Katika moja ya vikao vya bunge la Jamhuri ya Muungano TZ, kuna mbunge mwanamke alimfagilia sana E. Lowassa; na pia gazeti moja la kila wiki nchini lilimnukuu mbunge huyo mwanamama kutoka Tanga akisema alipoenda Nigeria aliambiwa na Mtumishi maarufu wa mungu nabiiTB Joshua kwamba mh.Lowassa ndiye rais ajaye wa Tanzania.
Sasa inakuwaje tunasikia katika makundi ndani ya CCM(mafisadi) kundi lake ndilo hutumia fedha kwa kiasi kikubwa ili kupenyeza watu wake kushika nyadhifa mbali mbali ndani ya chama na serikali; huku yeye Lowassa akijiandaa kugombea urais kwa tiketi ya CCM kwa kutumia fedha?
Je, hauamini unabii uliotolewa juu yake na TB Joshua? Kwa nini amsaidie Mungu kukamilisha unabii wake? Au huyo, mbunge mwanamama alikuwa mzushi tu?
Mh. E. Lowassa akiwa Nigeria akishiriki ibada katika SCOAN na mwenye kipaza sauti ni
Nabii TB Joshua mwaka jana.
Sasa inakuwaje tunasikia katika makundi ndani ya CCM(mafisadi) kundi lake ndilo hutumia fedha kwa kiasi kikubwa ili kupenyeza watu wake kushika nyadhifa mbali mbali ndani ya chama na serikali; huku yeye Lowassa akijiandaa kugombea urais kwa tiketi ya CCM kwa kutumia fedha?
Je, hauamini unabii uliotolewa juu yake na TB Joshua? Kwa nini amsaidie Mungu kukamilisha unabii wake? Au huyo, mbunge mwanamama alikuwa mzushi tu?
Mh. E. Lowassa akiwa Nigeria akishiriki ibada katika SCOAN na mwenye kipaza sauti ni
Nabii TB Joshua mwaka jana.