Kalimanzila ni mkazi wa Kasulu. Baada ya kupigika sana na njaa aliamua kuingia kwenye shamba la mihogo la jirani na kuchimba kiroba kimoja. Kabla hajaondoka mwenye shamba akatokea akiwa na upinde na kumwamuru asikimbie na kushikwa na kupelekwa polisi akiwa na ushahidi mkono. Kesi ilikuwa rahisi sana mahakamani kutokana na kuwepo kwa ushahidi, lakini kabla ya kuhukumu kesi hakimu alimpatia Kalimanzila nafasi ya kujitetea na mazungumzo yakawa kama ifuatavyo:
Hakimu: Mshtakiwa kalimanzila ushahidi upo wazi je una la kujitetea?
Kalimzanzila: Ngo, ndiyo hakimu ninataka kujitetea
Hakimu: endelea
Kalimanzila: ndugu hakimu ngo ninaomba kumuuliza maswali mwenye shamba
Hakimu: endelea
Kalimanzila: Ngo, je nilipokuwa nachimba mihogo shambani kwani ilikuwa lini?
Mwenye shamba: Ilikuwa jumatatu muheshimiwa hakimu
Kalimanzila: Ngo, hola, umekosa!! ilikuwa jumatano!
Kalimanzila: Ngo, je nilipokuwa nachimba mihogo nilikuwa nimevaa shati gani
Mwenye shamba: Jekundu mheshimiwa hakimu
Kalimanzila: Ngo, hola, umekosa!! lilikuwa jeusi
Kalimanzila: Ngo, muheshimiwa hakimu ni hayo tu, ngo nilitaka kuonesha kuwa mwenyeshamba, ngoananisingizia, ngo wote mneona ngo alivyokosa maswali yote, ngo kama alinikamata angejua siku na nguo niliyokuwa nimevaa!
Hakimu: kesi inaahirishwa mpaka itakapotajwa tena kwa ajili ya kusoma hukumu
Hakimu: Mshtakiwa kalimanzila ushahidi upo wazi je una la kujitetea?
Kalimzanzila: Ngo, ndiyo hakimu ninataka kujitetea
Hakimu: endelea
Kalimanzila: ndugu hakimu ngo ninaomba kumuuliza maswali mwenye shamba
Hakimu: endelea
Kalimanzila: Ngo, je nilipokuwa nachimba mihogo shambani kwani ilikuwa lini?
Mwenye shamba: Ilikuwa jumatatu muheshimiwa hakimu
Kalimanzila: Ngo, hola, umekosa!! ilikuwa jumatano!
Kalimanzila: Ngo, je nilipokuwa nachimba mihogo nilikuwa nimevaa shati gani
Mwenye shamba: Jekundu mheshimiwa hakimu
Kalimanzila: Ngo, hola, umekosa!! lilikuwa jeusi
Kalimanzila: Ngo, muheshimiwa hakimu ni hayo tu, ngo nilitaka kuonesha kuwa mwenyeshamba, ngoananisingizia, ngo wote mneona ngo alivyokosa maswali yote, ngo kama alinikamata angejua siku na nguo niliyokuwa nimevaa!
Hakimu: kesi inaahirishwa mpaka itakapotajwa tena kwa ajili ya kusoma hukumu