Kama hii ni kweli, CCM Zanzibar ndiyo Bye Bye?

Pascal Mayalla

Platinum Member
Sep 22, 2008
50,337
113,180
Wanabodi,
Haya ninayoyaandika ni maoni yangu binafsi ya nilichokishuhudia na nilicho ambiwa kuhusu kampeni za CCM, Zanzibar, kama ni kweli, basi October 31, CCM bye bye Zanzibar, wajiandae kuwa chama cha upinzani katika serikali mpya ya mseto.

Leo nilipata kajinafasi kwenye muda wangu, hivyo nikaamua kutia timu Zanzibar.

Kama moja ya viashiria vya ushindi ni wingi wa mabango, CCM imeshashinda Zanzibar kwa asilimia 90% na asilimia 10% iliyobaki ndio vyama vingine kwa jinsi mji wa Zanzibar ulivyoshehenezwa mabango ya CCM.

Nimehudhuria kampeni ya CCM pale Kibanda Maiti ambapo mgeni rasmi ni JK mwenyewe. Tangu kuanza kwa kampeni, leo ndio nimebahatika kuhudhuria kampeni za CCM akiwemo JK mwenyewe ndani ya nyumba.

Nimehudhuria kampeni za urais Zanzibar toka uchaguzi wa 1995, 2000, 2005 na sasa huu wa 2010, sijawahi kuona umati mkubwa wa watu kama niliuona leo hapo Kibanda Maiti. Hivyo tathmini yangu binafsi, kama ushindi ni umati wa watu, CCM imeshinda tena kwa
asilimia 90% tena.

Sambamba na umati huo, kwa haraka haraka unaweza kudhani ndio umati wa wananchi, la hasha!, asilimia 90% ya umati huu, ni ama wanachama wa CCM ama washabiki wa CCM
na asilimia 10% ndio wanachi wa kawaida. Asilimia hii nimeipiga kufuatia mavazi, t-shirt, kofia, kanga na scalf.

Uwanja wa Kibanda Maiti ukazungukwa na magari zile Chai Maharage za Zanzibar, mabasi na malori yaani ilikuwa ni vurugu mechi ya parking.

Nikashuhudia wasanii mbali mbali wakipanda jukwaani wakiwemo ze comedy original, huku waandishi wa habari, tena waheshimiwa sana 'akiwemo mkuu wa wilaya' na wale wa magogoni, wamepiga ama sare za CCM ama "Press Kikwete 2010". Wajameni wanahabari!, hizi njaa zitatuua!, sikatai kufadhiliwa viwalo, ndio mmenunuliwa kabisa?.

Ndipo nikafanya kajidodoso kadogo bila hojaji.

Matokeo ya dodoso hiyo ndiyo yaliyopelekea kutoa opinion yangu kuwa baada ya October 31, 2010, CCM Zanzibar ni bye bye.

Matokeo ya dodoso hiyo, yanafuatia hivi punde!
Update
Kwanza samahani sana wanabodi, jana nilishindwa kumaliza, nikitegemea ningemalizia usiku kabla sijajala, sasa wengine wetu tukisafiri ndio hivyo tena, kumbe unaweza ukamalizia kazi nyakati za usiku ukiwa home, sio ukiwa safari, Zanzibar nako!...

Matokeo ya Dodoso ni haya.
1.Nilimuuliza mwanahabari fulani aliyehudhuria uzinduzi wa kampeni za CCM na CUF kisiwani Unguja na jana alikuwepo kuhusu wingi wa watu, alikiri kuwa CCM kwa Unguja imeifunika CUF. Hivyo nikafikia conclusion 1. Kama ushindi ni wingi wa watu, basi CCM itashinda.
2. Nikamuuliza hayo magari yalitapakaa hapo, akanijibu, ndio yamesomba watu toka kila kona ya kisiwa cha Unguja, yaani CCM imekodisha magari yote bila kujali ni ya nani, na kugawa fulana kwa wananchi wote bila kujali ushabiki wao, na kwa chini chini nasikia pia wameshikishwa na kidogo dogo cha nauli.
3. Hivyo kuna uwezekano uwingi ule wa watu, sio tuu ni ushabiki kwa CCM au mapenzi yako kwa CCM, bali ni usafiri bute, fulana bure na kidogo dogo lakini siku ya kura, watapeleka yalipo mapenzi yao!.
4. Aliniambia hata mikutano ya CUF, watu hujitokeza kwa wingi kama unavyoona mkutano wa CCM, tofauti ya CUF na CCM, ni kuwa wale washabiki wa CUF hawapewi nauli, hujigharimia kwa mifuko yao, hawapewi fulana na kofia za bure, wala hawalipwi sentano toka CUF ili wahudhurie, hivyo wanahudhuria mikutano ya CUF bila shinikizo lolote. Hawa sasa ndio washabiki wa ukweli wakati wenzao ni washabiki maandazi!.
5. Kama ni kweli CCM imekodisha yale magari yote niliyoyaona jana, kama ni kweli CCM inagawa fulana, kofia, kanga na scuf kwa yoyote, na kama ni kweli, CCM inagawa kidogo dogo kwa hao wahudhuriaji mikutano yake ya kampeni kwa maoni yangu, hii inaweza kuwa ni kiashiria tosha kuwa October 31 kuna uwezekano mkubwa kwa CCM ndio Bye Bye Zanzibar!.

Angalizo: Washabiki wa CCM msinitolee mimacho, haya ni maoni yangu tuu kwa kutumia freedom of expression bila kuingilia mchakato wa uchaguzi, kwani kama hizo hoja ni za uwongo, si mtashinda kwa kishindo! hivyo hakuna haja ya kutoleana lugha kali kali humu!

Washabiki wa CUF pia msijifariji sana na mashabiki wenu ambao ni genuine, kunauwezekano hayo makundi yenu ni washabiki tuu na sio wapiga kura, hivyo jiandaeni kwa matokeo yoyote, sio mnapata kipigo halali na bado mnaendelea kulia lia.
 
Lete habari Pasco lete habari, nacho fahamu mimi, Dr Shein hana ubavu wa kushindana na Seif hata siku moja.
 
Zanzibar? Uchaguzi wao lini maaana uko mshindi na mshindwa ni serikali moja. Yaani ni kwamba hakuna upinzani..coalition gvt...Democrasia imechakachuliwa
 
Nawashauri CUF ambao wanategemea serikali ya Mseto watambue tu kwamba huku Bara Chadema anachukua nchi sasa huo Mseto sijui ndio utakuwa shubiri.. Ni bora kabisa CUF wajiandae kuongoza Zanzibar kwa ushirika waliopewa na Chadema kuliko kuunda serikali ya mseto na chama ambacho kitashindwa bara. Wazanzibar wamecheza tombola na hakika wana wasiwasi mkubwa baada ya kuweka muafaka ambao hauna afueni kwao.

Mwisho, Dr.Slaa tinga Zanzibar na uwafahamishe Wazanzibar, Chadema ina wapa offer gani!..
 
Pasco mbona umekimbia...njooo uwaambie CCM kuwa chama chao kimeshakufa kule Zanzibar kinasubiri Oktoba 31 kutimiza ada tu!
Naona sasa hata Dr. Sheni anaona uvivu kufanya kampeni...unategemea nini wakati meneja wa kampeni CCM-Z'bar anakuwa Hafidh Ali Tahiri hata darasa la watu wazima hakusoma?
 
"unategemea nini wakati meneja wa kampeni CCM-Z'bar anakuwa Hafidh Ali Tahiri hata darasa la watu wazima hakusoma?"
Duuuh nackia mawaziri wengi kule walowekwa na brazameni Karume ni vihiyo na karume mpaka leo anahangaika na Open university kwa miaka 10 sasa
 
Nawashauri CUF ambao wanategemea serikali ya Mseto watambue tu kwamba huku Bara Chadema anachukua nchi sasa huo Mseto sijui ndio utakuwa shubiri.. Ni bora kabisa CUF wajiandae kuongoza Zanzibar kwa ushirika waliopewa na Chadema kuliko kuunda serikali ya mseto na chama ambacho kitashindwa bara. Wazanzibar wamecheza tombola na hakika wana wasiwasi mkubwa baada ya kuweka muafaka ambao hauna afueni kwao.

Mwisho, Dr.Slaa tinga Zanzibar na uwafahamishe Wazanzibar, Chadema ina wapa offer gani!..
Mkuu mkandara,
Naona kama huelewi kwa nini CUF wamekubali serikali ya mseto. Ujuwe CUF haingekuwa na haja ya kukubali kuunda serikali ya mseto kama uchaguzi Zanzibar ungekuwa uhuru na haki na bila ya vurugu na mbinu chafu za CCM.

Ukumbuke kuwa chaguzi zote CCM imeiba kura na matokeo na kusababisha umwagaji mkubwa wa damu. Ukumbuke wao ndiwo wenye dola na vyombo vyake, wao ndiyo waliouwa watu, wao ndiyo waliosababisha wakimbizi (shimoni Mombasa-Kenya), wao ndiyo waliochochea migawanyiko ya U-Pemba na U-Unguja, wao ndiyo waliokuwa tayari kufanya chochote mradi maamuzi ya wananchi yapinduliwe.

CUF, kwa kuona hayo na kutafakari vizuri hiyo hali wameona wabadilishe mbinu ya mapambano, wameona kuwa CCM ni vin'gan'ganizi wa madaraka na hawatakubali kushindwa na wapo tayari kumwaga damu (kama una doubt nukta hii jiulize kwanini JWTZ litowe vitisho katika uchaguzi huu ambao CCM wamekabiliwa na hali ya upinzani usiotabirika?).

Kinachofanywa na CUF ni kuwa-assimilate CCM katika serikali ya pamoja ili kupoza joto la kushindwa na kidogo kidogo watazowea na mwishowe watakubali kuwa demokrasia si ugomvi.

Wazanzibar hawana hofu na serikali ya mseto, siku zote mabadiliko ya system iliyooza kwa mda mrefu ni faraja kwa wananchi. Wenzetu Kenya wameondowa system mbovu kwanza na mpaka sasa wamepiga hatuwa kubwa mpaka kubadilisha katiba ukiwatazama kimaendeleo wapo mbali hasa huku wakiwa wamepitwa na Tanzania kwa rasilimali nyingi zisizowafaidisha wananchi wake.

Kama wao hawakuwa na hofu kufanya mabadiliko hayo kwanini Wazanzibari wawe na hofu.
Ukiishi kuamini kuwa bila ya CCM nchi itayumba...ujuwe umasikini, maradhi na ujinga havitapunguwa hata siku moja...!

 
Mkuu mkandara,
Naona kama huelewi kwa nini CUF wamekubali serikali ya mseto. Ujuwe CUF haingekuwa na haja ya kukubali kuunda serikali ya mseto kama uchaguzi Zanzibar ungekuwa uhuru na haki na bila ya vurugu na mbinu chafu za CCM.

Ukumbuke kuwa chaguzi zote CCM imeiba kura na matokeo na kusababisha umwagaji mkubwa wa damu. Ukumbuke wao ndiwo wenye dola na vyombo vyake, wao ndiyo waliouwa watu, wao ndiyo waliosababisha wakimbizi (shimoni Mombasa-Kenya), wao ndiyo waliochochea migawanyiko ya U-Pemba na U-Unguja, wao ndiyo waliokuwa tayari kufanya chochote mradi maamuzi ya wananchi yapinduliwe.

CUF, kwa kuona hayo na kutafakari vizuri hiyo hali wameona wabadilishe mbinu ya mapambano, wameona kuwa CCM ni vin'gan'ganizi wa madaraka na hawatakubali kushindwa na wapo tayari kumwaga damu (kama una doubt nukta hii jiulize kwanini JWTZ litowe vitisho katika uchaguzi huu ambao CCM wamekabiliwa na hali ya upinzani usiotabirika?).

Kinachofanywa na CUF ni kuwa-assimilate CCM katika serikali ya pamoja ili kupoza joto la kushindwa na kidogo kidogo watazowea na mwishowe watakubali kuwa demokrasia si ugomvi.

Wazanzibar hawana hofu na serikali ya mseto, siku zote mabadiliko ya system iliyooza kwa mda mrefu ni faraja kwa wananchi. Wenzetu Kenya wameondowa system mbovu kwanza na mpaka sasa wamepiga hatuwa kubwa mpaka kubadilisha katiba ukiwatazama kimaendeleo wapo mbali hasa huku wakiwa wamepitwa na Tanzania kwa rasilimali nyingi zisizowafaidisha wananchi wake.

Kama wao hawakuwa na hofu kufanya mabadiliko hayo kwanini Wazanzibari wawe na hofu.
Ukiishi kuamini kuwa bila ya CCM nchi itayumba...ujuwe umasikini, maradhi na ujinga havitapunguwa hata siku moja...!



kwanza pole sana

nataka ujue wewe na maCUF wenzio safari hii mnaangukia pua maana mpaka kwenye ngome yenu kuu Pemba tutachukua viti tena si chini ya vitano

jengine nataka ujue kuwa hadi sasa hakuna mkutano uliofanywa na CUF uliofunika wa CCM popote pale na hilo walijua


bila ya kusita maCUF walitaka serikali ya pamoja kwa kujua weshapoteza mwelekeo na bila ya mtaji huo ndio CUF bye bye

kuhusu upemba na uunguja ni suali lilopandikizwa na viongozi wa CUf kwa uroho wao wa madaraka na hiliinajulikana wazi

kukimbi nchi hili nalo ni viongozi wenu kuchochea vurugu na uhasama na ukitaka kujua jiulize kwa nn Salim Msabah alijiondoa CUf hali akiwa muwakilishi jimbo la Mkunazini?

jiandaeni kuangukia pua ila tutakuliwazeni kwa unakamo na tumeona kufanya hivi ili tuendelee maana nyny mkishindwa tu mnawachochea wananchi wakae vibarazani na kuiga stori baada ya kufanya kazi kuleta maendeleo

nyny mna jadi ya fitna na choko choko na ukitaka kujua tembelea website Mzalendo.net utaona nn hasa nnamaanisha
 
kwa kuenzia kufa kwa CUF inatokana na hawa viongozi wa huku kujiona wao watukufu au bora kuliko hawa wenzao au wanawaita magozi
 
Kwa kipimo hiki, basi CCM ni "BYE-BYE" bara:-

Nimehudhuria kampeni za urais Zanzibar toka uchaguzi wa 1995, 2000, 2005 na sasa huu wa 2010, sijawahi kuona umati mkubwa wa watu kama niliuona leo hapo Kibanda Maiti. Hivyo tathmini yangu binafsi, kama ushindi ni umati wa watu, CCM imeshinda tena kwa
asilimia 90% tena.
 
kwa wale wanao tegemea Chadema kushinda hivi kweli Munaimani na NEC ya Lewis Makame na Kiravu??????????????
 
Pasco mbona umekimbia...njooo uwaambie CCM kuwa chama chao kimeshakufa kule Zanzibar kinasubiri Oktoba 31 kutimiza ada tu!
Naona sasa hata Dr. Sheni anaona uvivu kufanya kampeni...unategemea nini wakati meneja wa kampeni CCM-Z'bar anakuwa Hafidh Ali Tahiri hata darasa la watu wazima hakusoma?

mkuu hivi hafidh ali tahir ndo meneja wa kampeni? huyu ni rafiki sana wa bilal
 
Matokeo ya dodoso hiyo, yanafuatia hivi punde!
Update
Kwanza samahani sana wanabodi, jana nilishindwa kumaliza, nikitegemea ningemalizia usiku kabla sijajala, sasa wengine wetu tukisafiri ndio hivyo tena, kumbe unaweza ukamalizia kazi nyakati za usiku ukiwa home, sio ukiwa safari, Zanzibar nako!...

Matokeo ya Dodoso ni haya.
1.Nilimuuliza mwanahabari fulani aliyehudhuria uzinduzi wa kampeni za CCM na CUF kisiwani Unguja na jana alikuwepo kuhusu wingi wa watu, alikiri kuwa CCM kwa Unguja imeifunika CUF. Hivyo nikafikia conclusion 1. Kama ushindi ni wingi wa watu, basi CCM itashinda.
2. Nikamuuliza hayo magari yalitapakaa hapo, akanijibu, ndio yamesomba watu toka kila kona ya kisiwa cha Unguja, yaani CCM imekodisha magari yote bila kujali ni ya nani, na kugawa fulana kwa wananchi wote bila kujali ushabiki wao, na kwa chini chini nasikia pia wameshikishwa na kidogo dogo cha nauli.
3. Hivyo kuna uwezekano uwingi ule wa watu, sio tuu ni ushabiki kwa CCM au mapenzi yako kwa CCM, bali ni usafiri bute, fulana bure na kidogo dogo lakini siku ya kura, watapeleka yalipo mapenzi yao!.
4. Aliniambia hata mikutano ya CUF, watu hujitokeza kwa wingi kama unavyoona mkutano wa CCM, tofauti ya CUF na CCM, ni kuwa wale washabiki wa CUF hawapewi nauli, hujigharimia kwa mifuko yao, hawapewi fulana na kofia za bure, wala hawalipwi sentano toka CUF ili wahudhurie, hivyo wanahudhuria mikutano ya CUF bila shinikizo lolote. Hawa sasa ndio washabiki wa ukweli wakati wenzao ni washabiki maandazi!.
5. Kama ni kweli CCM imekodisha yale magari yote niliyoyaona jana, kama ni kweli CCM inagawa fulana, kofia, kanga na scuf kwa yoyote, na kama ni kweli, CCM inagawa kidogo dogo kwa hao wahudhuriaji mikutano yake ya kampeni kwa maoni yangu, hii inaweza kuwa ni kiashiria tosha kuwa October 31 kuna uwezekano mkubwa kwa CCM ndio Bye Bye Zanzibar!.

Angalizo: Washabiki wa CCM msinitolee mimacho, haya ni maoni yangu tuu kwa kutumia freedom of expression bila kuingilia mchakato wa uchaguzi, kwani kama hizo hoja ni za uwongo, si mtashinda kwa kishindo! hivyo hakuna haja ya kutoleana lugha kali kali humu!

Washabiki wa CUF pia msijifariji sana na mashabiki wenu ambao ni genuine, kunauwezekano hayo makundi yenu ni washabiki tuu na sio wapiga kura, hivyo jiandaeni kwa matokeo yoyote, sio mnapata kipigo halali na bado mnaendelea kulia lia.
 
Kwa kipimo hiki, basi CCM ni "BYE-BYE" bara:-

Rutashubanyuma na washabiki wa makundi ya watu, msijitabirie ushindi kwa kipimo cha makundi ya watu, wengine ni kweli huenda tuu kushangaa helcopter na wengine kufuata vikundi vya burudani tuu lakini sio wapiga kura!.

Mimi ni mmoja wa waliotangaza mwelekeo wa ushindi kwa Chadema wakati wa uchaguzi mdogo wa Busanda na Biharamulo kutiokana na makundi makubwa ya watu kwenye mikutano ya Chadema, na CCM ilikuwa inatilisha huruma licha ya 'Tingatinga' lao kuongoza mashambulizi, lakini bado Chadema ilifunika mwanzo mwisho!, Matokeo yalipotangazwa, mbona uso ulinishuka!.

Umati usiwe kipimo, kipimo ni commitment na wachezaji haswa wa ile game ya October 31, tusichuuzwe na washangiliaji tuu!. Ndio maana kuna mahali nilisema Online polls karibu zote zinaelekea upande mmoja, ila kumbuka most of online voters ni washangiliaji na watazamaji tuu wa game ya October 31 na sii wachezaji!.
 
Mkuu mkandara,
Naona kama huelewi kwa nini CUF wamekubali serikali ya mseto. Ujuwe CUF haingekuwa na haja ya kukubali kuunda serikali ya mseto kama uchaguzi Zanzibar ungekuwa uhuru na haki na bila ya vurugu na mbinu chafu za CCM.

Ukumbuke kuwa chaguzi zote CCM imeiba kura na matokeo na kusababisha umwagaji mkubwa wa damu. Ukumbuke wao ndiwo wenye dola na vyombo vyake, wao ndiyo waliouwa watu, wao ndiyo waliosababisha wakimbizi (shimoni Mombasa-Kenya), wao ndiyo waliochochea migawanyiko ya U-Pemba na U-Unguja, wao ndiyo waliokuwa tayari kufanya chochote mradi maamuzi ya wananchi yapinduliwe.

CUF, kwa kuona hayo na kutafakari vizuri hiyo hali wameona wabadilishe mbinu ya mapambano, wameona kuwa CCM ni vin'gan'ganizi wa madaraka na hawatakubali kushindwa na wapo tayari kumwaga damu (kama una doubt nukta hii jiulize kwanini JWTZ litowe vitisho katika uchaguzi huu ambao CCM wamekabiliwa na hali ya upinzani usiotabirika?).

Kinachofanywa na CUF ni kuwa-assimilate CCM katika serikali ya pamoja ili kupoza joto la kushindwa na kidogo kidogo watazowea na mwishowe watakubali kuwa demokrasia si ugomvi.

Wazanzibar hawana hofu na serikali ya mseto, siku zote mabadiliko ya system iliyooza kwa mda mrefu ni faraja kwa wananchi. Wenzetu Kenya wameondowa system mbovu kwanza na mpaka sasa wamepiga hatuwa kubwa mpaka kubadilisha katiba ukiwatazama kimaendeleo wapo mbali hasa huku wakiwa wamepitwa na Tanzania kwa rasilimali nyingi zisizowafaidisha wananchi wake.

Kama wao hawakuwa na hofu kufanya mabadiliko hayo kwanini Wazanzibari wawe na hofu.
Ukiishi kuamini kuwa bila ya CCM nchi itayumba...ujuwe umasikini, maradhi na ujinga havitapunguwa hata siku moja...!
Mkuu wangu najua sana CUF wamefanya nini na kama unakumbuka niliwaambieni mnafanya makosa makubwa sana kukubali muafaka kwa faida ya CCM ambao walikuwa wakichukiwa na watu wengi Zanzibar (kama Bara). Na ktk mahesabu ya CCM walijua fika kwamba mwaka huu hawataweza tena kuiba kura kihahisi Zanzibar ushindi ni wa CUF. Hata nguvu ya dola inaweza tu kutumika sehemu moja na sio visiwa vyote. Kushindwa kwa CCM kulikuwa Obvious hakuna hila isipokuwa....

Ndipo walipokuja na hili la Muafaka ili kuondoa chuki ya wananchi kwa CCM ili kuunda umoja na urafiki na CUF hali hakuna urafiki huo..Na leo hii CCM inaonekana kama sii chama kibaya visiwani na wabaya wao wako bara, hali wachawi wapo palepale Visiwani..Na asikwambie mtu ati kwamba hawa viongozi kina Karume, Salmin Amour, Seif Hamad, Bilal na wengineo wanaweza kuungana kuunda kitu kimoja.. Haiwezekani. Na utofauti wao ni wa kiitikadi sio maswala ya uzawa hivyo uongozi hauwezi kukamilika ikiwa itikadi bado zinatofautiana kama ilivyokuwa toka enzi ya Sultan.

Hivyo muafaka wote umeweza kurudisha uhalisia wa CCM visiwani na sasa hivi kuna dalili tosha za CCM kushinda visiwani ambako wao walikupigia mahesabu wakasahau huku bara wakidhania hakuna Upinzani. Lau kama CUF ingeungana na Chadema kwa malengo sawa na hayo ya muafaka na CCM, basi CUF wangesimama nafasi nzuri zaidi kwa kuwepo ktk uongozi wa bara (serikali kuu) na kikubwa zaidi kuongoza Zanzibar bila Ubia (mseto) na chama chochote. Na kikubwa zaidi uwezekanao wa Zanzibar kutambulika kama ni nchi ndani ya Muungano ingetimia pengine mwaka au miaka miwili tu baada ya ushindi. Lakini kwa ujinga wa huyo Seif amekubali kuwa Musolini kuweka muafaka na Hitler kwa hofu isokuwa na Ujasiri wa kusimamia haki ya wananchi wake.

Mara zote nasema kwamba Mpiganaji, mwanamapinduzi yeyote anayesalimu amri na ku shake hands na devil, basi jua fika yeye mwenyewe uatabadilika na kuwa devil.. CUF ni a long run will become devil themselves - Natanguliza SAMAHANI...
 
0 Reactions
Reply
Back
Top Bottom