Kama hii ni Tanzania; Basi tumelaaniwa, na aliyetulaani kafa

Kwa hay a wanaoshangilia serikali iliyo madarakani wanamatatizo.haya ndo maisha bora tuliyoahidiwa
 
Ni kweli Mkuu nilishaiweka article hii miaka ya nyuma hapa jamvini. Kinachofanyoka kuhusu rasilimali za Tanzania kinasikitisha sana na kutisha pia. Hakuna ncho yoyote duniani ambayo inaweza kuwaruhusu "wawekezaji" kuchukua almost $12 billion ya mapato yatokanayo na dhahabu ya Tanzania na kuiachia nchi $497 million tu. Huu ni wizi mkubwa sana lakini ndiyo hivyo mafisadi wameshafungua bank accounts nchi za nje na huwekewa mabilioni ya pesa na makampuni hayo hivyo mafisadi huangalia pembeni huku wizi mkubwa dhidi ya rasilimali za Tanzania ukiendelea.

DHAIFU katika kampeni zake za 2005 za Urais alidai kwamba Watanzania tunalalamikia sana mikataba ya uchimbaji wa madini kwamba haina maslahi kwa Watanzania hivyo akiwa rais angeiangalia upya ili kuhakikisha inabadilishwa ili kuinufaisha Tanzania, tangu alipoingia hakuna jipya alilolifanya zaidi ya kuongeza royalties toka 3% to 4%!!! Walitaka kuongeza hadi 5% "wawekezaji" wakagoma.

Muhongo alipoingia Nishati alitoa kauli kwamba "wawekezaji" wote katika sekta ya madini ambao wapo nchini kwa miaka mitano au zaidi watatozwa 30% ya mapato yao kama kodi asiyetaka afunge virago. Hili nalo limekufa kimya kimya baada ya "wawekezaji" kuligomea.
 
na bado mkuu wa kaya ana wafagilia wawwekezaji,JK ni janga la taifa,sehemu yeyote yenye hizi natural resource kuna mapigano,dhuluma na unyanyasaji
 
Ni kweli Mkuu nilishaiweka article hii miaka ya nyuma hapa jamvini. Kinachofanyoka kuhusu rasilimali za Tanzania kinasikitisha sana na kutisha pia. Hakuna ncho yoyote duniani ambayo inaweza kuwaruhusu "wawekezaji" kuchukua almost $12 billion ya mapato yatokanayo na dhahabu ya Tanzania na kuiachia nchi $497 million tu. Huu ni wizi mkubwa sana lakini ndiyo hivyo mafisadi wameshafungua bank accounts nchi za nje na huwekewa mabilioni ya pesa na makampuni hayo hivyo mafisadi huangalia pembeni huku wizi mkubwa dhidi ya rasilimali za Tanzania ukiendelea.

DHAIFU katika kampeni zake za 2005 za Urais alidai kwamba Watanzania tunalalamikia sana mikataba ya uchimbaji wa madini kwamba haina maslahi kwa Watanzania hivyo akiwa rais angeiangalia upya ili kuhakikisha inabadilishwa ili kuinufaisha Tanzania, tangu alipoingia hakuna jipya alilolifanya zaidi ya kuongeza royalties toka 3% to 4%!!! Walitaka kuongeza hadi 5% "wawekezaji" wakagoma.

Muhongo alipoingia Nishati alitoa kauli kwamba "wawekezaji" wote katika sekta ya madini ambao wapo nchini kwa miaka mitano au zaidi watatozwa 30% ya mapato yao kama kodi asiyetaka afunge virago. Hili nalo limekufa kimya kimya baada ya "wawekezaji" kuligomea.

BAK wakulaumiwa ni watanzania wenyewe sababu ikifika 2015 wakipewa kanga na kofia basi kura zao watawapa magamba. Tunajiroga wenyewe na hakuna sababu ya kulalama
 
  • Thanks
Reactions: BAK
Hilo ni kweli Mkuu VUVUZELA, lakini pia tusisahau Tume ya uchaguzi ya Magamba ambayo huruhusu ukiukwaji wa kila aina wa taratibu za uchaguzi ikiwemo kutoa rushwa, kunyanyasa wafuasi na wagombea hasa wa CHADEMA bila kusahau uchakachuaji mkubwa wa matokeo ya uchaguzi katika majimbo mbali mbali.

BAK wakulaumiwa ni watanzania wenyewe sababu ikifika 2015 wakipewa kanga na kofia basi kura zao watawapa magamba. Tunajiroga wenyewe na hakuna sababu ya kulalama
 
Last edited by a moderator:
Aliyeilaani tz wala hajafa,yu hai milele yote,ni ujinga wetu tu na kufuata maamuzi ya pamoja ya kijinga.wacha nikurudishe nyuma kosa lilikotokea ingawa nina hakika sio wote walipo janvini watakubaliana na mimi,miaka hiyo tz ilikuwa na uhusiano na Israel wakahusika kutuanzishia hata jeshi la kujenga taifa,mtafaruku na vita vilipotokea mashariki ya kati kati ya israel na waparestina wakuu wa wa nchi za kiafrika wakati huo OAU wakakutana wakawa na maamuzi ya pamoja ya kuilaani israel Nyerere akiwepo kwenye huo mkutano,akaenda mbali zaidi akavunja uhusiano wa kibalozi, aaah!!kosa kubwa rudi kwenye Biblia soma vizuri usiingie kanisani na kutoka tu Ailaanie israel na Mungu atamlaani kwishaa,haijalishi utayakubali au la ni muislam au mkristo dawa ni kutubu tena kwa machozi kujutia kosa tulilofanya kisha turejeshe uhusiano na israel,maana hata leo hii ukiulizwa kwa nini hatuna ubalozi na israel kuna mtu mwenye sababu zenye mashiko au ni bla-bla tu.kama yuko member hapa janvini na anafanyia wizara ya mambo ya nje atwambie.


Huu ndio ugonjwa mbaya unaotukabili Wtza tunaohusisha kila kitu na Dini!
Bible iko na mistari mingi, kwanini tunang'ang'ania huu wa kutukuza ISRAELI tuu?

Mimi naamini maamuzi ya mwalimu yaliongozwa na imani yake ya kikristo, inayojali ubinadamu na utu, hasa ukizingatia kua miongoni mwa wapalestina waliokua wakiuwawa ni ndugu zake ktk imani yaani WAKRISTO!

mwalimu ni mtu aliyejua dini yake vizuri na hakurupuki kama wewe, na ndio maana sisi WAKATOLIKI tunataka kumtangaza mtakatifu!

Suala la ISRAELI kwa kwel,i bado lina utata na kama ailaanie ndio analaaniwa basi ingelaaniwa UJERUMANI kwa mauwaji ya wayahudi 600,00,00! lkn. sasa ndio 'european economic giant!

Sikatai maandiko ila bado kuna maswali mwengi kuhusiana na ISRELI hayajajibiwa na viongozi wetu wa dini:

1)Tunaposema taifa la Mungu, tunaikusudia ISRAELI ya kale au hii political ISRAELI? israeli ya leo, ambayo haijali misingi ya kidini na ndio maana ukiwafanyia mchezo hata kama ni MKRISTO wanakutandika!

2)ISRAELI ya leo imeundwa na WAYAHUDI, WAPALESTINA ( WAKRISTO na WAISLAMU) sisi tunailenga ipi?

Ndugu yangu, hakuna uhusino kati ya kutukuza ISRAELI na maendeo ya nchi, wao wenyewe wanachapa kazi usiku na mchana... sula la kutukuza na kutokutukuza ni la kiimani zaidi!

Zipo nchi ambazo kila siku wanaitukuza ISRAELI na hawajawahi kuvunja uhusiano wa kibalozi na ISRAELI lkn. wana umaskini wa kufa mtu na migogoro kama na mfano wake ni CONGO nk.!

After all ISRAELI ni jeuri, walishaambiwa waje kufungua ubalozi wakasema kwa sasa hakuna haja na badala yake watawakilishwa na balozi wao aliyepo KENYA!.. SASA TUAFANYAJE?
 
Wananchi wangeweza kuishi katka hali yao ya kawaida pasipo adha hii. Kama tungeamini kati Strong sustainability! Hapa ndipo ninapotambua Hekima na Busara za JK Nyerere!
 
Mkowapi Lumumba members kama kina ritz,ifweelo,simiyu yetu nk mje muone udhalimu wenu. Shet.a.ni wakubwa nyie
 
Duh! Ama kweli kwa hakika hii ni laana.
Lakini hata hivyo wazungu wanathubutu je kuvuna rasilimali za masikini namna hii. Wanaweza kuufurahia utajiri wao katikati ya jirani zao wanaokufa njaa? Wakifanya hivyo tatizo lao ni kubwa kuliko letu.

Eti nini? Bora mzungu kuliko mwuza madawa ya kulevya asiyejali kuwafanya watoto wa jirani yake mataahira huku yeye akifurahia kila kitu chema hapa duniani isipokuwa amani ya kweli.

Sent from my BlackBerry 9860 using JamiiForums
 
alafu JAY2da4 acha mambo yako hizo picha sio west africa kweli? tanzania hii ya mwigulu na wenzake ndo kuna mambo haya! hivi mgombea wa chama flani anaombaje kura kwa hali hii,
 
Back
Top Bottom