Kupata kura 70 si kazi kwani kwa hesabu zet tayri kuna kura 48, kazi ipo kwenye kupata kura 22.
CCM hata wasipotoa kura hizi bado wabunge wengine wa upinzani (CUF,UDP, TLP na NCCR wanazidi idani hiyo. Sasa issue ni mkakati wa kuwashawishi hao kwani kambi ya Upinzani haina ushirikiano.
Cha msingi ni wananchi kuwashinikiza wabunge wao kupitia njia za mawasiliano zilizopo, na wapigakura wake wafuatilie kuona kama aliwasikiliza kwani watakaounga hoja hii Mkono tutawajua kwa majina.
Tatizo nilionalo mimi ni ile 51% ya kura kama hoja ikipitishwa. Hata hivyo wakulaumiwa ni watanzania, kwani wao ndio waliowachagua wabunge wengi wa CCM, na hili litakuwa ni fundisho tosha
Hawathubutu,hawawezi na wameshindwa sasa wanarudi nyuma.ccm oyeee.....!
Baada ya mh. Zitto kutoa azimio la wabunge kutia sahii kwa ajili kutokuwa na imani na PM, ndugu waJF tujua fika wabunge wa chadema wote 49 watatia sahihi zao. Je kuna wabunge gani tunaona kuwa huenda nao wakafanya hivyo.?
Tuwataje kwa majina na chama wanachotoka.
1. Magedelena Sakaya (cuf).
2. Godfrey Zambi (ccm).
3. Samuel Sitta (ccm)
4. Harison Mwakyembe(ccm) 5. Agustino Mrema (TLP).
6........
7.........
8....
Mkuu mtoa mada hivi kwa hali iliyotokea leo pale mjengoni unadhani Filikunjombe na Zambi bado wapo CCM?
ivi nyie mnajua adhabu ya uhaini??nyie mpeni kichwa tu uyo zitto mtamponza.
Mawaziri wetu wajue kujiwajibisha ni aibu na tuhuma hizo bado wanangangania madaraka. Dawa ni hiyo kuwalazimisha maana jk ameshindwa anawaonea haya.
hii ndoa ya cuf na ccm sidhani kama wana-cuf wanaiunga mkono, hio ilifosiwa na viongozi fulani fulani wa cuf kutokana na uroho wa madaraka. Yaani wameingia ndoa wakati hao viongozi ndo walisababisha hadi wanachama kibao wakafa wakati ule wa machafuko huku hao wakikimbiza roho zao.
Kwanza mimi huwa sipendi kuita hii ni ndoa, ktk hili suala naona kama vile cuf wamebakwa na ccm na hatimaye wakaozeshwa ndoa ya mkeka.