Father of All
JF-Expert Member
- Feb 26, 2012
- 6,376
- 6,708
Tapeli aitwaye Novatus Mutoka na kitabu chake cha "HARAKATI ZA DKT JAKAYA KIKWETE KATIKA KUMUENZI MWL JK NYERERE" mbele ya waandishi wa habari (hawapo pichani) mapema leo ofisini kwake mkoani Dodoma
Kwa wanaokumbuka kitabu cha hovyo cha "Tumaini Lililorejea" kilichoandikwa na Prince Bagenda akijikomba kwa Kikwete ili amkumbuke kama alivyofanya kwa Salva Rweyemamu, wanajua kilichofuatia. Bagenda akiwa msomi lakini mjinga, aliandika kitabu cha sifa za uongo sawa na Julius Nyang'oro ambaye hivi karibuni alikutikana na kashfa ya kughushi.
Naona sasa amejitokeza tapeli mwingine pichani aitwaye Novatus Mutoka ambaye eti ametunga kitabu cha kueleza Kikwete alivyomuenzi Nyerere! Ama kweli akutukanaye hakuchagulii tusi. Kikwete anaweza kumuenzi Nyerere kwa madudu anayofanya?