EJM_
JF-Expert Member
- Jul 8, 2011
- 3,836
- 2,091
Mi napata tabu kidogo, nimesikiliza MIKAKATI/MIPANGO NA MBIO nyingi ambazo zilikuwa na lengo la kutatua tatizo la umeme ifikapo mwaka 2015 (Miaka minne kutoka sasa) lakini juzi hapa waziri mkuu Mh. Mizengo Pinda amesema serikali inaingia kazini ili kufikia mwezi December mwaka huu tatizo la umeme liwe historia sasa mi najiuliza kidogo,
- Je Serikali ilikuwa na nia ya dhati kutatua tatizo la umeme?
- Kama wameshindwa kutatua tatizo kwa miaka zaidi ya kumi na saba (mgao wa kwanza wa umeme ulikuwa 1994) je wataweza kwa miezi mitatu?
- Nani anafaidika na matatizo ya umeme hapa nchini?