Kama kampuni za simu hazilipi kodi inavyotakiwa tufanyeje sisi wananchi?

harakat

JF-Expert Member
Jul 4, 2011
2,889
1,346
“Kampuni nyingi za simu za mkononi hazilipi kodi kama inavyotakiwa, hivyo tunatakiwa kutafuta njia maalumu za kuzibana ili ziweze kulipa kodi kama inavyotakiwa,” alisema Zitto.
Mbunge huyo wa Kigoma Kaskazini (Chadema) na Mwenyekiti wa Kamati ya Bunge ya Hesabu za Serikali (POAC), alitaja kipaumbele kingine kilichopendekezwa na upinzani katika Bajeti yake kuwa ni kuhakikisha Taifa linajiandaa kuwa na uchumi ambao utategemea rasilimali nyingine ikiwemo gesi.
“Tafiti zinaonyesha kwamba tuna gesi nyingi nchini sasa tunatakiwa kujiandaa namna ya kuiendesha rasilimali hiyo, ikiwamo kutunga sheria ya gesi,” alisema na kuongeza:


Hii kauli ya Mh.kabwe nashindwa kuelewa hapa badala ya kuhakikisha wanalipa kodi inavyotakiwa tunaliongelea ktk
nadharia tu hili ni suala ambalo si tofauti sana na suala la madini ,uzalishaji wa umeme na mabo mengine ya kusafiisha wanyama nawengine kudiriki hata kuwawinda faru tena wenye ulinzi kuliko mimi Mtz .
sasa tujiulize hawa viongozi wetu ni kwamba toka wanasajili hizi kampuni hawajui kwamba wanatakiwa kuwa wanalipa kodi?
Mbona wafanyakazi wa serikali na mashirika mengine kinachokatwa kwanza ni kodi halafu mambo mengine ndio yanafuata?
Haya makampuni sio tu ya simu hata ya uwindaji yaani utasikia story nyingi sana mara wanawinda kwa bei nafuu sana ukilinganisha na sehemu nyingine kwa nini isifanyike fisibility study kujua kwamba ni nini kifanyike na wakati gani?
nawasilisha...................................
 
0 Reactions
Reply
Back
Top Bottom