Kakobe aishukuru TANESCO
na Betty Kangonga
Askofu Mkuu wa Kanisa la Full Gospel Bible Fellowship (FGBC), Zachary Kakobe, amemshukuru aliyekuwa Waziri wa Nishati na Madini William Ngeleja pamoja na Shirika la Umeme Nchini (TANESCO) kwa kutumiwa na Mungu kupitisha umeme juu ya kanisa hilo hatua iliyochangia kuwa na maono makubwa.
Akizungumza wakati wa kuzindua tovuti mbili za kanisa hilo juzi, Askofu Kakobe, alisema kuwa hatua ya serikali kupitisha umeme katika eneo hilo imempa changamoto zaidi katika kuhubiri Injili ulimwenguni, kupitia tovuti hizo za intaneti ambayo itaangaliwa na watu wengi zaidi kuliko ilivyokuwa kwa televisheni ya Holiness ambayo ingetazamwa na watu wachache.
Hata hivyo, alidai pamoja na kupitisha umeme juu ya kanisa lake lililoko Mwenge, jijini Dar es Salaam, hadi sasa hakuna nguvu ya umeme inayopita katika nguzo hizo namba 19 na 20, na kuwa kama umeme ulishindwa kupita katika makaburi ya machifu mkoani Iringa hata katika nguzo hizo hautapita kwa kuwa Mungu anayemhubiri ni zaidi ya hao machifu.
Askofu Kakobe aliingia katika mgogoro na TANESCO baada ya serikali kuruhusu upitishwaji wa umeme wenye msongo wa kilovoti 132 mbele ya kanisa hilo.
na Betty Kangonga
Askofu Mkuu wa Kanisa la Full Gospel Bible Fellowship (FGBC), Zachary Kakobe, amemshukuru aliyekuwa Waziri wa Nishati na Madini William Ngeleja pamoja na Shirika la Umeme Nchini (TANESCO) kwa kutumiwa na Mungu kupitisha umeme juu ya kanisa hilo hatua iliyochangia kuwa na maono makubwa.
Akizungumza wakati wa kuzindua tovuti mbili za kanisa hilo juzi, Askofu Kakobe, alisema kuwa hatua ya serikali kupitisha umeme katika eneo hilo imempa changamoto zaidi katika kuhubiri Injili ulimwenguni, kupitia tovuti hizo za intaneti ambayo itaangaliwa na watu wengi zaidi kuliko ilivyokuwa kwa televisheni ya Holiness ambayo ingetazamwa na watu wachache.
Hata hivyo, alidai pamoja na kupitisha umeme juu ya kanisa lake lililoko Mwenge, jijini Dar es Salaam, hadi sasa hakuna nguvu ya umeme inayopita katika nguzo hizo namba 19 na 20, na kuwa kama umeme ulishindwa kupita katika makaburi ya machifu mkoani Iringa hata katika nguzo hizo hautapita kwa kuwa Mungu anayemhubiri ni zaidi ya hao machifu.
Askofu Kakobe aliingia katika mgogoro na TANESCO baada ya serikali kuruhusu upitishwaji wa umeme wenye msongo wa kilovoti 132 mbele ya kanisa hilo.