Ngandema Bwila
JF-Expert Member
- Sep 8, 2010
- 1,017
- 256
Serikali ya awamu ya nne yenye vyombo vyote vya ulinzi na usalama na Amri jeshi mkuu imejivua wajibu wa kulinda maisha na mali ya wananchi wake na kuibebesha jukumu hilo CDM.
Ni wazi sasa kuwa kila yanapotoke maafa yoyote nchini tutambiwa CDM wamewashiwishi wananchi, kama vile wananchi wamewachia CDM wafikiri kwa niaba yao.
Inawezekanaje serikali yenye wakuu wa wilaya , mashushu, majeshi, polisi (sasa wauwaji wa raia) mawaziri ikamtupia lawama mbunge mmoja tena wa upinzani kuwa amewashawishi watu wajimbo lingine zaidi ya 800 kuvamia mgodi.
kama mbunge mmoja wa chama pinzani toka jibo lingine ameweza kushawishi watu wakafanya uvamizi mpaka wakauwawa na polisi waliopaswa kuwalinda basi huyo mbunge na chama chake wanaushiwishi mkubwa.
Kama wabunge wawili wa CDM toka mbali (Mmoja Toka SINGIDA) wameweza kuwashwishi familia nne tofauti wasizike ndugu zao walio uwawa, wakati kuna mbuge wajimbo hilo, kuna mkuu wa wilaya, RPC,Wapelezi, kuna mkuu wa mkuo na utili wa viongozi kibao ambao tungetegemea watu Wanyamongo wanawaelewa zaidi ya hao wa kuja kina Lisu.hapa inaashiria hatuna serikali kuanzia viji, kata, wilaya na mkoa.
Mtu toka mbali aje kwangu awashawishi wanangu wavamie kile kiduka chetu(mimi na wanangu), wanangu wakubali kuvamia duka nami nichukue panga kuwauwa wanangu nani kichaa? Swali ni je hilo duka ni letu na wanangu? Je hawa ni watoto wangu kweli? Inawezekana ni watoto wa huyo aliyewashwishi na kama ni hivyo sinabudi nimwechie wanae!
Hili ni la Tarime, lakini tumeambiwa CDM walliwashawishi watuwaandamene Arusha polisi wakawauwa watatu, tunambiwa CDM imeshawishi wananchi wavamie mashamba ya wawekezaji Babati.
Swali ni kwamba hawa wananchi walio kaa mkao wa kushawishiwa na kutekekeleza kila wanacho ambiwa na CDM hatawakubali kupoteza maisha yao ni mbumbu kiasi hicho? Au kuna mambo yanafunikwa kwa jina la CDM?
Lakini kwa upande mwingine CDM haohao wamefanya Madamano yanahudhiliwa umati mkubwa wawatu katika mikoa yote ya kanda ya ziwa na Nyanda za juu Kusini bila polisi kuingiliai. Kote huko hatujasikia mtu kakanyagwa achilia mbali kupigwa kibao. Kwa hiyo CDM wamewashawishi wananchi huko kote wasifanye fujo na wananchi wakawasikia.
Inamaana wanachotaka CDM ndicho kinacho fanyika wala si asemacho Rais,Makumu, Waziri mkuu, Mawaziri,wakuu wa mikoa na viongozi wengine .Wamepoteza ushawishi hao.
Sasa kwanini tusiwape CDM nchi kwa sharti moja tu ambalo naamini wanaliweza kutokana na ushawishi wao. Wawashawishi wananchi kuchapa kazi na kusimamia jasho lao kwa ghalama yoyote ile. Nchi Itaenda na sisi tutaanza kutoa misaada kwa nchi zingine badala ya kuwa matonya wa kudumu.
Baba haombi kutambuliwa na wanae maana anajulikana na anasilikilizwa na wote waliokatika himaya yake! Kinyume chake ni matatizo makubwa!
Ni wazi sasa kuwa kila yanapotoke maafa yoyote nchini tutambiwa CDM wamewashiwishi wananchi, kama vile wananchi wamewachia CDM wafikiri kwa niaba yao.
Inawezekanaje serikali yenye wakuu wa wilaya , mashushu, majeshi, polisi (sasa wauwaji wa raia) mawaziri ikamtupia lawama mbunge mmoja tena wa upinzani kuwa amewashawishi watu wajimbo lingine zaidi ya 800 kuvamia mgodi.
kama mbunge mmoja wa chama pinzani toka jibo lingine ameweza kushawishi watu wakafanya uvamizi mpaka wakauwawa na polisi waliopaswa kuwalinda basi huyo mbunge na chama chake wanaushiwishi mkubwa.
Kama wabunge wawili wa CDM toka mbali (Mmoja Toka SINGIDA) wameweza kuwashwishi familia nne tofauti wasizike ndugu zao walio uwawa, wakati kuna mbuge wajimbo hilo, kuna mkuu wa wilaya, RPC,Wapelezi, kuna mkuu wa mkuo na utili wa viongozi kibao ambao tungetegemea watu Wanyamongo wanawaelewa zaidi ya hao wa kuja kina Lisu.hapa inaashiria hatuna serikali kuanzia viji, kata, wilaya na mkoa.
Mtu toka mbali aje kwangu awashawishi wanangu wavamie kile kiduka chetu(mimi na wanangu), wanangu wakubali kuvamia duka nami nichukue panga kuwauwa wanangu nani kichaa? Swali ni je hilo duka ni letu na wanangu? Je hawa ni watoto wangu kweli? Inawezekana ni watoto wa huyo aliyewashwishi na kama ni hivyo sinabudi nimwechie wanae!
Hili ni la Tarime, lakini tumeambiwa CDM walliwashawishi watuwaandamene Arusha polisi wakawauwa watatu, tunambiwa CDM imeshawishi wananchi wavamie mashamba ya wawekezaji Babati.
Swali ni kwamba hawa wananchi walio kaa mkao wa kushawishiwa na kutekekeleza kila wanacho ambiwa na CDM hatawakubali kupoteza maisha yao ni mbumbu kiasi hicho? Au kuna mambo yanafunikwa kwa jina la CDM?
Lakini kwa upande mwingine CDM haohao wamefanya Madamano yanahudhiliwa umati mkubwa wawatu katika mikoa yote ya kanda ya ziwa na Nyanda za juu Kusini bila polisi kuingiliai. Kote huko hatujasikia mtu kakanyagwa achilia mbali kupigwa kibao. Kwa hiyo CDM wamewashawishi wananchi huko kote wasifanye fujo na wananchi wakawasikia.
Inamaana wanachotaka CDM ndicho kinacho fanyika wala si asemacho Rais,Makumu, Waziri mkuu, Mawaziri,wakuu wa mikoa na viongozi wengine .Wamepoteza ushawishi hao.
Sasa kwanini tusiwape CDM nchi kwa sharti moja tu ambalo naamini wanaliweza kutokana na ushawishi wao. Wawashawishi wananchi kuchapa kazi na kusimamia jasho lao kwa ghalama yoyote ile. Nchi Itaenda na sisi tutaanza kutoa misaada kwa nchi zingine badala ya kuwa matonya wa kudumu.
Baba haombi kutambuliwa na wanae maana anajulikana na anasilikilizwa na wote waliokatika himaya yake! Kinyume chake ni matatizo makubwa!