Pascal Mayalla
Platinum Member
- Sep 22, 2008
- 50,337
- 113,180
Wanabodi,
Haya ninayoyaandika ni maoni yangu binafsi ya nilichokishuhudia na nilicho ambiwa kuhusu kampeni za CCM, Zanzibar, kama ni kweli, basi October 31, CCM bye bye Zanzibar, wajiandae kuwa chama cha upinzani katika serikali mpya ya mseto.
Leo nilipata kajinafasi kwenye muda wangu, hivyo nikaamua kutia timu Zanzibar.
Kama moja ya viashiria vya ushindi ni wingi wa mabango, CCM imeshashinda Zanzibar kwa asilimia 90% na asilimia 10% iliyobaki ndio vyama vingine kwa jinsi mji wa Zanzibar ulivyoshehenezwa mabango ya CCM.
Nimehudhuria kampeni ya CCM pale Kibanda Maiti ambapo mgeni rasmi ni JK mwenyewe. Tangu kuanza kwa kampeni, leo ndio nimebahatika kuhudhuria kampeni za CCM akiwemo JK mwenyewe ndani ya nyumba.
Nimehudhuria kampeni za urais Zanzibar toka uchaguzi wa 1995, 2000, 2005 na sasa huu wa 2010, sijawahi kuona umati mkubwa wa watu kama niliuona leo hapo Kibanda Maiti. Hivyo tathmini yangu binafsi, kama ushindi ni umati wa watu, CCM imeshinda tena kwa
asilimia 90% tena.
Sambamba na umati huo, kwa haraka haraka unaweza kudhani ndio umati wa wananchi, la hasha!, asilimia 90% ya umati huu, ni ama wanachama wa CCM ama washabiki wa CCM
na asilimia 10% ndio wanachi wa kawaida. Asilimia hii nimeipiga kufuatia mavazi, t-shirt, kofia, kanga na scalf.
Uwanja wa Kibanda Maiti ukazungukwa na magari zile Chai Maharage za Zanzibar, mabasi na malori yaani ilikuwa ni vurugu mechi ya parking.
Nikashuhudia wasanii mbali mbali wakipanda jukwaani wakiwemo ze comedy original, huku waandishi wa habari, tena waheshimiwa sana 'akiwemo mkuu wa wilaya' na wale wa magogoni, wamepiga ama sare za CCM ama "Press Kikwete 2010". Wajameni wanahabari!, hizi njaa zitatuua!, sikatai kufadhiliwa viwalo, ndio mmenunuliwa kabisa?.
Ndipo nikafanya kajidodoso kadogo bila hojaji.
Matokeo ya dodoso hiyo ndiyo yaliyopelekea kutoa opinion yangu kuwa baada ya October 31, 2010, CCM Zanzibar ni bye bye.
Matokeo ya dodoso hiyo, yanafuatia hivi punde!
Update
Kwanza samahani sana wanabodi, jana nilishindwa kumaliza, nikitegemea ningemalizia usiku kabla sijajala, sasa wengine wetu tukisafiri ndio hivyo tena, kumbe unaweza ukamalizia kazi nyakati za usiku ukiwa home, sio ukiwa safari, Zanzibar nako!...
Matokeo ya Dodoso ni haya.
1.Nilimuuliza mwanahabari fulani aliyehudhuria uzinduzi wa kampeni za CCM na CUF kisiwani Unguja na jana alikuwepo kuhusu wingi wa watu, alikiri kuwa CCM kwa Unguja imeifunika CUF. Hivyo nikafikia conclusion 1. Kama ushindi ni wingi wa watu, basi CCM itashinda.
2. Nikamuuliza hayo magari yalitapakaa hapo, akanijibu, ndio yamesomba watu toka kila kona ya kisiwa cha Unguja, yaani CCM imekodisha magari yote bila kujali ni ya nani, na kugawa fulana kwa wananchi wote bila kujali ushabiki wao, na kwa chini chini nasikia pia wameshikishwa na kidogo dogo cha nauli.
3. Hivyo kuna uwezekano uwingi ule wa watu, sio tuu ni ushabiki kwa CCM au mapenzi yako kwa CCM, bali ni usafiri bute, fulana bure na kidogo dogo lakini siku ya kura, watapeleka yalipo mapenzi yao!.
4. Aliniambia hata mikutano ya CUF, watu hujitokeza kwa wingi kama unavyoona mkutano wa CCM, tofauti ya CUF na CCM, ni kuwa wale washabiki wa CUF hawapewi nauli, hujigharimia kwa mifuko yao, hawapewi fulana na kofia za bure, wala hawalipwi sentano toka CUF ili wahudhurie, hivyo wanahudhuria mikutano ya CUF bila shinikizo lolote. Hawa sasa ndio washabiki wa ukweli wakati wenzao ni washabiki maandazi!.
5. Kama ni kweli CCM imekodisha yale magari yote niliyoyaona jana, kama ni kweli CCM inagawa fulana, kofia, kanga na scuf kwa yoyote, na kama ni kweli, CCM inagawa kidogo dogo kwa hao wahudhuriaji mikutano yake ya kampeni kwa maoni yangu, hii inaweza kuwa ni kiashiria tosha kuwa October 31 kuna uwezekano mkubwa kwa CCM ndio Bye Bye Zanzibar!.
Angalizo: Washabiki wa CCM msinitolee mimacho, haya ni maoni yangu tuu kwa kutumia freedom of expression bila kuingilia mchakato wa uchaguzi, kwani kama hizo hoja ni za uwongo, si mtashinda kwa kishindo! hivyo hakuna haja ya kutoleana lugha kali kali humu!
Washabiki wa CUF pia msijifariji sana na mashabiki wenu ambao ni genuine, kunauwezekano hayo makundi yenu ni washabiki tuu na sio wapiga kura, hivyo jiandaeni kwa matokeo yoyote, sio mnapata kipigo halali na bado mnaendelea kulia lia.
Haya ninayoyaandika ni maoni yangu binafsi ya nilichokishuhudia na nilicho ambiwa kuhusu kampeni za CCM, Zanzibar, kama ni kweli, basi October 31, CCM bye bye Zanzibar, wajiandae kuwa chama cha upinzani katika serikali mpya ya mseto.
Leo nilipata kajinafasi kwenye muda wangu, hivyo nikaamua kutia timu Zanzibar.
Kama moja ya viashiria vya ushindi ni wingi wa mabango, CCM imeshashinda Zanzibar kwa asilimia 90% na asilimia 10% iliyobaki ndio vyama vingine kwa jinsi mji wa Zanzibar ulivyoshehenezwa mabango ya CCM.
Nimehudhuria kampeni ya CCM pale Kibanda Maiti ambapo mgeni rasmi ni JK mwenyewe. Tangu kuanza kwa kampeni, leo ndio nimebahatika kuhudhuria kampeni za CCM akiwemo JK mwenyewe ndani ya nyumba.
Nimehudhuria kampeni za urais Zanzibar toka uchaguzi wa 1995, 2000, 2005 na sasa huu wa 2010, sijawahi kuona umati mkubwa wa watu kama niliuona leo hapo Kibanda Maiti. Hivyo tathmini yangu binafsi, kama ushindi ni umati wa watu, CCM imeshinda tena kwa
asilimia 90% tena.
Sambamba na umati huo, kwa haraka haraka unaweza kudhani ndio umati wa wananchi, la hasha!, asilimia 90% ya umati huu, ni ama wanachama wa CCM ama washabiki wa CCM
na asilimia 10% ndio wanachi wa kawaida. Asilimia hii nimeipiga kufuatia mavazi, t-shirt, kofia, kanga na scalf.
Uwanja wa Kibanda Maiti ukazungukwa na magari zile Chai Maharage za Zanzibar, mabasi na malori yaani ilikuwa ni vurugu mechi ya parking.
Nikashuhudia wasanii mbali mbali wakipanda jukwaani wakiwemo ze comedy original, huku waandishi wa habari, tena waheshimiwa sana 'akiwemo mkuu wa wilaya' na wale wa magogoni, wamepiga ama sare za CCM ama "Press Kikwete 2010". Wajameni wanahabari!, hizi njaa zitatuua!, sikatai kufadhiliwa viwalo, ndio mmenunuliwa kabisa?.
Ndipo nikafanya kajidodoso kadogo bila hojaji.
Matokeo ya dodoso hiyo ndiyo yaliyopelekea kutoa opinion yangu kuwa baada ya October 31, 2010, CCM Zanzibar ni bye bye.
Matokeo ya dodoso hiyo, yanafuatia hivi punde!
Update
Kwanza samahani sana wanabodi, jana nilishindwa kumaliza, nikitegemea ningemalizia usiku kabla sijajala, sasa wengine wetu tukisafiri ndio hivyo tena, kumbe unaweza ukamalizia kazi nyakati za usiku ukiwa home, sio ukiwa safari, Zanzibar nako!...
Matokeo ya Dodoso ni haya.
1.Nilimuuliza mwanahabari fulani aliyehudhuria uzinduzi wa kampeni za CCM na CUF kisiwani Unguja na jana alikuwepo kuhusu wingi wa watu, alikiri kuwa CCM kwa Unguja imeifunika CUF. Hivyo nikafikia conclusion 1. Kama ushindi ni wingi wa watu, basi CCM itashinda.
2. Nikamuuliza hayo magari yalitapakaa hapo, akanijibu, ndio yamesomba watu toka kila kona ya kisiwa cha Unguja, yaani CCM imekodisha magari yote bila kujali ni ya nani, na kugawa fulana kwa wananchi wote bila kujali ushabiki wao, na kwa chini chini nasikia pia wameshikishwa na kidogo dogo cha nauli.
3. Hivyo kuna uwezekano uwingi ule wa watu, sio tuu ni ushabiki kwa CCM au mapenzi yako kwa CCM, bali ni usafiri bute, fulana bure na kidogo dogo lakini siku ya kura, watapeleka yalipo mapenzi yao!.
4. Aliniambia hata mikutano ya CUF, watu hujitokeza kwa wingi kama unavyoona mkutano wa CCM, tofauti ya CUF na CCM, ni kuwa wale washabiki wa CUF hawapewi nauli, hujigharimia kwa mifuko yao, hawapewi fulana na kofia za bure, wala hawalipwi sentano toka CUF ili wahudhurie, hivyo wanahudhuria mikutano ya CUF bila shinikizo lolote. Hawa sasa ndio washabiki wa ukweli wakati wenzao ni washabiki maandazi!.
5. Kama ni kweli CCM imekodisha yale magari yote niliyoyaona jana, kama ni kweli CCM inagawa fulana, kofia, kanga na scuf kwa yoyote, na kama ni kweli, CCM inagawa kidogo dogo kwa hao wahudhuriaji mikutano yake ya kampeni kwa maoni yangu, hii inaweza kuwa ni kiashiria tosha kuwa October 31 kuna uwezekano mkubwa kwa CCM ndio Bye Bye Zanzibar!.
Angalizo: Washabiki wa CCM msinitolee mimacho, haya ni maoni yangu tuu kwa kutumia freedom of expression bila kuingilia mchakato wa uchaguzi, kwani kama hizo hoja ni za uwongo, si mtashinda kwa kishindo! hivyo hakuna haja ya kutoleana lugha kali kali humu!
Washabiki wa CUF pia msijifariji sana na mashabiki wenu ambao ni genuine, kunauwezekano hayo makundi yenu ni washabiki tuu na sio wapiga kura, hivyo jiandaeni kwa matokeo yoyote, sio mnapata kipigo halali na bado mnaendelea kulia lia.