Mwafrika wa Kike
JF-Expert Member
- Jul 5, 2007
- 5,185
- 56
Bwana unajua watu wengine sijui huwa wanawaza nini maana hata kwa asiekuwa na uelewa mkubwa kila kitu kiko wazi kabisa kuwa CCM si chama cha wote ni chama cha wachache (Chao) kabisa tena hata ufanye nini kama ikiwezekana na roho wanakutoa uhai ili tuu wakae wao, na hao hao wanao watetea mara nyingi hali yao kiuchumi ni mbovu ile mabaya lkn ukikuta wanavo itetea hiyo CCM unabaki kujiuliza hivi huyu kachanganyikiwa???
sasa hivi watz tumeamka fisadi hakatishi
Tuandamane,
Kila sehemu kuna diehards, unajua hata zimbabwe kuna watu hawaoni kuwa ni tatizo kwa kuwa na inflation big tyme, unajua kuna watu hawaoni tatizo kwa maelfu ya wasio na chakula. Katika societies zote watu kama hawa na hata hapa JF wanategemewa kuwepo.
Hii ni moja ya sababu ambayo wengine tuko hapa ili kuwakabili inavyowezekana. Kuzuia mipango yao ya uvurugaji. Kuna watu inawaumiza sana wakiona mafanikio ya JF. Kuna hasira na chuki kubwa toka kwa baadhi ya members hapa. Kuna wamepoteza ulaji kwa sababu ya JF. Usishangae chuki na yote yanayofanyika hapa.
Lakini you know what, as longer as nia ni thabiti hapa ya kuitoa Tanzania toka mikononi mwa mafisadi wasio na haya, mapambano yataendelea hata kama itachukua miaka 27 kama Mandela. Huu ni mwanzo na so far matokeo ni mazuri. Take your popcorn na ufurahie kinachoendelea - explosions!