Kigarama
JF-Expert Member
- Apr 23, 2007
- 2,492
- 1,230
Kama kwenye Orodha ya mambo haya au matendo haya wewe haumo basi jua wewe si fisadi bali ni mtu safi!!!
- Kama hujawahi kununua mtihani ili ufaulu
- Kama kwenye fomu ya maombi ya kupata mkopo wa elimu ya juu hujaandika kwamba wewe kwenu mna nyumba ya Udongo (wakati ya kwenu ni ya matofali tena imeezekwa bati) au wewe ni Yatima wakati wazazi wako wako hai
- Kama hujatoa rushwa ili upate kazi uliyo nayo sasa
- Kama hujachukua hela za mradi unaousimamia na kujengea nyumba au kununulia gari
- Kama unalipa Kodi kwa kila pato unalolipata.
- Kama hutumii madaraka uliyonayo kwa manufaa yako binafsi.
- Kama hujaomba rushwa ili utoe huduma unayoistaili kuitoa kwa mujibu wa kazi yako
- Kama hujaghushi jina unalotumia kupatia ajira
- Kama ulipojenga si eneo la kijamii ila wewe umelipora
- Kama hutumii vifaa vya ofisi ya umma kwa shughuli zako binafsi
- Kama huzidishi thamani ya gharama ya vitu unavyonunua kwa ajili ya ofisi ya umma unayofanyia kazi
- Kama hupati mgao kutokana na ufisadi unaofanywa kwa jamii
- Kama wakati wa kazi za umma wewe uko kwenye supu au shughuli zako binafsi.