Mbelwa Germano
JF-Expert Member
- May 7, 2011
- 789
- 289
- Kwa kuwa Raisi JK anao uhuru wa kuchagua waziri toka chama cha upinzani (akitaka), na kwa kuwa serikali inaongozwa na sera za CCM chini ya mwamvuli wa katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ambayo ni kinga ya CCM, na iwapo uteuzi huu utafanyika, je CDM watakuwa tayari kuunga mkono?
- Kwa kuwa idadi kubwa ya wabunge wanatoka CCM, Je wabunge hawa wanatuwa tayari kuheshimu maamuzi ya Rais?
- Iwapo CDM watakubaliana na uteuzi huu na Wabunge wa CCM kuheshimu maamuzi ya Raisi,lakini wabunge wa CCM wakaamua kumjengea zengwe Mh.Zitto la kumkwamisha katika maazimio ya wizara, Je CDM watakuwa kwenye nafasi salama?