafanyakazi makazini on time na kupunguza watumiaji wengi wa magari mjini. Kumbuka wengi wamenunua magari kufikiria watawahi mapema zaidi makazini kumbe ni kinyume chake kuongeza magari zaidi barabara na hivyo kuleta msongamano usio wa lazima.
 
lol jamani hata kama ccm tunaichukia tuwape credit zao pia..big up sana mwakyembe kwa hii ishu ya treni iko safi sana
 
Hana jipya,ana roho ya kunguni. Kaka jifunze kusema asante hata kwa kidogo maana "from little things bigger things grow" Kesho na keshokutwa hayo mawazo yako huenda yakafanyiwa kazi, kwa sasa ungetoa pongezi angalau kidogo kuonesha uzalendo
 
Naona mnamshambulia tu kama Paul Kijoka lakini hamjibu hoja zake, kuna kitu ameongea nakiona, great thinkers wa siku hizi wakoje, shule za kata zimetuharibia watu.
 
Mi naona Heading ya Mada ndo imeshtua sana na mtoa mada alipaswa kusupport juhudi za hawa Mawaziri na hoja zake zikawa ni angalizo lijalo kwa tiba ya Msongamano.
 
Mleta uzi si kweli wanayoyafanya Magufuli na Mwakyembe ni maamuzi yao binafsi kiasi cha kuwaita wahuni. Haya si mawazo yao binafsi!! Huu ni mchakato wa siku nyingi ambao hata Bunge limehusishwa. Iweje leo hawa wawili waonekane ni wahuni kwa kutekeleza mipango ya kitaifa? Kuna mantiki nyingi tu kwenye hoja yako ila kuwaita wahuni hawa mawaziri hujawatendea haki. Hizi point ungezitoa wakati miradi hii inajadiliwa. Vuta subira uone matokeo kama siyo mazuri basi majadilianao yataanza kuhusu nini kifanyike kurekebisha kasoro zitakazojitokeza.

Kwa kuongezea pengine kwa siku za karibuni, kuwe na "park lots" salama kwa ajili ya magari madogo binafsi nje ya jiji kama vile Ubungo, Mwenge, Mbagala, Tabata nk. Watakaoingia na magari madogo katikati ya jiji watozwe kiasi ambacho wataona ni vema kuchukua public transport au la, kulingana na shughuli walizo nazo. Hizi park lots zinaweza zikajengwa na kuendeshwa na sekta binafsi siyo lazima serikali.
TUWAPONGEZE KWA UJASIRI WALIOONYESHA. CHANGAMOTO ZILIKUWA NYINGI NA WAMEZIKABILI VILIVYO. MNYONGE MNYONGENI HAKI YAKE MPENI!!!!:A S thumbs_up:​

angalau mpo mnaojua kuwa huu mpango haukuanzishwa na kina magufuli na mwakyembe.
 
Hata wewe pia hujafanya utafiti wa kutosha......gharama ni sehemu ya utafiti...hujatuambia ni gharama kiasi gani itahitajika kwenye kujenga hizo fly-overs....umeishia kulaumu tu.....kwangu mimi suluhisho ninaona kupunguza magari.....kupunguza shughuli katika jiji la dar....KUHAMISHIA SERIKALI DODOMA ...
 
Kweli vyama vingi vimesababisha watu wawe wabishi na wasio taka kukubari. Mleta mada haueleweki, labda utueleweshe vyema maana naona kama vili ujumbe wako ni wa kuluka haja ndogo na kudumbukia kwenye haja kubwa. Hivi hao viongozi wote ni wapuuzi ila wewe tu ndo mwelevu.
Pale viongozi wanapo fanya jambo jema hata kwa nusu jaribuni kuwapa moyo na sio kupinga kila kitu hata kama hamkijui.
 
Back
Top Bottom