nguvumali
JF-Expert Member
- Sep 3, 2009
- 4,923
- 1,325
Kama kweli Rais Kikwete amefanya mengi mazuri , hadi kupigiwa chapuo la kupewa tena uongozi wa juu wa Taifa hili, mi najiuliza gharama zote hizi wanazotumia za nini ?nayatizama mabango njiani hapa Mwanza, na juzi nilikua Mkoani Kagera wameanza kubandika bado sipati picha, jana nikasikia habari kuwa wametumia 1.5Bn kwa gharama ya mabango tu....?bado kuna Tshirt, kofia, chupi na opener za vinywaji.na hakika kila mtu hapa Tz anamjua JK kwa sura, sauti, miondoko na hata mambo yake mengine. Je kuna mantiki yoyote ya kumuuza kwa nguvu Hivyo ama ni ile hadithi Kibaya cha jitembeza.?Bado nafikiri.